Le Poet Simaro Lutumba astaafu Muziki leo 19.03.2018 akiwa na Miaka 80

Le Poet Simaro Lutumba astaafu Muziki leo 19.03.2018 akiwa na Miaka 80

Masiya

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
7,602
Reaction score
7,332
Lutumba-Simaro-3.jpg

Nyota wa Muziki wa Rhumba (DRC) Mzee Simaro Lutumba (Micra Jazz 1958, Congo Jazz 1959/60, TP OK Jazz 1961-1993, Bana OK 1994-2018) wiki hii anastaafu kupiga muziki (umri na matatizo ya miguu). Atakuwa na maadhimisho 3.

Leo Jumatatu, March 19, 2018 atakuwa at Dancing bar 1,2,3 at Mama Kulutu, Alhamisi, March 22, ni Kamina street No. 24, Yolo North. Ijumaa March 23, Lutumba Simaro atapiga show yake ya mwisho ShowBuzz Hall iliyoko Colonel Mondjiba Avenue, Ngaliema Commune.

Simaro ni mpiga rythm mashuhuri wa OK Jazz na Bana OK, kwa wajuvi wa mambo huyu pia alikuwa mwalimu ndani ya OK Jazz kuanzia vijana wakina Youlou (1966) hadi wakina Malage de Lugendo (1980's). Lakini sifa yake kubwa ni katika utunzi-mfano ni Maya (iliyoimbwa na Carlyto Lassa), Mabele (iliyoimbwa na Sam mangwana), Dati Petroli (aliyoimba Madilu), Mbongo, Mandola, Kadima (alizoimba Djo Mpoyi) na utitiri wa record ambazo Josky Kiambukuta aliongoza waimbaji wa OK Jazz.Katika anga za utunzi yuko kule kwenye kundi la Franco na Tabu Ley. Lakini pia yeye ana mashairi mazito hadi kupewa jina la Le Poet.

Ame mentor wanamuziki wengi sana pamoja na Sarah Solo wa Werrason na Olivier Tshimanga mkali wa solo asiye na mfano-hawa wamepitia Bana OK. Ndani ya OK Jazz amekuwa mpiga rythm, Chef d'Orchestre, Vice President na mwisho kabisa President wa OK Jazz hadi bendi ilipovunjika. Kijana wa Luambo ameifufua miaka ya karibuni.

Nimtakie maisha mema nnje ya muziki baada ya kuwa kwenye game kwa miaka 60 wiki hadi wiki bila kupunzika labda alipokuwa na udhuru. Nyimbo zake na mashairi yake yataishi milele.

Update
Serikali ya DRC leo 19.03.2018 imemuenzi Simaro Lutumba kwa kubadilisha jina la Avenue Mushi kuwa Simaro Lutumba Avenue.

UPDATE
Papa Simaro Lutumba Ndoamanenu Masiya amefariki mjini Paris siku ya Jumamosi tarehe 30 March 2019 siku kama 11 baada ya kutimiza miaka 81. Mola aiweke pema Roho yake (RIP). Pole kwa familia yake, familia yake kubwa ya muziki na wapenzi wake.
 
nakumbuka kibao chake cha Elia, daah aisee ala za mziki zimepangwa na zikapangika kile kibao aisee
 
nakumbuka kibao chake cha Elia, daah aisee ala za mziki zimepangwa na zikapangika kile kibao aisee
Kibao hicho ni moto wa Bana OK. Jerry Dialungana ndo aliongoza kikosi cha magitaa-wakimwita "maboko ya bana OK"-hatari tupu.
 
Shukrani kaka ila huyu jamaa simfahamu
Na kweli sio wengi wanaomfahamu hata wakati TP OK Jazz inatusua watu walimjua Franco na waimbaji wake. Simaro ni mtu mtulivu hajawahi kuwa na mikiki-lakini huyu ni mwanamuziki wa wanamuziki. Wanamuziki wengi DRC wanamfahamu kwa umahiri wake na wanasema muimbaji mahiri lazima aweze kuimba wimbo wa Simaro bila wasi wasi. Yuko kiwango cha juu sana-walioimba nyimbo zake wanaweza wakajulikana kuliko mtunzi mwenyewe. Kama una muda ingia youtube au google-"Maya Simaro Lutumba youtube" halafu sikiliza hiyo kitu itakayo shuka.
 
makedonia-mkuu nikushukuru kwa kupandisha hiyo picha ya Le Poet Simaro Masiya kwenye huu uzi na kuufanya ueleweka zaidi. Great & thanks.
 
