Lengo la muungano wetu ni nini hasa?

Lengo la muungano wetu ni nini hasa?

mwananthropolojia

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2012
Posts
956
Reaction score
657
Bunge saizi linaboa,ni la upande mmoja baada ya wenzao wa serikali 3 kutoka,ila naona wale wa serikali 2 wameachiwa nafasi na bado wanashindwa kujenga hoja ya namna kuitoa Tanzania kwenye umasikini wa miaka 50,wamebaki kung'ang'ania kero zinarekebishika ndani ya2.

Ajabu kwa miaka50 ndani ya serikali2 wamejaribu kutatua bila mafanikio. Serikali3 ilikua imejaa maono/vision kuliko muundo wa serikali2.

Huu muundo wa serikali2 hauna mvuto wa kuvutia hata nchi nyingine kujiunga.Mimi nilidhani muungano wetu na Zanzibar lengo lilikua wenzetu wa mataifa mengine ya kiafrika wavutiwe na muungano wetu ili nao wajiunge kidogodogo, mwisho afrika nzima iwe moja.

Hilo ndilo lilikuwa lengo la waasisi wetu kuungana,na ndio ubishani mkubwa uliokuepo kati ya Nyerere na Nkrumah.

Nyerere alitaka tuungane kidogodogo wakati Nkrumah alitaka umoja wa haraka wa Afrika.Huu muundo wa serikali 3 unaruhusu na unavutia nchi zingine zijiunge,kwa maana nyingine ni muundo endelevu,umekaa kiexpansionist.

Wengi tumesahau lengo la kuungana hasa ilikua nini . Mwanzo mipango ilikuwa kuiunga East africa ndio iwe mfano kwa Afrika nzima kujiunga kua pamoja,wakenya na waganda wakalikataa kwa kipindi kile.

Nyerere alipoona imeshindikana akawageukia wazanzibar ili uwe muungano wa mfano.Sasa ni miaka50 imepita ndio tumeungana,je tumefanikiwa kuwashawishi wenzetu wajiunge nasi kwenye huu muungano?jibu ni hapana,kwa miaka50 tumeshindwa kuwashawishi.

Tujiangalie sasa tunaungana kwajili gani?.Kama ni kwajili ya ulinzi na undugu tujue, maana kama ni suala la kiuchumi basi hamna faida, muungano umekua ukiongeza gharama tu kwani ni sisi wananchi wa Tanganyika ndio tunaingia gharama na sio wenzetu wazanzibar.

Mapato tunayopata kutokana na muungano ni madogo kuliko matumizi. Tukiangalia hii miundo, Serikali3 imekaa kiuwazi na kiuwajibikaji wa matumizi ya rasilimali na uongozi,kwa maana nyingine una faida kiuchumi,kwani uchumi ni matumizi mazuri ya rasilimali ulizonazo kwa mpangilio mzuri.

Wakati serikali2 imekaa kisiasa zaidi na hautaki mabadiliko kwa mana nyingine aliye masikin ataendelea kua masikin na aliye juu atazidi kua juu.

Serikali1 imekaa kiulinzi na kindugu zaidi,ila tatizo wazenj washasema sisi ni watu tofauti,kwaio serikali moja itazid kuleta mgogoro.

Turudi kwenye lengo halisi.
 
Hata mimi nilitegemea wanaojiita WAUMINI WA DINI MPYA YA 2, fursa ya wao kuwa peke yao kuanzia leo, wangetumia muda huu vizuri kuweka bayana hizo Kero sugu za Muungano. Kisha waanze kuonyesha mipango na mikakati inayotekelezeka ili kumaliza kama sio kuziondoa kabisa.

Lakini cha ajabu hakuna HATA MMOJA mwenye maono ya kutafuta utatuzi wa Kero sugu za Muungano bali wachangiaji wote wamejificha kwenye ahadi kana kwamba, mara baada ya Katiba ya Serikali mbili kupita tutakuwa na ndege yenye Auto Pilot ambae kazi zake ni kuondoa hizo Kero..

