Leo ni kumbukumbu ya Edward Moringe Sokoine

Leo ni kumbukumbu ya Edward Moringe Sokoine

Miss Madeko

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
4,364
Reaction score
5,609
Miaka ya nyuma tuliona maandalizi ya hii siku kuanzia kwenye vyombo vya habari na hata viongozi wetu walikuwa wakilitaja hili jina kuanzia April mosi hadi siku kama ya leo kilele. Lakiini sasa hivi ni kimya kabisa hii ina maana anaanza kusahaulika au?
 
Hivii hii sio public day ????


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Miaka ya nyuma tuliona maandalizi ya hii siku kuanzia kwenye vyombo vya habari na hata viongozi wetu walikuwa wakilitaja hili jina kuanzia April mosi hadi siku kama ya leo kilele. Lakiini sasa hivi ni kimya kabisa hii ina maana anaanza kusahaulika au?
Kumbukizi yake inafanyikia Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine ( SUA) na leo ndo yanafikia kilele, yalianza jumatatu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi bado natafuta video au hata audio za huyu jamaa!
kwanini hazipatikani?
 
Uzi wa 2019, siyo mbaya.

Marehemu Edward Moringe Sokoine alikuwa mtu maarufu.

Jasiri, aliyethubutu.

Nikikumbuka ni kama aliwahi kuwa waziri kisha akaenda kusoma huko ughaibuni.

Alipoteuliwa kuwa waziri mkuu ni kama mteuzi wake alishtukia uwezo wa utendaji wake

Ikafika siku ya kufunga kikao cha bunge huko dodoma.

Wakati huo tukiona bunge laivu.

Aliaga kuwa tutaonana bunge lijalo. Hakujua masikini nini kitamfuata.

Ile anarudi zake dsm kwa njia ya barabara katikati ya pori ndipo alipokutana na gari landcruiser mkonga nje ikiendeshwa na dogo mkimbizi ikamvaa uso kwa uso.

Masikini Moringe Edward, safari ya maisha yake ikaishia pale.

Alizikwa kwao, japo miaka kadhaa nilisikia wanataka kuhamisha mwili maana boma limehama. Sijui kama zoezi lilifanikiwa.

Tuliomfahamu Edward Moringe Sokoine tunamkumbuka.

Lala salama huko uliko shujaa wetu, je umewahi kukutana na Mwalimu Nyerere huko, msalimie.
 
Back
Top Bottom