Leo nipo nyumbani baada ya Miaka 4 nikiwa sijui vipi nitaanza upya

Leo nipo nyumbani baada ya Miaka 4 nikiwa sijui vipi nitaanza upya

mudy92

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2014
Posts
671
Reaction score
531
Wasalaam!

Miaka kadhaa nyuma nilijiunga na Jeshi la kujenga Taifa, nilipata mafunzo ya awali kwa muda wa miaka miwili kikosi fulani huko Nyanda za juu kusini.

Mwisho wa mwaka 2019 ulitokea ujenzi wa ukuta wa IKULU huko DODOMA na mimi nikiwa mmoja wa vijana nilioshiriki ujenzi huo pamoja na miradi mingine kama Hospital ya Uhuru, Uwanja wa Gwaride mpaka kupewa sifa ya Ushujaa na Ahadi ya Ajira na hayati Dr. John Pombe Magufuli baada ya kumaliza ujenzi.

Baada ya sekeseke la vijana kugoma na kulazimisha Ajira sikuwepo katika kundi hilo hivyo kubaki mpaka siku tuliyokwenda huko katika Kambi ya JWTZ kwa mafunzo ya Ajira.

Baada ya check up ya afya inayofanywa kabla ya kozi, niliandikwa kama UNFIT kwasababu ya usikivu hafifu wa sikio la kulia ambao sijui ulianzia wapi.

LEO hii nipo nyumbani baada ya Miaka 4 nikiwa sijui vipi nitaanza upya NAHISI KUPOTEA, sina wa kumlilia, Sina wa kumweleza inaniua taratibu na sijui KESHO ITAKUWA VIPI

Kinachouma Zaidi kuona mwenzio mwenye Shida kama yako ambaye hakushiriki ujenzi kwa miaka 2 akiendelea kuwepo katika Ajira wewe unarudi nyumbani, AJIRA zina MENGI wahanga ni WATOTO WA MASKINI.
 
Kwanza pole sana, pili usilaumu sana kukosa nafasi kutokana na tatizo la kiafya kwani walizingatia vigezo.
Ulipaswa kumove on(kusonga mbele) tangu kipindi kile, inapaswa utambue maisha sio jeshini tu hakuna anayezaliwa imeandikwa atakuwa mwanajeshi.

Anyway, naamini bado hujachelewa. Your future is bright, Mungu akuonyeshe kile ambacho amekupangia. Kiukweli dunia ya sasa sio ya kung'ang'ania njia moja, kama uliweza kukaa JKT miaka miwili kwa nidhamu basi unaweza kufanya jambo lolote,jiamini.

MUNGU AKUONGOZE.
Again; jiamini, sahau muda uliopoteza, acha kuishi na jambo moja moyoni, acha kulaumu, TUFUNGE MKANDA TUSONGE MBELE
 
Mfano, sasa hivi kuna makampuni mengi ya ulinzi, kukaa JKT kwa miaka miwili ni asset kubwa na advantage kubwa kwako, tena huna haja ya kuwaambia habari za sikio lako moja.

Kikubwa usifikirie kukata tamaa, wengi wana matatizo makubwa kuliko hilo la ajira, WAKE UP AND LIVE BRO!! NO MATTER WHAT
 
Pole kwa changamoto ulizopitia, ila napenda kukutia moyo kwamba hujapotea na hutapotea na uachane na mawazo ya kujihisi kupotea. Jambo moja kubwa unapaswa kufahamu, maisha sio lazima uajiriwe, wapo wengine wanaacha ajira na wanajiajiri na maisha yanaenda, labda utuambie una elimu/ujuzi gani ambao unajiamini kabisa kwamba kwenye hilo eneo upo fiti?
 
Pole sana SM.

Tafuta skills za muda mfupi kuzimasta mfano udereva au uoperator kisha jichanganye hatakati huwa zifunguka mbeleni tu... Si uliona kama kwenye inshu za uhamiaji?

Sikiliza na hili pini likufute machozi..
Mbele kwa mbele - Dj Yusuph ft Hardmad 🎶

The world is for fighters, fight SM
 
Pole kwa changamoto ulizopitia, ila napenda kukutia moyo kwamba hujapotea na hutapotea na uachane na mawazo ya kujihisi kupotea. Jambo moja kubwa unapaswa kufahamu, maisha sio lazima uajiriwe, wapo wengine wanaacha ajira na wanajiajiri na maisha yanaenda, labda utuambie una elimu/ujuzi gani ambao unajiamini kabisa kwamba kwenye hilo eneo upo fiti?
Ujuzi mbona ametaja??
 
Huko kupotea kwako ndio furaha yao hawa wanasiasa wa Tanzania kama akina mwigulu nchemba na wengineo...ushauri ni piga moyo konde amka hapo ulipo simama na uendelee na safari ya maisha ...HAKIKA SAFARI YA MAISHA IMEJAA MABONDE NA MIRIMA..
 
wasalaam!

Miaka kadhaa nyuma nilijiunga na Jeshi la kujenga Taifa, nilipata mafunzo ya awali kwa muda wa miaka miwili kikosi fulani huko Nyanda za juu kusini.

Mwisho wa mwaka 2019 ulitokea ujenzi wa ukuta wa IKULU huko DODOMA na mimi nikiwa mmoja wa vijana nilioshiriki ujenzi huo pamoja na miradi mingine kama Hospital ya Uhuru, Uwanja wa Gwaride mpaka kupewa sifa ya Ushujaa na Ahadi ya Ajira na hayati Dr. John Pombe Magufuli baada ya kumaliza ujenzi....

