Pre GE2025 LHRC: Mamlaka itoe haki ya dhamana kwa Dkt. Slaa, ni haki yake

Pre GE2025 LHRC: Mamlaka itoe haki ya dhamana kwa Dkt. Slaa, ni haki yake

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimetoa wito kwa mamlaka zinazohusika na usimamizi wa haki kuhakikisha Dkt. Wilbroad Slaa anapatiwa haki yake ya dhamana, kufuatia kukamatwa kwake tarehe 9 Januari 2025 kwa tuhuma za kuchapisha taarifa za uongo kinyume na Sheria ya Makosa ya Mtandao.

Pia, Soma: Wakili Madeleka: Dkt. Wilbrod Slaa ataendelea kusota Magereza hadi Januari 30, 2025, kwa sababu; "Kuna ugeni wa Marais"

Dkt. Slaa alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu chini ya shauri la jinai Na. 993 la mwaka 2024, lakini alinyimwa dhamana.


TAARIFA KWA UMMA

WITO KWA MAMLAKA ZA USIMAMIZI WA HAKI KUMPA HAKI YA DHAMANA DKT. WILBROAD SLAA.


Dar es Salaam, 27 Januari 2025

Tarehe 9 Januari mwaka 2025 zililipotiwa taarifa kupitia vyombo vya habari za kukamatwa kwa mwanadiplomasia na mwanasiasa mkongwe Dkt. Wilbroad Slaa kwa tuhuma za kuchapisha taarifa za uongo kinyume na kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao Na.14 ya mwaka 2015. Siku hiyohiyo Dkt. Wilbroad Slaa alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kupitia shauri la jinai Na. 993 la mwaka 2024 kujibu tuhuma zilizokuwa zikimkabili.

Katika hali ya kushangaza licha ya kosa hilo kutokuwa miongoni mwa makosa yasiyo na dhamana kama ilivyoanishwa katika kifungu cha 148(5) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura Na. 20 kama ilivyofanyiwa mapitio mwaka 2022, Dkt. Slaa alilipotiwa kukosa dhamana baada ya Jamhuri kuwasilisha shauri dogo la kuzuia dhamana.

Kwa mujibu wa sheria za Tanzania dhamana ni haki ya kikatiba kama ilivyoanishwa katika ibara ya 13(6)(a) na 15 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 sanjali na Mikataba ya Kikanda na Kimataifa ambayo Tanzania ni nchi mwanachama.

Siku za hivi karibuni kumekuwepo na utamaduni wa vyombo vya upelelezi kuwasilisha viapo au mashauri madogo ya kuzuia dhamana kwa watu wanaotuhumiwa kuwa na makosa yenye mtazamo wa ukosoaji wa utendaji wa Serikali. Makosa mengi ya namna hii japokuwa kisheria yanastahili dhamana, kwa mfano kesi iliyokuwa inamkabili aliyekuwa Meya wa Manispaa ya Ubungo ndugu Boniface Jacob; kada wa CHADEMA mkoa wa Tanga ndugu Kombo Mbwana na watanzania wengine wengi wamekuwa wakikosa haki ya dhamana.

Ikumbukwe kuwa, mwaka 2022 Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ilifanyiwa marekebisho kwa kuongeza kifungu cha 131A ambacho kilipiga marufuku Jamhuri kuwasilisha kesi mahakamani wakati upelelezi haujakamilika. Hivyo ni muhimu kwa Jamhuri kuzingatia sheria hii kwa kutowasilisha mashauri mahakamani kama upelelezi haujakamilika.

LHRC inatoa wito kama ifuatavyo:

1. Vyombo vya upelelezi nchini kuacha utamaduni wa kuzuia dhamana kwa makosa ambayo si miongoni mwa makosa yanayoangukia chini ya kifungu cha 148(5) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.

2. Vyombo vya usimamizi wa haki kumpa haki ya dhamana Dkt. Wilbroad Slaa na watanzania wengine waliokutwa na madhila haya ya usimamizi wa haki jinai.

Imetolewa na:

Dkt. Anna Henga
Mkurugenzi Mtendaji- LHRC
IMG_2796.jpeg

IMG_2797.jpeg

 
Mzee anasikitisha sana

Lakini breki ya mdomo ni silaha Muhimu sana katika maisha
 
Screenshot 2025-01-27 150057.png

Screenshot 2025-01-27 150112.png

WITO KWA MAMLAKA ZA USIMAMIZI WA HAKI KUMPA HAKI YA DHAMANA DKT. WILBROAD SLAA.

