Leo TRA wamepita mitaa ya Manzese na kuwataka wenye maduka bila kujali ukubwa wa duka kuweka EFD machine

Leo TRA wamepita mitaa ya Manzese na kuwataka wenye maduka bila kujali ukubwa wa duka kuweka EFD machine

Mario Kejob

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2020
Posts
441
Reaction score
536
Leo TRA wamepita mitaa ya Manzese na kuwataka wenye maduka bila kujali ukubwa wa duka kuweka EFD machine na kuwalazimisha wafanya biashara kusaini form za kukubali kuweka hizo EFD katika kipindi kisichozidi siku tatu.
Miongoni wa waliolazimishwa kusaini form hizo ni pamoja na saluni, barbershop,viduka vya uchochoroni na hata baadhi ya mama ntilie wenye frame.
Wadau hili limekaaje? Ninavyoelewa mimi ni maduka yenye mtaji wa zaidi shilingi milioni tano na si kila duka au kila frame. Au serikali ilitoa waraka mwingine wa kufanya hivyo? Nimeambiwa hizo EFD huuzwa shilingi laki nane na wenye viduka hivyo sidhani kama hizo pesa wanazo.
 
Tulipe kodi sisi ni dona kantri. Tra ni janja janja swala la efd lingekua kwenye package unapewa mtu kabla ya biashara bure au kulipia nusu kwa nusu na mamlaka. Au unapewa some tax exemption ukitumia efd kwa uwakika
 
Tatizo hizo machine za EFD ni bei sana, na zimejaa mambo mengi kuipata,unajikuta unakata mataji kuipata iyo mashine.
Nasemea kwa mfanyabiashara wa kawaida wa mataji wa 5,000,000 .
 
Back
Top Bottom