LAT, Voice of a Reason, Malila, Ameoba na wengine wengi...

Nimependa idea hii,
tatizo langu hatujuani hata hapo dar mnakutania wapi? Nataka ku join nanyi
 

Mkuu Mbegu Bora huanza na Jogoo,nashauri mchukue kuchi ,mimi nitakuja kuchukua mayai.

Umedokeza Segeara,hivi bei ya Ardhi kwa heka ni kiasi gani kwa sasa,kwani kila nikipita Segera huwa napatapani. utadhani Las Vegas ilipokuwa ikianzishwa Flamingo Casino.
mkuu karibu ktk vikao vya JE Saccos
 
Mlachake,LAT,Malila,Voice of Reason,
hizi character/Personalities huwa zinanipa Raha sana moyoni kwangu na smiles Lukuki ,Ubavu wangu huwa anielewi na kuniona chizi nikismile mbele ya laptop.Amesema weee ,amelalamika wee amechoka ,kwani JF ni zaidi ya uijuavyo. huwa nasoma hizi Thread usiku nikifika home, nikiwa nakaribia kulala.

Hawa watu kichwani kwangu nimewa Class hivi:
LAT - Action Plan(JE)
Malila- Implementation(you Can Always Count on this Guy)
Voice of Reason - Critical Anaylisis
Mlachake- Ideas Tu(yeye Anakula Vyake- Avatar yako huwa haifichi)
New Mzalendo - Mh.hapa mnaonijua mnajua( sometimes i think i am all of the above)

TAFADHALI NAMI NIPO KTK MRADI WA MBUZI FARM. (MEMBER No.5)

Mkuranga kuna Ardhi. 55Km from City center. 14Km from Mkuranga Center(NMB Bank).ntaleta Satelite location
NinaArdhi nzuri tu.mkikagua na kuonekana inafaa. nitakodisha mradi kwa MIAKA 10. kwa Kodi ya Dola 5/acre kwa mwaka,kwa Rent Increment of 15% kila mwaka.
Narudia Dola TANO 5USD /year.
Nipo Tayari kukodisha 10Acres

 

NM

I commend your tireless contribution to this subforum, you have always been a tool towards an array of entrepreneurship endevours and yes you are a true patron, i can not think or read anything from you except encouragement and moral support plus a character of forefront actions

je eneo hilo lina maji au karibu na hapo kuna maji?
je soil ya huko ni ya aina gani?
je uwanda wa maeneo hayo kuna uwezekano wa malisho ya mbuzi yaliyo karibu?
je kuna uwezekano wa kufanya manunuzi ya stock za mbuzi at around the vicinity?
je security ikoje
how is the availability of labour?
are there any opportunities za ku expand project (land)

je unaonaje tukuvue eneo kabisa?
 
Nimependa idea hii,
tatizo langu hatujuani hata hapo dar mnakutania wapi? Nataka ku join nanyi

Ndio tayari umeshajiunga,
Cha msingi tiririka na hii thread mpaka utaona kibao kimeandikwa hapa kuna mkutano wa kwanza, basi ingia utatukuta.
 

Bei za Tanga si mbaya kama Dar, kuna mjuba mmoja anatokea mitaa ile nitamuuliza ili nijue.

Niko nje ya Dar mkuu wangu, ningefika nihudhurie vikao, nikifika Dar inabidi zile milioni za watu niziingize shambani, na msimu ndio huu. Au wewe nikuache kule ?
 
Nami nimo,
What to do then??!!!

Jitayarishe,
mara baada ya kupata idadi tarajiwa, tunaanza shughuli rasmi. Mi naamini tukigawana majukumu itakuwa rahisi sana kufikia malengo. Kwa sasa tunahitaji yafuatayo kwa pamoja; members ( tayari wapo na wanaongezeka), ardhi nzuri kwa ajili ya wazo letu na fedha.Kwa hiyo viongozi wa muda ni muhimu wawepo ili maswali kama haya ya akina Shark yapate majibu moja kwa moja.
 

Toa majibu kwa LAT ili tusonge mbele wadau.
 
Kuna njia hii nzuri sana inaweza kutusaidia,
kiingillio kiwe ni kila mmoja wetu kununua eka moja ya ardhi mahali tutakapokuwa tumepata, kwa hiyo kama tutapata eka moja kwa laki tatu,kila mjumbe atatoa 330,000/, hii 30,000/ ni ten percent ya kijiji husika.

Nimetoa bei hizi kama tutanunua ardhi ya kijiji huko Msorwa au Shungu pale Mkuranga. Ni kilomita 16 toka Mkuranga wilayani njia ya Kisiju. Eneo laweza kupanuka mpaka eka 1000, lina maji ya kutosha mwaka mzima, udongo ni wa kichanga na baadhi ya maeneo ni mweusi, pale Shungu ni udongo mweusi na pana kijito cha mwaka mzima(Manundu/Kasopa walishafika).