Seriously guys, tuweke mambo hadharani tuache kuishi kwa nadharia kwamba Kero za Muungano zinaweza kumalizika ndani ya Serikali mbili bila kuwa wakweli wa nafsi zetu kwa kuonyesha jinsi zinavyo weza kushughulikiwa. NIMECHOKA NA AHADI HEWA kwamba Kero hizi za Muungano zitaisha. Hili ndilo jambo waumini wa Serikali mbili wanatakiwa kujibu. The question is HOW not WHO?

Kama hatutegemei miujiza kwanini hatusemi bayana jinsi mbinu/mkakati mbadala unavyoweza kushughulikia hizo Kero?
"....You cant fool all the people all the Time..." by Bob Marley
 
Hili ni swali la msingi sana. Kwa bahati mbaya wabunge wote wamejikita kwenye "uumini" wa Muungano bila hata kwanza kujadili muungano wenyewe ni nini hasa na upo kwa sababu zipi? Wananchi wengi wa kawaida kwa upande wa Tanganyika hawaoni wala "kuu-feel" huu muungano na vivo hivyo kwa wazanzibari.

Muungano umekuwa upo kwa viongozi wa juu tu na vyama vyao. Viongozi wa juu wa nchi (kisiasa) ndio kwa kiwango kikubwa wanaguswa na muungano huu. Kwa miaka 50 viongozi wa kisiasa wameshindwa kuwaunganisha na kuwaelemisha wananchi juu ya manufaa ya muungano (kama yapo).

Leo hii tunashuhudia vurugu, matusi na kejeli za kila namna katika bunge la katiba kwa sababu kuna siri kubwa juu ya muungano wa nchi hizi mbili. Wajumbe wengi wamekuwa wakieleza faida mojawapo kubwa ya kuwa na muungano ni kuendeleza udugu wa kihistoria uliopo kati ya watu wa Tanganyika na zanzibar. Lakini binafsi naona sababu hii haina mashiko, kama ingekuwa na mashiko tungungana na Kenya, Msumbiji au Zambia au hata Malawi ambapo nchi hizo kijiographia ndio zina ukanda mkubwa uliopakana na Tanganyika. Zanzibar imepakana na mikoa ya Dar es salaam na Tanga, tena kwa eneo dogo tu la kijiographia pamoja na idadi ya watu. Kama hii ndo sababu kuu, watu wa Kigoma, Songea, Mwanza, Shinyanga, Mbeya, Dodoma etc wanahusiana vipi na wazanzibar?

Binafsi muungano ungekuwa na faida kubwa kwa wananchi kama ungejikita kiuchumi zaidi. Leo hii kusingekuwa na mabishano pale bungeni kwa sababu kila mjumbe angekuwa hana shaka juu ya faida za muungano. Hoja ingekuwa ni namna gani nchi hizi mbili zinaweza zikanufaika zaidi na muungano, mfumo upi utazaa manufaa zaidi na sio mabishano ya kivyama kulaumiana kuwa wanataka kuvunja muungano.


Iwe serikali 2 au 3, kama wananchi hawaoni umuhimu wa muungano, basi muungano huu utavunjika tu. Na ndio maana kero za muungano kwa miaka 50 hazijatatuliwa mpaka leo.


Nawasihi wajumbe wa bunge la katiba kuwa isiwe dhambi kuhoji umuhimu wa muungano kabisa. Hata ikibidi turudi kwa wananchi ili tupige kura (referendum) je muungano uendelee kuwepo ama la. Na kama uendelee kuwepo, kwa mfumo upi? Mambo gani yawe ya muungano na yapi yawe ya serikali washiriki?


Tusitumie nguvu nyingi na kupitisha mifumo isiyokuwa na manufaa kwa wananchi. Tusidumishe muungano kwa sababu ya kutom dissappoint Mwalimu Nyerere. Tujifunze kuwa na fikra huru, tusikariri. Mazingira yanabadilika, kitu kizuri leo sio lazima kikawa kizuri kesho.