Baada ya sekeseke la vijana kugoma na kulazimisha Ajira sikuwako katika kundi hilo hivyo kubaki mpk siku tuliyokwenda huko ktk Kambi ya JWTZ kwa mafunzo ya Ajira.

baada ya check up ya afya inayofanywa kabla ya kozi, niliandikwa kama UNFIT kwasababu ya usikivu hafifu wa sikio la kulia ambao sijui ulianzia wapi...


LEO hii nipo nyumbani baada ya Miaka 4 nikiwa sijui vip nitaanza upya NAHISI KUPOTEA, Sina wa kumlilia, Sina wa kumweleza inaniua taratibu na sijui KESHO ITAKUWA VIPI

Kinachouma Zaidi kuona mwenzio mwenye Shida kama yako ambaye hakushiriki ujenzi kwa miaka 2 akiendelea kuwepo katika Ajira wewe unarudi nyumbani, AJIRA zina MENGI wahanga ni WATOTO WA MASKINI.
Pole sana
 
Anyway pole, tumia ujuzi ulioupata kwa miaka hiyo 4 kufanya shughuli za kujamiii, utatoboa tuuu
 
JKT na nafasi za ajira mfano wake ni kama sahani ya chakula, wenye connection wanawapa kwanza chakula watoto wao, watoto wao wakishakula yale mabaki ndo wanapewa watu wasio na connection, Sasa kama watoto wa wenye connection ni wengi na nafasi za ajira ni chache basi nyie msio na konekshen jiandaen kukosa au wachache wenye bahati ndo watapata
 
Hujachelewa Kaka.....Kuna makampuni yanalipa poa tu yanawataka makomando Kama nyinyi.everything gonna be alright
 
wasalaam!

Miaka kadhaa nyuma nilijiunga na Jeshi la kujenga Taifa, nilipata mafunzo ya awali kwa muda wa miaka miwili kikosi fulani huko Nyanda za juu kusini.

Mwisho wa mwaka 2019 ulitokea ujenzi wa ukuta wa IKULU huko DODOMA na mimi nikiwa mmoja wa vijana nilioshiriki ujenzi huo pamoja na miradi mingine kama Hospital ya Uhuru, Uwanja wa Gwaride mpaka kupewa sifa ya Ushujaa na Ahadi ya Ajira na hayati Dr. John Pombe Magufuli baada ya kumaliza ujenzi....

Baada ya sekeseke la vijana kugoma na kulazimisha Ajira sikuwako katika kundi hilo hivyo kubaki mpk siku tuliyokwenda huko ktk Kambi ya JWTZ kwa mafunzo ya Ajira.

baada ya check up ya afya inayofanywa kabla ya kozi, niliandikwa kama UNFIT kwasababu ya usikivu hafifu wa sikio la kulia ambao sijui ulianzia wapi...


LEO hii nipo nyumbani baada ya Miaka 4 nikiwa sijui vip nitaanza upya NAHISI KUPOTEA, Sina wa kumlilia, Sina wa kumweleza inaniua taratibu na sijui KESHO ITAKUWA VIPI

Kinachouma Zaidi kuona mwenzio mwenye Shida kama yako ambaye hakushiriki ujenzi kwa miaka 2 akiendelea kuwepo katika Ajira wewe unarudi nyumbani, AJIRA zina MENGI wahanga ni WATOTO WA MASKINI.
[emoji769]Watoto wa maskini tunapata shida sana, na ukute unae mzazi ambae haamini kwy ujasiriamali na katika connection za KAZI Hana. Ni changamoto sana, unakuta kijana anatakiwa awe na shughuli ya kufanya lakini unakuta kakauka tuuu, wazazi wanatakiwa kubadilika sana
 
Pole sana mkuu, umenikumbusha mwaka 2013 pale UDSM walikuja "jeshi la anga" kutafuta wanafunzi wanaomaliza course za Engineering pale.
Kwa mujibu wao walihitaji watu 40 na kitu hivi. Ila baada ya kutupa semina na kutuonesha jinsi kupitia projector namna jeshi hilo linavyofanya kazi, tulijitikeza watu 64 hivi, wengine walikataa wakatoka nje.
Basi walifurahi sana wakasema hatukutegemea tungejitokeza kwa idadi ile. Kweli tumekua wazalendo.
Basi wakachukua CV zetu pale then wakatufanyia vipimo na kwa upamde wangu niliFITI.
Sasa wakatuambia baada ya wiki mbili tutapigiwa simu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
Mungu huyu jamani, mpaka leo nasubiri.
Ila nilikutana na jamaa flani baada ya miezi mingi kupita ambae tulikua nae kwenye hiyo ishu. Yeye alibahatika, akaniambia katika wale 64 walichukua wanafunzi 10 tu.
Basi ndo hivyo tena. Tupo tunapambana hapa Karume na soko letu
 
Sasa mkuu ulitaka uchukuliwe hivohivo na tatizo la usikivu?
 
Sasa mkuu ulitaka uchukuliwe hivohivo na tatizo la usikivu?

kumbuka niliahidiwa Ajira mkuu na zaidi si force ajira hii ila nasikitika kukosa altenative kama sitoshi jeshini tusaidiwe mahala pengine ambapo tungesukuma Gurudumu la maisha, lakini hakuna wala haijatokea anaejali.....
 
Back
Top Bottom