Letter of recommendation imemwepusha jela rafiki yangu

OK 1

Member
Joined
Oct 9, 2014
Posts
37
Reaction score
18
Habari Wanajamii.

Kuna rafiki yangu 1 tulisoma nae chuo sasa majuzi nimekutana nae tukaanza kubadilishana mawazo ya hapa na pale.
Basi akaanza kunieleza jinsi alivyonusurika kufungwa miaka mitano kwa kosa la kusingiziwa.

Ilikuwa hivi;

Huyu rafiki yangu alifanya kazi kwenye kampuni fulani hapa nchini kama procurement officer kwa muda wa miaka 10 baadae akaamua kuacha na kwenda kujiajiri.baada ya miaka 3 toka aache kazi akashangaa kampuni aliyokuwa anafanya kazi zamani wanamtafuta.mwanzoni akahisi labla wanataka kumwomba arudi tena kazini...kumbe looh alikuwa anatafutwa kwa kosa la wizi uliofanyika miaka ya nyuma wakati yeye akiwa kazini.basi kilichotokea kesi ikafika mpaka mahakamani...maskini kumbe kaka wa watu walimzingizia tu kwa alifanya fraud.

Sasa wakati kesi inaendelea mahakamani rafiki yake 1 ambae alikuwa anasoma sheria akamwuliza-kwani wewe ulipoacha kazi haukuomba barua ya recommendation?akasema niliomba na ninayo na boss wangu alirecommend vizuri kwamba kwa kipindi chote nilifanya kazi kwa uaminifu.rafikie akamwambia ndugu katafute hiyo barua iwe ushaidi mahakamani.huwezi amini ile ya recommendation ilisaidia na mahakama ilitumia kama ushaidi kwamba hana hatia.( kumbe hii issue yote alichomekewa tu mmoja wa wafanyakazi aliowaacha;yaani kuna mfanyakazi alikamatwa kwa mambo ya fraud akamsingizia rafiki yangu kwamba walikuwa wanashirikiana nae toka zamani.


Nilimpa pole kwa yaliyomkuta lakini nikabaki na swali hili;hivi kweli letter of recommendation ikiwa ni nzuri kwa mfanyakazi aliyeacha kazi inaweza ikasaidia kiasi hiki?

Karibuni wanasheria mtujuze ukweli huu nina shauku ya kujua.
 
inategemea upo sekta gani kuna sekta zingine watu wanaona bora wapotee tuu japo ni hatari sana lakini no way
 
Mkuu hizi kazi zetu ni risk sikuzote hasa sisi tulioajiriwa sekta binafsi.. Ni kuomba Mungu tu yasikukute
 
Wengi wanaotumikia vifungo kesi zao za kusingiziwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…