TUULIZE MASWALI, TUSIKILIZE HOJA NA KISHA TUAMUE.
 
bila ya kuandika story ndefu mwanzo kabisa lengo la Muungano ni kudhibiti Ukomunisti upande za zanzibar.
mabeberu walimtumia nyerere kuimeza znz ili kuondoa au kuupunguza kasi ukomunisti.
wakati huo mwalimu bado hajawa mjamaa.
baadae lengo kuu likawa ni kuudhibiti uislam basi hakuna jengine.
Tanganyika kama nchi haifaidiki chochote na muungano huu...hakuna faida yoyote.zaidi nyimbo za kisiasa.
na znz nao hawafaidiki chochote na muungano huu zaidi ya kulima vitunguu kama alivosema kikwete.
watu wa kawaida waishio Tannganyika kule mtwara,mbeya , ukerewe hawana faida yoyote na muungano..vivyo hivyo wananchi wa makunduchi micheweni urowa hawana walipalo kwenye muungano huu
muungano huu hauna hata shule moja pale znz au hospitali au kitu cha maana ukasema hichi ni faida ya muungano.

raia wa nchi hizi mbili wao ndio kuhangaika na maisha wapo wamepata na kuchuma kwa maslahi ya familia zao na sio kwa maslahi ya nchi walizo toka
hiyo ukweli utabaki tanganyika anataumikia mradi wa nje wa kuidhibiti znz ili kuzuia nuru ya uislamu na lukuvi ametuthibitishia hili
 
Hili ni swali la msingi sana. Kwa bahati mbaya wabunge wote wamejikita kwenye "uumini" wa Muungano bila hata kwanza kujadili muungano wenyewe ni nini hasa na upo kwa sababu zipi? Wananchi wengi wa kawaida kwa upande wa Tanganyika hawaoni wala "kuu-feel" huu muungano na vivo hivyo kwa wazanzibari.

Muungano umekuwa upo kwa viongozi wa juu tu na vyama vyao. Viongozi wa juu wa nchi (kisiasa) ndio kwa kiwango kikubwa wanaguswa na muungano huu. Kwa miaka 50 viongozi wa kisiasa wameshindwa kuwaunganisha na kuwaelemisha wananchi juu ya manufaa ya muungano (kama yapo).

Leo hii tunashuhudia vurugu, matusi na kejeli za kila namna katika bunge la katiba kwa sababu kuna siri kubwa juu ya muungano wa nchi hizi mbili. Wajumbe wengi wamekuwa wakieleza faida mojawapo kubwa ya kuwa na muungano ni kuendeleza udugu wa kihistoria uliopo kati ya watu wa Tanganyika na zanzibar. Lakini binafsi naona sababu hii haina mashiko, kama ingekuwa na mashiko tungungana na Kenya, Msumbiji au Zambia au hata Malawi ambapo nchi hizo kijiographia ndio zina ukanda mkubwa uliopakana na Tanganyika. Zanzibar imepakana na mikoa ya Dar es salaam na Tanga, tena kwa eneo dogo tu la kijiographia pamoja na idadi ya watu. Kama hii ndo sababu kuu, watu wa Kigoma, Songea, Mwanza, Shinyanga, Mbeya, Dodoma etc wanahusiana vipi na wazanzibar?

Binafsi muungano ungekuwa na faida kubwa kwa wananchi kama ungejikita kiuchumi zaidi. Leo hii kusingekuwa na mabishano pale bungeni kwa sababu kila mjumbe angekuwa hana shaka juu ya faida za muungano. Hoja ingekuwa ni namna gani nchi hizi mbili zinaweza zikanufaika zaidi na muungano, mfumo upi utazaa manufaa zaidi na sio mabishano ya kivyama kulaumiana kuwa wanataka kuvunja muungano.


Iwe serikali 2 au 3, kama wananchi hawaoni umuhimu wa muungano, basi muungano huu utavunjika tu. Na ndio maana kero za muungano kwa miaka 50 hazijatatuliwa mpaka leo.


Nawasihi wajumbe wa bunge la katiba kuwa isiwe dhambi kuhoji umuhimu wa muungano kabisa. Hata ikibidi turudi kwa wananchi ili tupige kura (referendum) je muungano uendelee kuwepo ama la. Na kama uendelee kuwepo, kwa mfumo upi? Mambo gani yawe ya muungano na yapi yawe ya serikali washiriki?