Dar es Salaam, 27 Januari 2025

Tarehe 9 Januari mwaka 2025 zililipotiwa taarifa kupitia vyombo vya habari za kukamatwa kwa mwanadiplomasia na mwanasiasa mkongwe Dkt. Wilbroad Slaa kwa tuhuma za kuchapisha taarifa za uongo kinyume na kifungu cha 16 cha Sheria ya Makosa ya Mtandao Na.14 ya mwaka 2015. Siku hiyohiyo Dkt. Wilbroad Slaa alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kupitia shauri la jinai Na. 993 la mwaka 2024 kujibu tuhuma zilizokuwa zikimkabili.

Katika hali ya kushangaza licha ya kosa hilo kutokuwa miongoni mwa makosa yasiyo na dhamana kama ilivyoanishwa katika kifungu cha 148(5) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Sura Na. 20 kama ilivyofanyiwa mapitio mwaka 2022, Dkt. Slaa alilipotiwa kukosa dhamana baada ya Jamhuri kuwasilisha shauri dogo la kuzuia dhamana.

Kwa mujibu wa sheria za Tanzania dhamana ni haki ya kikatiba kama ilivyoanishwa katika ibara ya 13(6)(a) na 15 za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 sanjali na Mikataba ya Kikanda na Kimataifa ambayo Tanzania ni nchi mwanachama.

Siku za hivi karibuni kumekuwepo na utamaduni wa vyombo vya upelelezi kuwasilisha viapo au mashauri madogo ya kuzuia dhamana kwa watu wanaotuhumiwa kuwa na makosa yenye mtazamo wa ukosoaji wa utendaji wa Serikali. Makosa mengi ya namna hii japokuwa kisheria yanastahili dhamana, kwa mfano kesi iliyokuwa inamkabili aliyekuwa Meya wa Manispaa ya Ubungo ndugu Boniface Jacob; kada wa CHADEMA mkoa wa Tanga ndugu Kombo Mbwana na watanzania wengine wengi wamekuwa wakikosa haki ya dhamana.

Ikumbukwe kuwa, mwaka 2022 Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ilifanyiwa marekebisho kwa kuongeza kifungu cha 131A ambacho kilipiga marufuku Jamhuri kuwasilisha kesi mahakamani wakati upelelezi haujakamilika. Hivyo ni muhimu kwa Jamhuri kuzingatia sheria hii kwa kutowasilisha mashauri mahakamani kama upelelezi haujakamilika.

LHRC inatoa wito kama ifuatavyo:
1. Vyombo vya upelelezi nchini kuacha utamaduni wa kuzuia dhamana kwa makosa ambayo si miongoni mwa makosa yanayoangukia chini ya kifungu cha 148(5) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.
2. Vyombo vya usimamizi wa haki kumpa haki ya dhamana Dkt. Wilbroad Slaa na watanzania wengine waliokutwa na madhila haya ya usimamizi wa haki jinai.

Imetolewa na:
Dkt. Anna Henga
Mkurugenzi Mtendaji - LHRC
 
Huyo mzee angukwa anacheza na wajukuu pesa ipo ila anataka zaidi ningekuwa mm CDF mzee kama yule akikutwa na kesi kama ile mahakamani asiingie akiwa anatembea yaani analuka uchura na akitoka anatembea ubataubata mpaka akitoka pale hatamani kulopoka
Ukifanya hivyo, unatambua una wanao nyuma? unawatakia mema kwenye maisha yao baada ya wewe kufa au hata wakati ukiwa mzee hujiwezi..
Usiongee tu sabb una mdomo lbd km umepagawa hujui unachosema.
 
Ukifanya hivyo, unatambua una wanao nyuma? unawatakia mema kwenye maisha yao baada ya wewe kufa au hata wakati ukiwa mzee hujiwezi..
Usiongee tu sabb una mdomo lbd km umepagawa hujui unachosema.
Kwahy huyo mzee yeye alichofanya kipo sawa
 
Rule makewakeanayempelekesha akamwekeezamaa yulemzeeanalaana amekiukakiapo chaupradi mwacheaozee segedansi
 
Huyo mzee angukwa anacheza na wajukuu pesa ipo ila anataka zaidi ningekuwa mm CDF mzee kama yule akikutwa na kesi kama ile mahakamani asiingie akiwa anatembea yaani analuka uchura na akitoka anatembea ubataubata mpaka akitoka pale hatamani kulopoka
Kwa àkili hizi hata za kuandika huna, unaweza fanya upuuzi wowote kulingana na uwezo wako wa kufikiri.
 
Wakati mwingine ubinadamu utumike!
Dr.Slaa ni mzee sana, hastahili kupelekeshwa namna hivyo.
 
Haki za binadamu my $@%##
Watoto wanajisaidia porini hawawatetei
Kwanza ukiwa mtu mzima unachunga mdomo
Kelele na matusi waachiwe vijana
Wazee watoe ushauri tu
Hakuna kuwadekeza
 
Back
Top Bottom