Leo nimzungumzie kidogo Kijana Wangu Maltinez!!

Song of Solomon

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2021
Posts
2,752
Reaction score
5,609
The butcher

-pale Ajax amsterdam walikuwa wanapenda kumuita hivo ikiwa na maana CHINJA CHINJA

-Inaweza kuwa mapema kusema hivi but .. believe me Lisandro martinez ni aina ya beki tuliyemkosa kwa kipindi kirefu tangu Vidic aondoke kwenye kikosi

[emoji294]️una mashaka na kiwango cha Martinez ?
- Ana uwezo mkubwa wa kupiga pasi ndefu hivyo anasaidia kwenye counter attack , ana uwezo wa kupiga pasi fupi fupi hivyo husaidia kwenye build up na transition ya haraka kwenda mbele

+Kama hujaona alichokiongeza Martinez kwenye kikosi nakupa pole [emoji40]

- Kuna kazi chafu tena za kihuni anapiga bwana mdogo, anafanya sliding tackles inapobidi , anablock mipira..lakini cha ajabu zaidi pamoja na ufupi wake anafanya vyema kwenye Aerial duels battles

+ More importantly ana mapafu ya mbwa, utamuona muda mwingi anakimbia kuziba gepu ,utamuona muda mwingi amekaa kwenye njia zinazoleta hatari kwenye lango la Man United

-Martinez ananusa hatari (threat awarenes ), Martinez anavuruga mipango kwa kufanya tactical fauls na interceptions [emoji16]kuna kipindi hata yeye mwenyewe alishawahi sema

“My function is to destroy, to be heavy, to cut out counter attacks” !!!

Manchester united ya sasa haihitaji wachezaji wenye vipaji tu ,bali inahitaji wachezaji wenye utayari wa kufia uwanjani kwa ajili ya kupambania timu.

GGMU[emoji1666]
 
I second you, jamaa nimemuangalia these two last games, Ni very agrresive sana. Ana traits zote za Nemanja Vidic. Kikubwa atafutiwe beki mtulivu, akishachafua kazi yake ibaki kuondoa uchafu. Hata mimi ni aina ya defenders ninao wakubali sana. Bahati mbaya wanapotea siku hizi. Ni kama zile Namba 6 za kina Gattuso zilivo adimu sasa
 
Uko sahihi kabisa kiongozi Jamaa anajituma sana
 
Miaka yetu United team nzima ilikuwa na spirit kama ya huyu Martinez sio hawa wapaka poda wanaolipwa mamilioni ya pound!
 
Nawaza huyu jamaa awekwe na Bailly sijui itakuwaje pale nyuma? Though Bailly kaondoka, maana wote ni kazi kazi.
 
Tatizo ni team yenyewe. Coz hata Magwaya alivyofika man u alikuwa wa moto kuliko huyu butcher
 
Kwani Magwaya kaputeni anasemaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…