Leo nazungumzia kifaa cha umeme kinaitwa motion detector sensor

Leo nazungumzia kifaa cha umeme kinaitwa motion detector sensor

jose lupembe

Member
Joined
Aug 24, 2016
Posts
38
Reaction score
58
Ni kifaa cha elektroniki cha usalama ambacho kinafungwa kwenye majengo mbalimbali ili kugundua harakati zisizoruhusiwa katika Maeneo haswa baada ya muda wa kazi. Kifaa hiki kinatumika katika maeneo ya biashara na makazi
Kama vile kwenye majengo ya viwanda na jeshi

Leo tunazungumzia jinsi gani MOTION SENSOR inaweza ikatuma nyumbani

Pamoja na aina mbalimbali za MOTION SENSOR zinazopatikana kwenye soko leo
Faida za MOTION SENSOR ni nyingi katika matumizi mbalimbali

Wamiliki wa nyumba hutumia MOTION SENSOR kwa matumizi ya vitu vingi kwa usalama dhidi ya wizi, hadi ufuatiliaji wa watoto na wanyama.

JINSI MOTION SENSOR ZINAVYOTUMIKA MAJUMBANI
Husaidia kufuatilia watoto wako au wanyama Ikiwa kuna maeneo kwenye nyumba yako ambayo hayafai kwa watoto MOTION SENSOR inaweza kukusaidia.

Karibu na mlango wa maeneo ambayo hutaki watoto wacheze au waende mfano karakana utafunga MOTION SENSOR ikiwa mtoto atakaribia maeneo hayo basi itakuarifu kwa alarm

MOTION SENSOR HUSAIDIA KUWASHA TAA NA KUZIMA

Hii motion sensor itakusaidia kuwasha taa pale tu unapo karibia mlangoni na itazima baada ya kuondoka
Ni nzuri kufunga chooni, kwenye kolido, veranda na parking za magari
Hata taa za kwenye senyenyenge unaweza kufunga itasaidia pia kupunguza matumizi ya umeme kwasababu zitafanya kazi pale tu itakapo detect motion.
Zipo za dizaini tofauti na zimetofautiana umbali wa kudetect.

Imeandaliwa na electrician lupembeTz

Kwa maelezo zaidi call
0769233063
0652353333


images%20(6).jpg
images%20(4).jpg
images%20(5).jpg
images%20(5).jpg
 
Bei gani hio nataka niweke kwenye taa za getini. Za nje kuzunguka nyumba nimeweka sensor zinawaka zenyewe giza likiingia na kujizima asubuhi mwanga ukitoka.
 
nataka taa za chooni na kwenye corridor nifunge hii kitu. moja inaweza kutosha?
bro zipo ambazo taa pamoja na sensor complete 55000 watt 20 na 30watt 65000.

Na kuna sensor peke yake ambayo gharama yake 60000 lakini unaweza ukatumia kwa taa nyingi.

Sasa hapo kama kolido na chooni vipo karibu unanunua sensor moja
 
Mkuu uweke na gharama za kufunga tunafuatilia huu uzi
 
bro zipo ambazo taa pamoja na sensor complete 55000 watt 20 na 30watt 65000.

Na kuna sensor peke yake ambayo gharama yake 60000 lakini unaweza ukatumia kwa taa nyingi.

Sasa hapo kama kolido na chooni vipo karibu unanunua sensor moja
Ufungaji wake ni rahisi kwa fundi umeme yoyote kufunga? Na vipi kama kila taa ilikuwa na switch yake na mimi nimenunua sensor moja?
 
Ni kifaa cha elektroniki cha usalama ambacho kinafungwa kwenye majengo mbalimbali ili kugundua harakati zisizoruhusiwa katika Maeneo haswa baada ya muda wa kazi. Kifaa hiki kinatumika katika maeneo ya biashara na makazi
Kama vile kwenye majengo ya viwanda na jeshi

Leo tunazungumzia jinsi gani MOTION SENSOR inaweza ikatuma nyumbani

Pamoja na aina mbalimbali za MOTION SENSOR zinazopatikana kwenye soko leo
Faida za MOTION SENSOR ni nyingi katika matumizi mbalimbali

Wamiliki wa nyumba hutumia MOTION SENSOR kwa matumizi ya vitu vingi kwa usalama dhidi ya wizi, hadi ufuatiliaji wa watoto na wanyama.

JINSI MOTION SENSOR ZINAVYOTUMIKA MAJUMBANI
Husaidia kufuatilia watoto wako au wanyama Ikiwa kuna maeneo kwenye nyumba yako ambayo hayafai kwa watoto MOTION SENSOR inaweza kukusaidia.

Karibu na mlango wa maeneo ambayo hutaki watoto wacheze au waende mfano karakana utafunga MOTION SENSOR ikiwa mtoto atakaribia maeneo hayo basi itakuarifu kwa alarm

MOTION SENSOR HUSAIDIA KUWASHA TAA NA KUZIMA
Hii motion sensor itakusaidia kuwasha taa pale tu unapo karibia mlangoni na itazima baada ya kuondoka
Ni nzuri kufunga chooni, kwenye kolido, veranda na parking za magari
Hata taa za kwenye senyenyenge unaweza kufunga itasaidia pia kupunguza matumizi ya umeme kwasababu zitafanya kazi pale tu itakapo detect motion.
Zipo za dizaini tofauti na zimetofautiana umbali wa kudetect.

Imeandaliwa na electrician lupembeTz

Kwa maelezo zaidi call
0769233063
0652353333


View attachment 1720205View attachment 1720206View attachment 1720207View attachment 1720208
Ni nzuri sana kuifunga kwenye ngazi za maghorofa ambazo zinafungwa taa katika kila steps za ngazi.
 
hakuna na kufunga kwenye chupi ili nijue movement yake ikivuliwa na kuvaliwa!??
 
Mkuu uweke na gharama za kufunga tunafuatilia huu uzi
SENSOR 50000

Contactor 45000 Hii itatumika kama current ya taa zako itakuwa kubwa

Waya 20000

Labour charge 40000 kwa dar

Jumla 155000
 
Ufungaji wake ni rahisi kwa fundi umeme yoyote kufunga? Na vipi kama kila taa ilikuwa na switch yake na mimi nimenunua sensor moja?
Fundi yoyote anaweza kufunga lakini kama hana uzoefu na hizo sensor itampa shida

Kujitegemea switch siyo tatizo kwasababu ukifunga hiyo sensor switch muda wote zinatakiwa kuwa ON
 
Back
Top Bottom