Pre GE2025 Lema: Rushwa imekithiri kwenye uchaguzi wetu

Pre GE2025 Lema: Rushwa imekithiri kwenye uchaguzi wetu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Makada na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wameendelea kutoa maoni juu ya hali ya sasa ndani ya chama hicho kuelekea uchaguzi wa uongozi hasa ule wa nafasi ya uenyekiti taifa.
IMG_2593.jpeg

Godbless Lema, mwanachama wa muda mrefu na kada wa CHADEMA, ameandika ujumbe wa kina kupitia ukurasa wake wa X, akitoa wito kwa wanachama kutafakari kwa makini mwenendo wa maadili ndani ya chama.

Pia, Soma: Godbless Lema: Mbowe ameniambia zaidi ya mara 5 amechoka anataka kuachia Chama hiki

Katika ujumbe wake, Lema amehoji tabia za uongozi na ushindani ndani ya chama hicho, akisisitiza kuwa chama kikuu cha upinzani kinapaswa kujitofautisha na tabia za kimaadili zinazokinzana na malengo ya mabadiliko.

"Tafakarini kwa makini tabia za chama chetu kwa sasa... Ushindani ndani ya chama unatukuza maadili na malengo yetu kama chama cha siasa kinachotaka mabadiliko? Je, sisi na CCM tofauti yetu ni nini?" ameandika Lema.

Ameeleza kuwa uimara wa chama unatokana na maadili na usafi wa viongozi na wanachama wake, huku akionya dhidi ya matumizi ya rushwa katika mchakato wa kuchagua viongozi.

"Uimara na ukubwa wa chama unajengwa na maadili na usafi wa viongozi na wanachama wake na wala sio mtandao wa matawi. Uongozi wa chama cha siasa unaopatikana kwa rushwa hauwezi kukemea rushwa wala matendo mabaya katika jamii", ameandika Lema.

Lema ametoa wito kwa wajumbe wa CHADEMA kuhakikisha kuwa uchaguzi wa uongozi unazingatia maadili na matendo mema. Amesisitiza kuwa, "Tukiuua maadili ya wanachama wetu, hatuwezi kuwa na ujasiri wa kudai haki."

Ameshauri wajumbe kumchagua Tundu Lissu kwa nafasi ya uenyekiti, akisisitiza kuwa ni muhimu kuchagua viongozi kwa misingi ya uadilifu badala ya kufuata rushwa au maslahi binafsi.
 
Angesema haya wakati Lowasa alipoamia CHADEMA 2015, Kwa Sasa yameshazoeleka Imeshakuwa DOA tayari .. wajumbe mmesipofanya cha maana katika Uchaguzi huu mnamiaka 5 ya kuishi kama Manyani Pesa ni tamu Sana ila ni mbaya sana
 
Lema mpanga matokeo huyu ansongea nini? Ni mchafu sana akiwa kiongoz wa kanda alinyima haki za wa2 walioshinda uchaguzi na kuwaweka watu wake hata hivyo hao wa2 wake walitimkia CCM. Lema hana moral authority ya kusema hayo kwakua yy ni mhuni kma walivyo wahuni wengne
 
Mihela ya Mama Abdul, Mbowe kaitapakaza Chadema
 
Jumanne ifike tu tujadili mustakabali wa hiki chama!
 
Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Bawacha ulikuwa na wagombea watatu ambao walikuwa Sharifa, Simba na Suzan. Simba alitangaza kuwa yeye anamuunga mkono Lissu. Na Lissu bila hiyaana akataka wajumbe wampigie kura Simba. Wagombea waliobaki hawakusema wameegemea wapi. Baada ya awamu ya kwanza kukosa mshindi aliyepata zaidi ya asilimia 50, Suzan akaondolewa wakabaki Sharifa na Simba. Kabla ya awamu ya pili ya uchaguzi kuanza wajumbe walipokea ujumbe kutoka kwa "Suzan" ukiwataka waliompigia kura wampigie Simba. Suzan akasimama jukwaani kaukana kabisa huo ujumbe na kuwa hajautuma. Kwa sababu ujumbe huo ulitarajiwa kumfaidisha Simba, bila shaka aliyetuma alikuwa ni mfuasi wa Lissu. Mpaka sasa hivi huu ni uthibitisho pekee wa mchezo mchafu kufanyika na wahusika ni wafuasi wa Lema na Lissu. Lema hana moral authority kuzungumzia rushwa katika uchaguzi. Anachofanya ni kutayarisha sababu za watu wao kufanya fujo endapo Lissu atashindwa. Ovyo kabisa.

Amandla...
 
  • Nzuri
Reactions: Tui
Back
Top Bottom