Le Mutuz ashindwa kuhudhuria mazishi ya Dkt. Mwele mkoani Dodoma

Ruwamangi

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2020
Posts
1,292
Reaction score
2,382
King of All Social Media Bongo! William Malecela na ndugu wa Karibu wa aliyefariki nje ya nchi kwa Saratani Dr. Mwele Malecela, ameshindwa Kufika nyumbani Mvumi kwa kile alicho Dai Afya yake Haikumruhusu baada ya kuwasiliana na dr wake.

Mfanyabiashara huyo maarufu bongo na mwanamitandao amesikitishwa kwa maneno ambayo yamekuwa yakizunguka kumhusu yeye kutokushiriki Mazishi hayo ya Dada yake.

Alichokisema...

 
Huyu jamaa kukaa nje muda mrefu naona kulimjengea katabia fulani ambacho ni kagumu sana kukubalika kwa wazawa, inawezekana hili ndio tatizo lililomfanya asiende kuzika kwa kuogopa maneno ya watu.
 
"Mfanyabiashara huyo maarufu bongo na mwanamitindo..."

Naomba kujua anafanya biashara zipi mpaka awe maarufu kwa hizo. Na mitindo anafanyia wapi
 
Kuna watu wanamfatilia sana le mutuz kutwa kujigeuza mahakimu wa maisha yake mbona kwenye msiba wa mama yake hawakuuliza kwann ndugu zake wengine hawakwenda kumsaidia.

Jamaa kaumwa sana mwili wote umeporomoka ila hawaoni wanachotaka afanye wakitakacho wao aiseee
 
Tena wakawa wanamcheka eti mama yake anaishi kwenye nyumba mbaya!

Kuna watu wanapenda sana kufuatilia maisha ya watu utadhani wanapata ujira.
 
Huyu lemutuz anamiaka 60+ lakin uandishi wake utasema kachalii kenye miaka -25 yaani utoto mwingi anajisifu balaa.
Watoto wa kishua huwa hawakomai kiakili muda wote wanajiona watoto tu
 
Hata mimi nilishangaa sana kumuona pale kwenye mjengo wake wa kifahari karibia na mnazi mmoja wakati shughuli ikiendelea.

Ila to be honest anaonekana kabisa ni mgonjwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…