GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
Akiwa mfanyakazi wa Redio Berlin Internation nchini Ujerumani, James Lembeli alikutana na binti wa Kijerumani, Birgit Lifka, wawili hawa wakaanzisha urafiki uliowapeleka kwenye uhusiano wa kimapenzi.
Kwa Lembeli uhusiano huo haukuwa wa kupoteza muda, aliamini kuwa mwanamke huyo ndiye atakayekuja kuwa mke wake na mama wa watoto wake kwa kuwa alishamridhia kwa shida na raha.
Wakati yeye akiwaza hivyo, mambo yalikuwa tofauti kwa Birgit, yeye alitaka uhakika wa maisha yake, hilo lilimfanya akatae kuja Tanzania kuishi na mwanamume huyo kwa kuwa hakuona hatima yake siku za usoni.
Katika mahojiano aliyofanya na gazeti hili, Lembeli anasimulia kisa hicho akikumbuka namna umaskini ulivyomfanya amkose mrembo huyo wa Kijerumani.
Mwanasiasa huyo mkongwe, mbunge wa zamani wa jimbo la Kahama mjini, anasema kutokuwa na kazi kuliharibu ndoto hiyo, ingawa baadaye alikuja kumpata mke wa maisha yake, Hawa Mchinja.
"Ni 'binti' mrembo wa Kimasai kutoka Arusha, alibadilisha maisha yangu kabisa, nilipomchumbia ikabidi nimwambie yule wa Ujerumani kwamba sasa nataka kuoa.
"Aliniandikia barua ya kurasa tisa, kilichoandikwa mule ni siri yangu," anasimulia Lembeli, katika mahojiano maalumu na Mwananchi yaliyofanyika Julai Mosi, jijini Dar es Salaam yakiangazia masuala mbalimbali ya kisiasa na kijamii.
Chanzo: mwananchi_official
Jidanganye tu hapo ulipo kuwa hata kama huna Hela basi Mwanamke atakupenda na kukuvumilia Maishani sawa?
Kudadadeki......!!
Kwa Lembeli uhusiano huo haukuwa wa kupoteza muda, aliamini kuwa mwanamke huyo ndiye atakayekuja kuwa mke wake na mama wa watoto wake kwa kuwa alishamridhia kwa shida na raha.
Wakati yeye akiwaza hivyo, mambo yalikuwa tofauti kwa Birgit, yeye alitaka uhakika wa maisha yake, hilo lilimfanya akatae kuja Tanzania kuishi na mwanamume huyo kwa kuwa hakuona hatima yake siku za usoni.
Katika mahojiano aliyofanya na gazeti hili, Lembeli anasimulia kisa hicho akikumbuka namna umaskini ulivyomfanya amkose mrembo huyo wa Kijerumani.
Mwanasiasa huyo mkongwe, mbunge wa zamani wa jimbo la Kahama mjini, anasema kutokuwa na kazi kuliharibu ndoto hiyo, ingawa baadaye alikuja kumpata mke wa maisha yake, Hawa Mchinja.
"Ni 'binti' mrembo wa Kimasai kutoka Arusha, alibadilisha maisha yangu kabisa, nilipomchumbia ikabidi nimwambie yule wa Ujerumani kwamba sasa nataka kuoa.
"Aliniandikia barua ya kurasa tisa, kilichoandikwa mule ni siri yangu," anasimulia Lembeli, katika mahojiano maalumu na Mwananchi yaliyofanyika Julai Mosi, jijini Dar es Salaam yakiangazia masuala mbalimbali ya kisiasa na kijamii.
Chanzo: mwananchi_official
Jidanganye tu hapo ulipo kuwa hata kama huna Hela basi Mwanamke atakupenda na kukuvumilia Maishani sawa?
Kudadadeki......!!