Lafudhi

Swts

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2012
Posts
3,062
Reaction score
1,294
>Nini chanzo cha lafudhi?
>Kwanini lafudhi ya watu wa mkoa fulani hutofautiana na mkoa mwingine?ilhali tu nchi moja
Mfano,wamakonde,wachaga,wapemba,wazaramo,wangon, wanalafudhi tofaut kabisa,kwanin,nin tatizo ama tuseme chanzo
 
hii hutokana na lugha mama ama lahaja ya mtu anayozungumza. sio kwenye kiswahili pekee, mfano : wataliano wa Napoli hawatamki sawa na wataliano wa Milan
Tanzania ni moja ila haina kabila moja ...kumbuka hilo
Kiswahili ni lugha moja ila ndani yake kuna lahaja nyingi sana, na kila lahaja ina namna yake ya kutamka. mfano watu wa tanga na mombasa wanafanana kiasi kimatamshi. Dar na Unguja pia hufana kiasi fulani.(kwa kuwa Dar ni mji kubwa na kuna watu wa makabila mengi ,kwa hiyo pana mchanganyiko wa lafdhi)
 
Mtu kitu,dah asante man..kwel umejaa vitu kama hivyo sasa..
 
>Nini chanzo cha lafudhi?
>Kwanini lafudhi ya watu wa mkoa fulani hutofautiana na mkoa mwingine?ilhali tu nchi moja
Mfano,wamakonde,wachaga,wapemba,wazaramo,wangon, wanalafudhi tofaut kabisa,kwanin,nin tatizo ama tuseme chanzo

Athari ya lugha ya kwanza-au lugha mama ndio hufanya kuwepo na lafudhi mbalimbali. Na tofauti hizi zitaonekana tu pale wazungumzaji wenye lugha mama tofauti wanapozungumza lugha ambayo si yao kwa asili.
 
Athari ya lugha ya kwanza-au lugha mama ndio hufanya kuwepo na lafudhi mbalimbali. Na tofauti hizi zitaonekana tu pale wazungumzaji wenye lugha mama tofauti wanapozungumza lugha ambayo si yao kwa asili.
Mkuu ndo wewe ninaye kufahamu?
 
mie naona lafudhi inatokana na mazoea yanayorithishwa toka kizazi hadi kizazi, hii inatokana na hali ya jamii ilivyo mfano wamarekani lugha yao ni ya mkato mkato haraka na jazba iliyojificha.
ingawa ni kiingereza kile kile jamaika pia wanakaribiana nao ingawa jamaika wamezidi ilitokana na kutokuelewana ambapo watu mara nying waliongea kwa kubishana na kurushiana maneno. tukiangalia watu wa mwambao walipata lugha laini kwa vle hawakuwa wafanya kaz ngumu pia waliishi maisha mazur kukaza kwa herufi imepatikana maeneo ya kaskazini kujionesha kuwa wao ni mashujaa hata kupitia sauti angalia hata wazulu wakiongea urithi wa hz lafudhi toka kizazi hadi kizaz umetufikisha hapa leo na ndio maana unakuta kuna watu wana lugha laini za kukaza za mkato na za kutirika na nyingne charehani watu wa vijiji kama bungu na maeneo kuizunguka rufiji na baadhi ya watu wa badgamoyo kifupi vijiji vya jirani na dar kupita coment nahs utafikiri beyound the ordinary.
nahs lugha mama sio 7bu ya kuzuka kwa lafudhi
 
angalia watu wa dar wamezimaster lafudh za mikoa na lugha zote h inatokana na wao walirithishwa kila lafudhi leo h mtu wa dar anaweza kupretend upemba uchaga hata umakonde na akaweza ila hawez kutirika (cherehani) kama mkolesa hii ni kwa sababu mkolesa amekimaster kiswahili peke yake hvyo ni mtu ambaye anaongea faster hapa tz cjawaona mfanowe
 
Mambo yasiasa za propaganda yameshika hatamu sana, hii imepelekea watu makini ambao zamani walikuwa wanatoa michango maridadi kulikimbia jukwaa.

Mi nafikiri hoa ndo wanatakiwa walishape jukwaa, kukimbia inamaanisha wamekubali kushindwa?
 
>Nini chanzo cha lafudhi?
>Kwanini lafudhi ya watu wa mkoa fulani hutofautiana na mkoa mwingine?ilhali tu nchi moja
Mfano,wamakonde,wachaga,wapemba,wazaramo,wangon, wanalafudhi tofaut kabisa,kwanin,nin tatizo ama tuseme chanzo
Kitaaluma tungesema hivi:

Lafudhi ni matamshi ya msemaji wa lugha fulani ambayo yanatokana na athari za kimazingira. Mazingira hayo yanaweza kuwa eneo atokalo mtu, mahali alikosomea, kiwango chake cha elimu, tabaka lake la kijamii na kadhalika.

Kwa hiyo hapa chanzo kikubwa cha lafudhi ni mazingira alimo huyo mtumiaji lugha, mazingira hayo ni kama yalivyotajwa hapo juu. Lugha mama pia inaweza kuwa chanzo cha lafudhi tofautitofauti, kwa mfano katika kiswahili, hawa watu wakizungumza wazungumzaji wa kiswahili watajua wanatoka mkoa gani au ni kabila gani:


  1. Usiniretee maswara ya ubaguzi wa kikabira hapa
  2. Amemupiga mutoto ya watu juu amemuibia mfaranga makumi mawili
  3. Ukikaa nchale, ukichimama nchale
  4. Wewe unakamuaga mang'ombe tu moja kwa moja
  5. Mbona unakuwa kinganganizi, nilishakwambia sikupendi lakini wewe bado unaningangania tu!
Lafudhi sio kitu kibaya, lakini pia huweza kubadilika kwa kutambua au bila kutambua (hii inaweza kutokea hadi umri wa miaka ishirini na). Lakini chanzo kikubwa cha lafudhi ni mzaingira alimo huyo mzungumzaji.
 
Mi nafikiri hoa ndo wanatakiwa walishape jukwaa, kukimbia inamaanisha wamekubali kushindwa?

Hili jukwaa ni 'user generated', yaani watumiaji ndio huamua nini kiwepo humu kwa kuwa wao ndio waandikaji. Sasa unakuta mtu anatoa hija za msingi, mwingine anakuja kunanga na hoja za kantangaze, kama unavyoona Bunge la Muungano. Katika hali hiyo mtu na akili zake anaona bora alisuse jukwaa tu...
 

Nimeipenda no. 2 ambayo ni ya Kongo Mashariki...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…