Leo ni Hukumu ya kesi ya Yanga Vs Morrison

Leo ni Hukumu ya kesi ya Yanga Vs Morrison

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
4,016
Reaction score
6,759
Kesi inayomuhusisha aliyekuwa mshambuliaji wa klabu ya Yanga ambaye kwa hivi sasa anakipiga Simba Sc, Bernard Morrison itasikilizwa na kutolewa hukumu leo hii.

Morrison anadai kuwa hakusaini mkataba wa kuongeza miaka 2 Yanga huku Yanga na wao wakidai mchezaji huyo ni mali yao.
 
Yanga ile timu kama vile haina uongozi, mambo yao ya kiswahili sana, tena washukuru TFF wakati ule waliwabeba walitakiwa kushushwa daraja kabisa.
 
Aisee, sikujua kama hukumu itatolwa siku hiyo hiyo ya kusikilizwa!
Hata mi sikujua hili

Nilidhan leo inasikilizwa tu halafu itapangwa tarehe nyingine ya hukumu
 
Kinachofanyika leo ni usikilizaji wa kesi ila maamuzi yanafanyika baada ya siku kadhaa
 
Kinachofanyika leo ni usikilizaji wa kesi ila maamuzi yanafanyika baada ya siku kadhaa
Kama sijakosea hii kesi haisikilizwi leo Bali inafanyiwa hukumu mana pande zote mbili zilikubaliana kukusanya ushahidi na kuwasilisha CAS hivyo CAS watahukumu kutokana na hizo evidences. Kwa maana hiyo CAS walishapitia huo ushahidi na Leo ni hukumu
 
Back
Top Bottom