LHRC yalaani Ukatili aliofanyiwa Edgar Mwakalebela (Sativa)

LHRC yalaani Ukatili aliofanyiwa Edgar Mwakalebela (Sativa)

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
photo_2024-06-28_10-59-33.jpg

Kituo cha sheria na haki za binadamu Tanzania (LHRC) kimelaani kikali kitendo cha kikatili alichafanyiwa Edger Mwakalebela maarufu kama Sativa.

Iliripotiwa kwamba, baada ya kutekwa, aliteswa na kushambuliwa kikatili kabla ya kupatikana katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi siku ya tarehe 27/06/2024 akiwa na majeraha makubwa katika sehemu mbalimbali za mwili wake.

LHRC imelaani vikali tukio hili kwani matukio kama haya sio tu yanapoka Haki za Binadamu na kutweza utu lakini pia yanaashiria hali ya hatari na udhaifu wa usalama wa raia.

LHRC inalaani vikali tukio la utekaji na kushambuliwa kwa Bwana Edgar na matukio yote kama haya kwa kuwa ni ukiukwaji wa moja kwa moja wa Haki za Binadamu zilivyoainishwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, ikiwemo;

Ibara 13 (6) (e) inayoweka katazo dhidi ya mateso, ukatili, na adhabu za kinyama, Ibara ya 14 inayoainisha haki ya kuishi, Ibara ya 15 inaweka haki ya usalama wa mtu binafsi na ulinzi dhidi ya vurugu sambamba na haki ya uhuru na usalama wa mtu kutokukamatwa na kuwekwa kizuizini kinyume na sheria za nchi.
LHRC inatoa wito kwa mamlaka husika;

1. Kufanya uchunguzi wa haraka na wa kina kuhusu utekaji nyara na shambulio dhidi ya Edgar Mwakabela.
2. Kuhakikisha wale waliohusika na matendo haya ya kikatili wanakamatwa na kufikishwa mbele ya sheria.
3. Kutoa huduma za matibabu na msaada wa haraka kwa Edgar Mwakabela ili kusaidia afya yake kutoka kwa maumivu ya kimwili na kisaikolojia aliyopitia.
4. Kuchukua hatua za mahususi kuweka ulinzi wa ziada wa Bwana Edgar dhidi ya kitendo hicho kujirudia.

Soma zaidi ====>> SATIVA: Nilitekwa nikapelekwa Karakana ya Polisi Oysterbay kabla ya kusafirishwa sehemu nyingine na nimepigwa risasi ya kichwa
 
Daaah madaraka yanalevya..alikuwepo mwendazake akafanya ya kufanya kisa cheo leo hayupo...na nasikia alipokaribia umauti eti alimwita cardinal pengo atubu madhambi yake ha ha ha....Sina hakika kama Mungu alisikiliza toba yake .
 
Haya matukio ya kinyama kuishia kuyalaani kwa maneno matupu pekee imeshathibitika hayataisha, hata watekwaji kwenda kufichwa karakana ya Oysterbay police station haitakuwa mara ya mwisho.

Wakina Lijenje na Adamoo walishatekwa na kuteswa kwenye vituo vyetu vya polisi, Boni yai, Lema nao wakateswa kituo cha polisi Oysterbay, kwa hali hii naamini na wengine watafuatia.

Watawala hawawezi kuwaadhibu wale wanaotufanyia ukatili, kwasababu wanafanya kwa manufaa yao, hawataki kukosolewa, siku zote wao wanataka kusifiwa tu.

Mpaka siku ile tutakapoamka sisi tunaotekwa na kuteswa kila siku, ndio mwisho wa matendo ya kihuni tunayofanyiwa na polisi yatakapokwisha dhidi yetu, sio vinginevyo.
 
Naomba kuuliza, hivi hawa jamaa wakiisha laani kama hivi, ni Nini Huwa kinafuata baada ya laana waliyoitoa?
 
View attachment 3028172
Kituo cha sheria na haki za binadamu Tanzania (LHRC) kimelaani kikali kitendo cha kikatili alichafanyiwa Edger Mwakalebela maarufu kama Sativa.

Iliripotiwa kwamba, baada ya kutekwa, aliteswa na kushambuliwa kikatili kabla ya kupatikana katika Hifadhi ya Taifa ya Katavi siku ya tarehe 27/06/2024 akiwa na majeraha makubwa katika sehemu mbalimbali za mwili wake.

LHRC imelaani vikali tukio hili kwani matukio kama haya sio tu yanapoka Haki za Binadamu na kutweza utu lakini pia yanaashiria hali ya hatari na udhaifu wa usalama wa raia.

LHRC inalaani vikali tukio la utekaji na kushambuliwa kwa Bwana Edgar na matukio yote kama haya kwa kuwa ni ukiukwaji wa moja kwa moja wa Haki za Binadamu zilivyoainishwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, ikiwemo;

Ibara 13 (6) (e) inayoweka katazo dhidi ya mateso, ukatili, na adhabu za kinyama, Ibara ya 14 inayoainisha haki ya kuishi, Ibara ya 15 inaweka haki ya usalama wa mtu binafsi na ulinzi dhidi ya vurugu sambamba na haki ya uhuru na usalama wa mtu kutokukamatwa na kuwekwa kizuizini kinyume na sheria za nchi.
LHRC inatoa wito kwa mamlaka husika;

1. Kufanya uchunguzi wa haraka na wa kina kuhusu utekaji nyara na shambulio dhidi ya Edgar Mwakabela.
2. Kuhakikisha wale waliohusika na matendo haya ya kikatili wanakamatwa na kufikishwa mbele ya sheria.
3. Kutoa huduma za matibabu na msaada wa haraka kwa Edgar Mwakabela ili kusaidia afya yake kutoka kwa maumivu ya kimwili na kisaikolojia aliyopitia.
4. Kuchukua hatua za mahususi kuweka ulinzi wa ziada wa Bwana Edgar dhidi ya kitendo hicho kujirudia.

Soma zaidi ====>> SATIVA: Nilitekwa nikapelekwa Karakana ya Polisi Oysterbay kabla ya kusafirishwa sehemu nyingine na nimepigwa risasi ya kichwa
Hali ni mbaya sana.

Hatia kali za vitendo kupinga Uovu huu zinapaswa kuchukuliwa na Watu wote ambao wanakerwa na vitendo viovu kama hivi
 
Back
Top Bottom