Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Mamlaka ya Serikali ya Baraza la Ushauri Watumiaji Usafiri Ardhini - LATRA CCC (LATRA Consumer Consultative Council) imeanza kufanya utafiti na kuchukua maoni ya Wananchi na Wadau wengine kuhusu matumizi ya Kadi za Elekroniki zinazotumika katika usafiri wa Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka, Dar es Salaam (DART) maarufu kwa jina la Mwendokasi.
Ikumbukwe Septemba 2, 2024, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa alizindua kadi hizo na kusisitiza matumizi sahihi ili kusaidia kurahisisha huduma.
LATRA CCC imesema inapokea mtazamo wa Wadau juu ya matumizi ya Kadi ya Mwendokasi katika huduma za mabasi za BRT Jijini Dar es Salaam.
Taarifa ya LATRA CCC imeeleza “Tunaomba utumie dakika chache kujaza fomu, maoni yako ni muhimu katika kuboresha huduma za usafiri ardhini. Tafadhali jaza fomu kupitia Link hii:
ee.kobotoolbox.org
Ilivyokuwa siku ya Uzinduzi wa Kadi Septemba 2, 2024
Kabla ya uamuzi wa Serikali kisisitiza matumizi ya Kadi kwenye usadfiri huo, mara kadhaa Wadau wa JamiiForums.com waliwasilisha malalamiko yao kuhusu usumbufu wa matumizi ya fedha taslimu (cash) ambapo wengi wao walidai kuna changamoto ya utoaji 'chenji' kutoka kwa wahudumu, huku wengine wakidai Wahudumu wamekuwa na michezo ya upigaji kutokana na mfumo wa cash.
Kusoma Wadau zaidi kuhusu kero zao, bofya Link chini
~ Nakerwa na tabia ya wakata tiketi wa Mabasi ya Mwendokasi kudai hawana chenji kila siku
~ Mabasi ya Mwendokasi: Hili suala la mimi nakudai chenji wewe unanipa vocha ya VODA, kuna nini hapa?
~ Bila kadi sasa hupandi Mwendokasi. Waziri Mchengerwa awataka DART kutoa fursa Kwa Watanzania kuwekeza kwenye Mwendokasi
~ Wahudumu mabasi ya Mwendokasi wanatoza nauli zaidi ya iliyopangwa kwa kisingizio cha kukosa chenji
~ Serikali iamue moja; nauli ya Mwendokasi iwe Tsh. 700 kamili au 800
Ikumbukwe Septemba 2, 2024, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa alizindua kadi hizo na kusisitiza matumizi sahihi ili kusaidia kurahisisha huduma.
Licha ya uzinduzi huo baadhi ya Wadau wameonekana bado wakisuasua kutumia Kadi hizo katika huduma ya Mwendokasi, hivyo, upande wa LATRA CCC imeamua kukaribisha watumiaji wa usafiri huo kutoa maoni.LATRA CCC imesema inapokea mtazamo wa Wadau juu ya matumizi ya Kadi ya Mwendokasi katika huduma za mabasi za BRT Jijini Dar es Salaam.
Taarifa ya LATRA CCC imeeleza “Tunaomba utumie dakika chache kujaza fomu, maoni yako ni muhimu katika kuboresha huduma za usafiri ardhini. Tafadhali jaza fomu kupitia Link hii:
Enketo Express for KoboToolbox
Ilivyokuwa siku ya Uzinduzi wa Kadi Septemba 2, 2024
Kusoma Wadau zaidi kuhusu kero zao, bofya Link chini
~ Nakerwa na tabia ya wakata tiketi wa Mabasi ya Mwendokasi kudai hawana chenji kila siku
~ Mabasi ya Mwendokasi: Hili suala la mimi nakudai chenji wewe unanipa vocha ya VODA, kuna nini hapa?
~ Bila kadi sasa hupandi Mwendokasi. Waziri Mchengerwa awataka DART kutoa fursa Kwa Watanzania kuwekeza kwenye Mwendokasi
~ Wahudumu mabasi ya Mwendokasi wanatoza nauli zaidi ya iliyopangwa kwa kisingizio cha kukosa chenji
~ Serikali iamue moja; nauli ya Mwendokasi iwe Tsh. 700 kamili au 800