Leo nimekumbuka namna mpenzi/ mama wa watoto wangu alipoanza kunishinda kipato baada ya kupata kazi kila kitu kikaparaganyika

Dah!... hatari hii....
 
tahadhari kwa kenge wanaooa eti wasaidiane majukumu
 
Pole sana Mkuu, kuna kisa kilimkuta jamaa fulani mwaka 2006 alimchukua Mwanamke tena alikuwa Barmaid akawa anaishi naye jamaa alikuwa analipwa 150,000 tu, sasa akamtafutia kazi za Kuuza duka mjini yule Mwanamke akawa anapata hela maana na dili zilikuwa zinatokea kwenye ishu za kuuza duka. Yule demu alijichanga akanunua mabati na akayasafirisha kwao Singida. Taarifa zilisema kwao kajenga nyumba ya bati, lakini kwa jamaa alikuwa analeta mapicha picha sana mpaka alikuwa anampeleka jamaa yake Polisi na kule Polisi alikuwa anahonga hela yaani jamaa alikuwa ananyanyasika sana na Kipesa alikuwa kazidiwa na yule Mwanamke. Watu wenye roho mbaya wakamtia gundu yule Mwanamke maana alikuwa na dharau sana. Akafukuzwa kazi na Jamaa waliachana. Mara ya mwisho mwaka 2010 yule demu nilimuona Tandale kwa Mtogole anachoma Mahindi.
 
Ndio maana kaka yangu mdogo na 40+ yake hataki kuoa,mwanamke aliyetaka amuoe kamgharamia nusu ya gharama za chuo lakini alipopata kazi kamkimbia. Sasa ana mtoto kazaa na mwanamke mwingine anamlea yeye mwenyewe,alipitia katika hali ngumu sana ila kwa sasa ana ajira yake kwenye shirika moja la umma,amejenga nyumba ila suala la ndoa hataki kusikia kabisa.
Na nina kaka mwingine tumezaliwa mama tofauti,yeye kaoa mwanamke akaamua kumsomesha,akaajiriwa serikalini lakini baadae mwanamke akaamua kumkimbia akakimbilia Dar alipata Injinia wa Ujenzi(wale jamaa wa vimacho vidogo akina Chang Chung),sasa jamaa mkataba ukawa umeisha akarudi kwao,mwanamke akaona hapa sirudi mkoani,akapata Injina mbongo ambaye yupo nae hadi sasa na amemzalisha mtoto,na kwa kiburi akarudi mkoani kusalimia akaenda kumsalimia Bro na kumuonesha mwanae aliyempata Dar. Kazi kaacha,akiitwa halmashauri aje atoe maelezo kwa nini haonekani kazini anakataa kwenda..Akina Delila hawa sijui wanataka nini?
 
Pole sana mkuu kwa uliyoyapitia.
 
Hawa viumbe hawakuumbiwa ku handle excess, ka pesa kidogo, mabega juu..Umaarufu kidogo, midomo juu. Kiwiliwili hakiwezi kutawala kichwa hata kama ni kichwa maji. But kuna wachache wenye hekima na akili,yeah bado wapo.
 
Pole sana
 
Mali mkuu, nyumba, gari na duka.
Huyu mke wake alipata tamaa mbaya sana
Dah kuna ujinga mwingi kwa hawa wanawake yaani...mimi manzi yangu alipata kazi nzuri baada ya miaka 3 mapicha yakawa mengi dah nikajiondoa taratibu mpaka siku ananitamkia tuachane tayari nilishamuacha miaka 3 nyuma japo bado ilinichoma.

Mwisho tukubali tu lazima uwe na kipato kuliko mkeo vinginevyo utateseka sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…