Tusitumie nguvu nyingi na kupitisha mifumo isiyokuwa na manufaa kwa wananchi. Tusidumishe muungano kwa sababu ya kutom dissappoint Mwalimu Nyerere. Tujifunze kuwa na fikra huru, tusikariri. Mazingira yanabadilika, kitu kizuri leo sio lazima kikawa kizuri kesho.

TUULIZE MASWALI, TUSIKILIZE HOJA NA KISHA TUAMUE.

Mkuu! ndio maana nimeshangaa sana,watu wamekaa na kuwaza jambo moja tu,usalama/ulinzi.Hiki ndio kitu kikubwa kinachowatisha watu wengi kwamba serikali3 zitaleta vita.toka siku ya kwanza nilipoisikia hii hoja nikajua propaganda za vitisho zimeanza,kama yaleyale ya 95! ooh wapinzan wataleta vita kisa wanatumiwa na mataifa ya nje!sasaivi ni ooh wapinzani wataleta vita kisa wanataka serikali3! kwahiyo tusiwachague mwaka 2015.
Hii propaganda ishaanza na watanzania kwajili ya hofu zisizokuwepo watawapigia magamba kura za kishindo hata wakiweka jiwe. Kwenye suala la gharama nawashangaa sana watu, kwani leo hii tunasita kujiunga na east africa maana tunaona hatuna maslahi makubwa ya kiuchumi na wakenya na waganda watatunyonya tu,ila kwenye suala la muungano huu kuwa mzigo hatuoni gharama zake kubwa tunazoingia, hatuzioni kweli? hatujui kama tunanyonywa?je ni sahihi kufumbia macho mfumo unaojua unakupotezea mapato?unaokupunguza ufanisi kutokana na urasimu?unaokutia hofu kila siku maana upande wa pili wa muungano hawaishi kulalamika na kukutishia wanataka nchi yao iliyotekwa kila siku ? Ni heri tuingie gharama za kuendesha serikali3 tukijua ufanisi utaongezeka kwani urasimu utapungua na mzunguko wa pesa utaongezeka ,kwani pesa zitatembea haraka hivyo kuongeza mapato,mgawanyo wa pesa utakua wazi, kwa maana nyingine pesa zisizo na maelezo hazitakuepo tena zitpelekwa moja kwa moja zikahudumie wananchi.mapato yataongezeka maana wazenj watatafuta na sisi tutatafuta katika mambo yasiyo ya muungano,kwa wale wenye wake zao wanaofanya kazi au biashara wanajua hili suala la baba na mama kufanya kazi. na mwisho kila mtu atawajibika kuulinda muungano kwa pande zote ,kwani utakua na faida zinazoonekana na zinajulikana kwa pande zote2. kama ni mambo7 basi yawe 7 na sio utitiri wa mambo ya muungano ambayo kusema ukweli hawana sababu za kushirikiana zaidi ya kuleta uhasama. Na sasahivi kama umegundua wazanzibar watawala wamegundua wanatunyonya kwahiyo wanakazana kuutetea muungano na sisi lazima maslahi yetu kwenye huu muungano usimamiwe kikamilifu kwa kumrudisha Tanganyika kwenye meza.tutafute faida za ukweli za kuungana na sio faida za kutafuta kwa tochi eti undugu,waafrika wote mbona ndugu lakini hatujaungana nao?muungano ni utashi na maridhiano na sio vingine,upande mmoja unapolalamika ujue kuna tatizo na ni lazima tatizo lisahihishwe ili muende sawa. huwezi kuacha kichwa kiendelee kuuma wakati panadol zipo za kutuliza.tunatakiwa tuangalie mfumo utakaotufaidisha kiuchumi,kwani ndio dunia ya sasa nchi za wenzetu wanavyoungana, mfano china na hong kong na tuachane na hizi propaganda za kisiasa,tuendeshe nchi kisayansi na sio kwa mazoea.tufuate ushauri wa wataalamu
 
