LHRC: Adhabu Ya Kifo Inapoteza Nguvu Kazi!

LHRC: Adhabu Ya Kifo Inapoteza Nguvu Kazi!

chakii

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2013
Posts
20,834
Reaction score
26,217
MKURUGENZI wa Utetezi na Maboresho kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Harold Sungusia, amesema adhabu ya kunyongwa inachangia kupoteza nguvu kazi nchini.

Sungusia alitoa kauli hiyo mjini hapa jana alipokuwa akitoa mada kwenye mkutano wa Jukwaa la Wahariri nchini (TEF).

Alisema pindi mtuhumiwa anapohukumiwa kunyongwa, nchi inakuwa inazidi kupoteza nguvu kazi, kwani na yeye tayari anakuwa ameshampoteza anayetuhumiwa kumuua.

"Adhabu ya kifo sio sahihi na kwanza haimjengi mtuhumiwa, kwani na yeye anapohukumiwa kunyongwa tunakuwa tunazidi kupoteza nguvu kazi ambayo ingeweza kuzalisha na kipato kikaendelea kusaidia wale waliobaki," alisema Sungusia.

Badala yake ameishauri serikali kuwatengea magereza maalumu watuhumiwa hao ambako watakuwa wakifanya shughuli za kuzalisha na kisha fedha zinazopatikana kuhifadhiwa kwenye mfuko ambao utawasaidia wajane na yatima wanaobaki.

" Si kwamba tunawatetea watuhumiwa wa mauaji, lakini adhabu ya kifo kwake haimsaidii, kwani unapomuua na yeye tayari unakuwa umepoteza nguvu kazi ambayo ingeweza kuzalisha kipato na kikasaidia wanaobaki kuliko adhabu ya kifo," alisema Sungusia.

Pamoja na mambo mengine, Sungusia aliitaka serikali kuruhusu kufanyika kwa mikutano ya hadhara katika mikoa ya Lindi na Mtwara ambayo ilizuiwa kwa muda usiojulikana kutokana na vurugu za gesi mwaka jana.

Source: Tanzania Daima
 
Ah wapi! Sikubaliani naye kabisa.

Adhabu ya kifo ni muhimu sana iwepo.

Kama haipo kwenye sheria, basi waifanyie tu marekebisho hiyo sheria ili wale wahanga ambao hawataki mtu aliyewaulia ndugu yao asipewe adhabu ya kifo waweze kuamua kuwa hawaitaki na wale ambao wanataka muuaji anyongwe, nao wapewe fursa ya kuamua.

Jitu lililoua binadamu mwenzake kwangu nao halistahili liendelee kuishi. Nyongelea mbali kabisa.
 
teh aahaaaa heeeee. naona huyo jamaa kaishiwa hoja kabisa. tukumbuke sababu hasa ya adhabu ya kifo ni kuonya na kutisha kusababisha vifo vya wengine wasiendelee kuua watu au pia kupunguza hasira za watu walio uliwa ndugu yao .bila sheria kufanya hivyo huku mitaani kungepelekea vita za wenyewe kwa wenyewe sababu ya kulipiza kisasi.mwmbieni hoja yake haina mashiko na arudi tena shule ya sheria akasome falsafa za sheriia maana anachanganya hisia na sheria
 
tukumbuke sababu hasa ya adhabu ya kifo ni kuonya na kutisha kusababisha vifo vya wengine wasiendelee kuua watu au pia kupunguza hasira za watu walio uliwa ndugu yao.

Sababu ya adhabu ya kifo ni haki. Kujaribu kutenda haki kwa yule aliyepotezewa uhai wake.

Wewe ukiua mtu basi unapoteza na wewe haki yako ya kuishi.

Deterrent siyo sababu maana ingekuwa hivyo basi watu wasingeendelea kuua ilhali wanajua kwamba wanaweza kuhukumiwa kifo.

Mimi kama ikija kutokea nauliwa na mtu, basi ningependa huyo mtu naye auliwe tu.

Mtu akiniulia mtoto wangu, kama sitamuua mwenyewe basi ningependa sana auliwe na serikali.

Ni haki tu, na si jingine.
 
sheria imewekwa kwa ajili ya walio hai na si wafu alioyekufa hawezi pata haki bali walio salia hai
 
Back
Top Bottom