Na kweli sio wengi wanaomfahamu hata wakati TP OK Jazz inatusua watu walimjua Franco na waimbaji wake. Simaro ni mtu mtulivu hajawahi kuwa na mikiki-lakini huyu ni mwanamuziki wa wanamuziki. Wanamuziki wengi DRC wanamfahamu kwa umahiri wake na wanasema muimbaji mahiri lazima aweze kuimba wimbo wa Simaro bila wasi wasi. Yuko kiwango cha juu sana-walioimba nyimbo zake wanaweza wakajulikana kuliko mtunzi mwenyewe. Kama una muda ingia youtube au google-"Maya Simaro Lutumba youtube" halafu sikiliza hiyo kitu itakayo shuka.
Shukrani mkuu ngoja nifanye hvyo
 
Mashairi adhimu na jadidi kwenye wimbo wake "Ebale ya Zaire" ukiimbwa na Sam Mangwana ulidhihirisha kuwa hana mfanowe
 
Masiya,

- Saafi sana anaitwa Le Commandant Lutumba Simaroo, ndiye aliyekua the right hand man wa Franco Lwambo Makiadi na katika nyimbo zake zote alizotunga ni wimbo wa "Eau Benitte" ambao ni maarufu sana na Wanawake wengi sana wa KiZaire na France, ingawa "Maya" ndio unajulikana zaidi kuliko nyimbo zote alizowahi kutunga.

- Ni mmoja kati ya Wacongo ninayemuheshimu sana kwani hana tamaa na mambo ya kijinga kama Wacongo wengine hata Madilu alifanya makosa sana kuachana naye kimuziki kwa sababu nguvu yake akiwa na Simaroo haikuwahi kuwa sawa na akiwa peke yake.

- Lutumba Simaroo anaendelea kua mmoja wa my Icons wa music Duniani hasa Wanamuziki ninaowaheshimu from Congo, nimemuona sana New York alipokua anakuja na Lwambo kwani siku zote walikua wanapiga kwenye Club Kilimanjaro nilipokua DJ wa Club hiyo. Na nimekutana nao sana nikiwa ninaishi Belgium kule Matonge ambako huwa wanakuwa watu wa kawaida sana.

- Wafuatao ni WaCongo ninaowaheshimu sana kimuziki all the times nao ni:- (TP. Ok Jazz) ni Lwambo Makiadi, Maestro Diluangana, Lutumba Simaroo, Djo Mpoyi, Pepe Ndombe, na Josky Kiambukuta. (Orch. Sosoliso) ni Mario Matadidi Mabele MWana Kitoko, Loko Masengo. (Orch. Veve) ni Verkys Kiamuangana Mateta, Mujos, Matalanza. (Orch. Lipua Lipua) ni Mbumbi Malanda, Vata Mombassa, Mongo Ley, Nzaya Nzayadjo, Nsayi Nono Nkuka, Kilola Kitoko Kiyangani. (Orch. Kiam) ni Muzola Ngunga, na Memi. (Orch. Kamale) ni Kzunga Ricos, Mulemba na Tshimanga Asossa. (Orch. Banangenge) ni Nsilu wa Bansilu Manitcho, Fataki Los Los MAsumbuko ya Dunia. (Orch. Grand Pizza) ni Djodjo Ikomo. (Mangelepa) ni Kai Kai, Kabila Kabanze, Bwami Walumona, (Orch. Langa Langa) ni Nyoka Longo. (Emperial Bakuba) ni Pepe Kalle. (Wenge Musica BCBG) ni Jean Bendel Mpiana, Werason, Alain Makaba, Alain Mpela "Afande", Robero Atalaku, Dominquez.

le Mutuz
 
Saafi sana anaitwa Le Commandant Lutumba Simaroo, ndiye aliyekua the right hand man wa Franco Lwambo Makiadi na katika nyimbo zake zote alizotunga ni wimbo wa "Eau Benitte" ambao ni maarufu sana na Wanawake wengi sana wa KiZaire na France, ingawa "Maya" ndio unajulikana zaidi kuliko nyimbo zote alizowahi kutunga.
Imekaa vizuri lakini huyu ni Le Poet Simaro Lutumba, Le Commandant de Bord ni Josky Kiambukuta (Jo Sex) aliye letwa OK Jazz na Simaro Lutumba. Kwa ujumla katika waimbaji wa OK jazz (ambao karibu wote wana majina makubwa kwa umahiri wao) wa miaka ya 1975 na kuendelea Josky alikubalika kama kiongozi wao na kuwa Vice wa Simaro baada ya Franco kufariki.
 
Kwa vijana wa enzi hizo itapendeza pia kujua ya kuwa Vicky Longomba (Baba yake Awilo) alipoanzisha bendi ya Negro Success (1961) akitokea Round Table na African Jazz, alimchukua BHOLEN kutoka OK Jazz. Bholen alikuwa akipiga rythm guitar na solo guitar OK Jazz hivyo kukawa na pengo la mpiga rythm gitaa na Franco ndio katika kutafuta mrithi wa Bholen akamsajili Lutumba Simaro. Hapa Franco "alilamba" dume'.
 
Imekaa vizuri lakini huyu ni Le Poet Simaro Lutumba, Le Commandant de Bord ni Josky Kiambukuta (Jo Sex) aliye letwa OK Jazz na Simaro Lutumba. Kwa ujumla katika waimbaji wa OK jazz (ambao karibu wote wana majina makubwa kwa umahiri wao) wa miaka ya 1975 na kuendelea Josky alikubalika kama kiongozi wao na kuwa Vice wa Simaro baada ya Franco kufariki.

- Sure my bad, ni Le Poet Lutumba Simaroo Masiya, good stuff!

le Mutuz
 
Back
Top Bottom