Usafiri upo wa daladala toka Mbagala mpaka huko. Ni mapori yasiyo na watu wanaoishi pamoja, mpaka sasa usalama wa mifugo ni mkubwa kwa sababu kuna jamaa wachache wana mifugo hapo karibu. Tunaweza kupata mbuzi toka Ikwiriri, visiwa vya Pombwe au kisiwa cha Kruti. Kisiwa cha Kruti kipo karibu zaidi kuliko Pombwe.Muhoro/Somanga kuna mbuzi wa kutosha na usafiri kwa sasa ni mzuri.
 

mkuu

umetoa data zenye uono wa utekelezaji, kikubwa hapa ni umoja wetu, kwa bei hiyo, hata tkianza watu watano kwa sasa na tukaendelea kupokea wengine mpaka tutimie idadi, mimi nadhani ninaunga mkono hoja yako na hivyo basi tunaweza kuanza muda wowote ule bila kusubiri tutimie idadi

wajameni kwa wenye nia tukanyage twende
 
Kwa sasa nina uhakika na Nm, LAT,VOR,Shark, Mapinduzi, Zion Train, Kasopa,Mihayo,dada mmoja( kani-PM), mimi, sijui shemeji yangu Manundu kama atatia timu au la, nina hakika tunaweza kuanza bila kuchelewa.

Mawazo yangu, ni kwamba, ni vizuri mbuzi wa kwanza wafike pale kabla ya masika.
 

Poa wakuu tufanye cost breakdown ya hizo hekari na mabanda ya mwanzo kama ni fence au nini ili tujue vizuri....

Katika pita pita zangu pia nimeona hii (Raising Goats for Meat)
http://extension.umd.edu/publications/PDFs/FS816.pdf

This might be the begging of something good 🙂

Tena kama ardhi ni kubwa tunaweza tukawa tunatenga maeneo ya free grazing mbuzi wanakula hapa wakati pale majani yanaota alafu pale tena by the time hapa wameshamaliza kula pale pa mwanzo yameshaota tena hususan kama ardhi ni bei raisi
 

Naomba tufanye hivi, tununue shamba kwanza kama awamu ya kwanza, pili tunajenga banda zuri dogo kwa ajili ya farm manager, tunanunua mbuzi kama 20 wa kuanzisha kijiwe(hiki ndio kipindi cha kujichuja sisi wenyewe kwa njia ya vitendo). Baada ya hapo watalaamu wa miradi wataanza kuweka mambo ktk makaratasi rasmi, idara ya fedha wakitengeneza vitu vyao, wa operation wanaendelea na watu wa marketing wakianza kupanga mikakati ya kuliingia soko.
 
Majibu yako hivi

je eneo hilo lina maji au karibu na hapo kuna maji?= kuna mto,ila mwaka huu umekauka
je soil ya huko ni ya aina gani?= mfinyanzi na kichanga kidogo
je uwanda wa maeneo hayo kuna uwezekano wa malisho ya mbuzi yaliyo karibu?= malisho mazuri sana,kuna wasukuma wanahamia kula kukicha kulisha ng'ombe
je kuna uwezekano wa kufanya manunuzi ya stock za mbuzi at around the vicinity?= hapana ,ila tunaweza kupata from kilwa
je security ikoje= security nzuri
how is the availability of labour?= Mbaya Sana,watu wa mkuranga si wachapa kazi
are there any opportunities za ku expand project (land)= mh!yes majirani wapo wa kununulika mostly they own 10 to 20Acres though there are newcomers every month

je unaonaje tukuvue eneo kabisa?= MKUU kulivua Gamba la umiliki HAPANA kwani nina kishamba chenyewe ni 25Acres only


Proposal ya Malila kuhusu land ni nzuri,nilishawahi kuitembelea.Nashauri tununue As a Single Community land for the project.kila member atatoa 1million as a seed money.
tukiwa members 20 hiyo ni 20million,siyo pesa ndogo kwa shamba la mbuzi.nimepiga hesabu ya fasta fasta kuwa kila mwaka nikipata mbuzi 4 free kwa ajili ya matumizi binafsi.after 3years ni mbuzi 12 ambao ni sawa na 1mil.niliyotoa,plus the value of community and networking bado inanilipa.
ukizingatia tutakuwa tunapromote organic farming
 
Wakuu nimekuwa nafuatilia michango yenu kwa karibu kwa kweli ni mawazo mazuri na nadhani ni muda muafaka wa kuyatekeleza tuliyoandika kwa vitendo.

Wazo la mbuzi ni zuri sana na mimi naunga Mkono.

Mkuu Malila....ninaomba nishirikishwe kwenye mipango yote na nitakuwa tayari kuchangia. Japo mara nyingi nakuwa mbali but please count on me ...will be there kila nikiitajika (nita kuPM kwa maelezo zaidi)

Ahsanteni
 
Wakuu, plz count me in kwenye hiyo project. Mimi na business partner wangu ambae ni member humu. Tutatolea kwenye kikao. Kama ikionekana vyema naweza kumualika na prof mmoja dr wa mifugo ambae ni member humu pia. Ataweza kutoa ushauri juu ya technical issues bure kama member. Very good ideas.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…