LATRA yafungulia mabasi 38 ya kampuni ya New Force kuanza safari za usiku

LATRA yafungulia mabasi 38 ya kampuni ya New Force kuanza safari za usiku

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Haya wenye Mbeya Yao haooo wamerejea na ratiba ya saa tisa na kumi na Moja usiku baada ya Kumalizia kifungo Cha LATRA.

Ni kama tuu Newforce walikuwa likizo ya services

=======

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imerudisha ratiba na leseni za mabasi 38 ya kampuni ya New Force kuanzia tarehe 11 Septemba, 2023. Mabasi hayo yataanza safari zake muda wa 9.00 usiku na saa 11.00 alfajiri.

Latra.PNG


Zaidi soma: Basi 38 za new force zapigwa stop na LATRA kusafiri usiku, kuanza huduma saa 12 asubuhi
 
Haya wenye Mbeya Yao haooo wamerejea na ratiba ya saa tisa na kumi na Moja usiku baada ya Kumalizia kifungo Cha LATRA.

Ni kama tuu Newforce walikuwa likizo ya services

=======

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imerudisha ratiba na leseni za mabasi 38 ya kampuni ya New Force kuanzia tarehe 11 Septemba, 2023. Mabasi hayo yataanza safari zake muda wa 9.00 usiku na saa 11.00 alfajiri.

View attachment 2743821

Zaidi soma: Basi 38 za new force zapigwa stop na LATRA kusafiri usiku, kuanza huduma saa 12 asubuhi
Ngoja tuone
 
Yaani kila nikisoma habari za New Force, nawazia ajali ajali.
 
Rushwa wanakula vigogo kufa wanakufa wasio na hatia.
Asiyejua tabia ya magari ya NEW FORCE Ni Nani?
LATRA WANA FORCE AJALI.
 
Wameanza kuona vizuri gizani/usiku hao madereva wa New Force?Wawanunulie miwani maalumu kama zile za oparesheni maalumu ili kuona vema gizani.
 
Mwandishi Wetu, Dar es salaam

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka udhibiti Usafiri Ardhini, C.P.A, Habibu Suluo akiwa sambamba na Kamanda wa Trafiki, SACP, Ramadhan Ng'anzi, wameeleza kuwa kati ya Mabasi 759, yaliyokamatwa, Mabasi 723 yalipewa onyo na mengine 36 yamesitishiwa leseni zao.



Wakizungumza na Vyombo vya Habari wametolea ufafanuzi na kubainisha sababu ya Mabasi hayo kukamatwa, kufungiwa leseni na mengine kupewa onyo ni ukiukwaji wa sheria na kanuni za barabarani hali inayohatarisha usalama kwa abiria pamoja na mali zao.

Maamuzi hayo yanatokana na tathimini ya mamlaka ya usimamizi iliyofanywa na (LATRA), ikiwa imepita mwezi mmoja tangu Serikali iruhusu safari za Mabasi kwa saa 24, huku ikishuhudiwa ukiukwaji mkubwa wa sheria na kanuni za barabarani kwa baadhi ya makampuni.

Kutokana na ukiukwaji huo jumla ya mabasi 759, yalikamatwa na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA), kwa ushirikiano na kikosi kazi cha usalama barabarani, kwa makosa ya kuchezea mfumo wa VTS, unaodhibiti na kutoa taarifa za kasi ya gari pamoja na kudhibiti mwendokasi.

Suluona na Ng'anzi wamesema ''Mabasi yaliyositishiwa leseni kurejeshewa ni mpaka pale Mamlaka itakapojiridhisha kuwa wamebadilika ni 36, kati ya mabasi 246 ambayo ni sawa na asilimia 80, mabasi 1997 yamebainika yameendeshwa kwa mwendokasi kati ya km 86 hadi 89 kwa saa huku asilimia tisa yakiendeshwa kwa km 90 hadi 103 kwa saa''.

Wameendelea kwa kufafanua kuwa madereva 10, wamefungiwa kwa kuchezea mfumo tangu safari za masaa 24 kuanza octoba mwaka huu, lakini taarifa imeonyesha walioandikiwa faini kwa makosa ya mwendo kasi ni 666, waliofikishwa Mahakamani ni 32 na walioonywa ni 50.

Hata hivyo dereva atatakiwa kuomba kufunguliwa na ofisi ya Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani na kabla ya kufunguliwa atalazimika kutahiniwa ili kupimwa uwezo wake kwenye taaluma ya udereva, mara baada ya kumalizia kutumikia adhabu yake na ikiwa atafaulu atarejeshewa madaraja ya leseni yake kama atatetea sifa ya kuendelea kumiliki madaraja hayo.
 
Back
Top Bottom