Unawaset watu, huna shida wewe umekuja kupiga story tu mwenye shida hanaga konakona nyingi
Muda utaongeaMpenzi ingekuwa hivyo ni siku nyingi ningepotea.. mimi nimejikuza mwenyewe na mtaani kwetu Hakuna binti aliesoma na alietulia na asie na mtoto zaidi yangu… huko nilishapita kinachoniwazisha hapa ni hii hatua nitavukaje
Mbona hujibu umesomea nini usaidike?Rafiki angu amini unachoamini
Bonge la point. Umeongea vema sana.Hakuna uhalali wowote ule wa mwanamke kudanga. Hii kitu itachafua maisha yako na itaharibu kabisa maisha yako kiasi kwamba hata ukiwa ndani ya ndoa bado utatamani kudanga.
Kupewa vitu vya bure ni tabia ambayo itakukaa mpaka unakufa, ukizoea vya bure kupewa na mwanaume utaingiwa na tamaa za maisha zaidi, hapo sasa hata utatamani maisha ya juu zaidi, hautaweza kuridhika, na ukifka hatua hiyo kutulia ndani ya ndoa au kuwa na mwanaume wa kawaida kuanza nae maisha kwako itakuwa ngumu.
Unapokuwa na shida kama hivi, omba msaada usaidiwe ila usije fikiria kufanya umalaya, yaani kudanga sababu ya hali ya maisha. Ninakwambia hivi sababu mimi nmeshahuhudia mabinti wengi wadangaji wanapofika 30s maisha yao yanapoanza kujawa na majuto ambayo hawawezi tena kuyerekebisha.
Duh! Ushauri huu? haujakuwa mzuri aisee.Tafuta sponsor wa usafirishaji, wa nywele, wa kodi na kukutoa out weekend. Unakaaje kizembe town.
Sawa binti,kwa hiyo lengo la kuleta uzi lilikuwa lipiNatamani kufanya hivyo ila kuna watu humu wanaweza kutumia namba yangu kunikejeli
Nauli 3000 x 30 = 90,000
kula 2000 x 30 = 60,000
jumla Tshs 150000/-
baki 100,000/-
pangia huko nyumbn , nenda kapange huko kazn life simple
ingekua shida imembana ni kama choo kikikuchoma lazma utafte choo huna cha kusubiri nawaza ukute anatutaniaSawa binti,kwa hiyo lengo la kuleta uzi lilikuwa lipi
Baraka huwa haziji hivyo mkuu ebu tuachane na ule msemo huu msemoPole dada yangu,ukiona hivyo ujue baraka zimekukaribia.
Hebu PM namba yako tuweke chochote.Hapa nilipo nina majonzi, roho imeniuma sana kwa kuzaliwa kwenye familia maskini
Ipo hivi mimi kwetu ndio wa mwisho msichana peke yangu kati ya watoto 6.. Mzee wangu alitangulia mbele za haki hivyo tumebaki na mama tu.. hao ndugu zangu wote hawana maisha ya kueleweka isipokuwa mmoja tu angalau yeye ameajiliwa serikalini ndio kidogo anaibeba familia, yeye ameshaoa ana familia yake
Mimi nimeshahitimu chuo nina kama Miaka miwili nyumbani.. nimepata sehemu ya kujishikiza wananilipa 250000.. Kwetu ni bunju nafanyia kazi magomeni kila siku natumia 5000 yaani 3000 nauli 2000 nakula mchana hapo Ndio najibana mno..
Sasa kwasasa Hivi nyumbani Hakuna mtu nipo peke yangu mama ameenda kijijini kwao bibi anaumwa, mama yangu hana kazi ile ya kumtegemea anauza chupa za maji hivyo siwezi kumsumbua kwa chochote, amesafiri hajaniachia hata shilingi 100.. Hakuna chakula ndani Hakuna chochote, nachofanya nikitoka kazini nashukia kwa brother nakuta wamepika nakula naondoka
Leo nimeumia sana sijaenda kazini Nina siku 2 sina nauli hela niliokuwa nayo akiba imeisha nimemuomba bro kasema yeye hana hela hawezi kuwa anatoa hela mara mbili mbili kwa familia yake na kwangu, Kama niliweza kutafuta kazi basi nijitegemee nauli nikitaka kula nije nyumbani,, nikamuuliza sasa nitatoa wapi na Ndio naanza kazi akanijibu nitajua mwenyewe
Hiyo kauli imeniuma yaani anamaana gani kusema nipambane nitafute nauli yaani naitafutia wapi ..
Leo nimeacha kuwa judge Watu na maisha wanayoishi Kama ndugu yangu wa damu ananiambia maneno haya hao wa nnje watanijibu vipi
Ni hayo tu wakuu
Huyo anatafuta kivuli kwa long way wewe soma kwa umakini utaelewaDuh! Ushauri huu? haujakuwa mzuri aisee.