bila ya kuandika story ndefu mwanzo kabisa lengo la Muungano ni kudhibiti Ukomunisti upande za zanzibar.
mabeberu walimtumia nyerere kuimeza znz ili kuondoa au kuupunguza kasi ukomunisti.
wakati huo mwalimu bado hajawa mjamaa.
baadae lengo kuu likawa ni kuudhibiti uislam basi hakuna jengine.
Tanganyika kama nchi haifaidiki chochote na muungano huu...hakuna faida yoyote.zaidi nyimbo za kisiasa.
na znz nao hawafaidiki chochote na muungano huu zaidi ya kulima vitunguu kama alivosema kikwete.
watu wa kawaida waishio Tannganyika kule mtwara,mbeya , ukerewe hawana faida yoyote na muungano..vivyo hivyo wananchi wa makunduchi micheweni urowa hawana walipalo kwenye muungano huu
muungano huu hauna hata shule moja pale znz au hospitali au kitu cha maana ukasema hichi ni faida ya muungano.

raia wa nchi hizi mbili wao ndio kuhangaika na maisha wapo wamepata na kuchuma kwa maslahi ya familia zao na sio kwa maslahi ya nchi walizo toka
hiyo ukweli utabaki tanganyika anataumikia mradi wa nje wa kuidhibiti znz ili kuzuia nuru ya uislamu na lukuvi ametuthibitishia hili

Kama lengo la muungano wetu ni kujilinda na maadui wa nje kwa nini tusiweke wazi tu? kuliko kuingia gharama za kila mwaka kuihudumia zenj kama vile ni watoto wasioweza kujiamulia mambo yao?wahafidhina wanaamini bila total control kwa wazenj nchi itaingia vitani,hili sio kweli!na hili linathibitishwa na mabadiliko katika ukoloni, wakati tunapata uhuru tulijua tupo huru ila kuja kujichunguza tukagundua wanatumia ukoloni mamboleo kututawala.je na sisi hatuwezi kutumia mbinu nyingine ili tuishi na wazenj vema?kwani mabadiliko hayaepukiki, hata mkoloni alijua wakati wa kuachia nchi umefika akaondoka kabla hatujaongeza nguvu,sehemu ambazo alijiamini kama msumbiji na kwingineko aliendelea kukaa na pamoja na silaha zake na ukuu wa nchi, waafrika walifaniikiwa kujikomboa.je tunataka historia ya aina hiyo hapa nchini?makubaliano ni muhimu kwenye hili suala tena kwa uwazi,watu sio wajinga tena.
 
Serikali1 imekaa kiulinzi na kindugu zaidi,ila tatizo wazenj washasema sisi ni watu tofauti,kwaio serikali moja itazid kuleta mgogoro.

Acha maneno ya kiuchochezi, mbona hata watanzania bara nao wanajokataa kwamba na hawautaki kabisa muungano kama wazanzibar tu.

Lakini pili, wewe bdo hujaelewa lengo kwanini Nyerere aliunganisha zanzibar na Tanganyika, na kwanini Karume aliuwawa. Endelea kutafuta.
 
Serikali1 imekaa kiulinzi na kindugu zaidi,ila tatizo wazenj washasema sisi ni watu tofauti,kwaio serikali moja itazid kuleta mgogoro.

Acha maneno ya kiuchochezi, mbona hata watanzania bara nao wanajokataa kwamba na hawautaki kabisa muungano kama wazanzibar tu.

Lakini pili, wewe bdo hujaelewa lengo kwanini Nyerere aliunganisha zanzibar na Tanganyika, na kwanini Karume aliuwawa. Endelea kutafuta.

Imekaa Kiulinzi kwani tuna ugomvi na nani ?? Nyerere nchi ilimshinda na hana uwezo wa kuongoza akaona atafute watu kutoka Zanzibar wamsaidie , watu wenyewe ndio wale akina Abdulrahmani Babu waliomshawishi kuleta sera za ujamaa matokeo yake nchi yote imeoza si bara si visiwani.
 
Back
Top Bottom