LHRC, ACT-Wazalendo wajitosa mauaji Ali Kibao, kada wa CHADEMA

LHRC, ACT-Wazalendo wajitosa mauaji Ali Kibao, kada wa CHADEMA

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Snapinsta.app_459011416_18338668285133657_8122613007661454742_n_1080.jpg
Snapinsta.app_458753671_18338668294133657_8169961796100603849_n_1080.jpg

Snapinsta.app_458962360_1069342657890575_4832739752087787833_n_1080.jpg
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimetaka uchunguzi wa kina ufanyike kubaini wahusika wa mauaji ya kada wa Chadema, Ally Kibao siku moja baada ya kuchukuliwa na watu wasiojulikana majina yao wala walipotokea.

Wito wa LHRC unaungana na wa Chama cha ACT-Wazalendo, kilichohoji maswali kadhaa, ikiwemo nani anayefanya matukio hayo huku kikitaka Jeshi la Polisi kuwasaka wahusika.

Kauli za wadau hao, zinakuja baada ya kupatikana kwa mwili wa Kibao, katika eneo la Ununio jijini Dar es Salaam akiwa ameuawa na uso wake ukiwa umejeruhiwa kiasi cha ndugu zake kushindwa kuutambua.

Mwili wa kibao, umekutwa katika hali hiyo siku moja baada ya kuripotiwa kuchukuliwa katika eneo la Tegeta, mbele ya Jengo la Kibo Complex, baada ya basi la alilokuwa amepanda, kuzuiwa na magari mawili.

Kutokana na tukio hilo, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimeisihi Serikali ifanye uchunguzi wa kina na haraka kubaini wahusika na wachukuliwe hatua.

Soma Pia:
Kituo hicho kimesisitiza uchunguzi huo unapaswa kuwa wa wazi ili kuondoa sintofahamu na kurudisha imani ya wananchi kwa vyombo vya ulinzi na usalama.

Mbali na LHRC, Chama cha ACT-Wazalendo nacho, kimelaani tukio hilo, kikisema kunaongeza hofu juu ya usalama na amani na kuchafua imani iliyopo kwa wananchi.
 
Nikiwa siti ya mbele ninasema kwamatukio haya bora kusiwe na waziri wa mambo ya ndani.
Hakemei,hajutii,haumii na hataki kuwajibika

Hii ni aibu kwake kama sio kwaaliye muweka hapo. Namshauri ifikapo kesho awe ameondoka ofisini kwasababu wanaopotea na kufa niwatu kama yeye
Utu ni muhimu kuliko vyeo
 
Ushauri wenu lifanyike nini kwenye hili?

..hili jambo ndugu yangu ni kubwa kuliko linavyozungumziwa hapa.

..mimi ningeshauri Raisi aunde Tume ya Uchunguzi kuchunguza matukio yaliyotokea ktk utawala wake. Na Tume hiyo iwasilishe uchunguzi wake kwa umma.

..pili, nashauri Raisi aunde Tume ya Haki, Ukweli, na Maridhiano, ambayo itapitia matukio yote tangu tupate Uhuru. Tume hii ni kama ile ya Desmond Tutu ya Afrika Kusini.

..Tatu, Raisi aunde Tume Huru ya Uchaguzi itakayoakisi maoni na mapendekezo ya wadau wote.

..Nne, Raisi aanzishe mchakato wa Katiba Mpya kwa kuzingatia maoni ya Tume ya Warioba.
 
Back
Top Bottom