Lazaro Nyalandu: Nitapeleka muswada binafsi kurudisha mchakato wa katiba ya Warioba ili tupate katiba mpya

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2012
Posts
4,572
Reaction score
26,885
Anaandika Mh Mbunge: Lazaro Nyalandu

NAKUSUDIA kuwasilisha kwa SPIKA wa BUNGE, Mh. Job Ndugai, Mb., AZMA yangu ya kuleta MUSWADA binafsi wa SHERIA katika KIKAO kijacho cha BUNGE itakayoweka SHARTI la kurejea UPYA mjadala wa KATIBA MPYA ya Tanzania, kwa KUZINGATIA RASIMU ya KATIBA kama ilivyowasilishwa na TUME ya JAJI WARIOBA. (Lazaro S. Nyalandu, Mb., Singida Kaskazini-CCM).
(Pichani, nikiwa Kijijini Mgori, [HASHTAG]#SingidaKaskazini[/HASHTAG], jana wakati wa hafla ya sherehe za Mahafali ya Kidato cha IV, Sekondari ya Mwanamwema Shain)

[HASHTAG]#PrayForTunduLissu[/HASHTAG]
 
Nyalando nadhani anaelekea kurukwa na akili.
Mchakato ulifikia hatua ya kupiga kura ya maoni,na waliopitisha kwa wingi ni wao wabunge,simuelewi anavyotaka kurudi reverse,kisheria tunangoja tu kura ya maoni.
Ni kura ya hapana tu itarudisha upya mchakato,Nyalando usitake kutuharibia nchi kisa tu umenyimwa uwaziri,mbona hukusema haya wakati unauza vitalu
 
Safi sana Mh. Nyalandu. Tunataka watu wa aina yako muongezeke mjiunge na kaka wa Taifa Lissu ili tuikomboe Taifa hili la Mwl. Nyerere ambalo kwa kweli linahitaji ukombozi.
 
Huyu nyalando ameanza kujitambua
 
Hata mimi nashangaa hilo. Mchakato umefikia kwenye kupiga kura, labda angehamasisha watu ikifika wakati wa kura wapige ya kuikataa huku akiwaleza sababu ya kukataa huko. Au apiganie mchakato mzima ufutwe uanze upya.
 

Wale Wamarekani wake naona hawakati tamaa.
 

Hatuhitaji kura ya maoni kwa Katiba pendekezwa ambayo kimsingi haina maana yeyote. Ni kupoteza fedha bure. Mchakato wa kuipitia Katiba Upya uanze tukiongozwa na maoni ya wananchi yaliyomo kwenye Muswada wa Katiba maarufu kwa jina la Warioba.
 
Anajitambua ile ya warioba ndio ilikuwa yenyewe. Yenye mawazo ya watanzania sio maccm. Alafu kingu ameacha imani na kukimbilia unafiki wakati kanisa alilopo linawashep sana waumini yeye anaboa kuliko wabunge wote. Hatari sana. Tunakuombea sana Nyarandu now unajitambua . zaidi nawaombea Nape nauye ,Bashe, wekeni tinted kwenye magari yenu maana maoni yenu haya ni mwiba mkubwa sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…