Lazima wewe uwe kama chujio tena chujio la umakini kuchagua yupi wa kuwa nae karibu

Joined
May 2, 2018
Posts
20
Reaction score
27
Nikuumbushe kitu kimoja ndugu yangu, ni lazima maisha yako uwe kama chujio tena chujio la umakini kuchagua yupi wa kuwa nae karibu au kubaki nae katika safari yako ya mafanikio kwasababu hakuna anayeweza kukupiga kofi akiwa mbali na wewe na wala hakuna mtu anayeweza kukuambukiza mafua akiwa mbali na wewe.

Yule ambaye unaamua kuwa nae karibu ndiye ambaye anaweza kupiga kelele za kukupa moyo au kukukatisha tamaa katika mwelekeo wowote ambao atakuwa anaona unao katika maisha yako.
 
Kiongozi umetumia fasihi ngumu kidogo. Sijakuelewa kwa mbaali unamaana gani au ulitaka kumanisha nini
 

Nimekusoma
 
Kwa lugha nyepesi kufanikiwa kwako kunategemea sana aina ya watu uliokaribu nao.
Hali kadhalika kwenye anguko lako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…