LHRC yatoa tamko kulaani kitendo cha mwandishi kukamatwa, inasemekana ndiye wa kwanza kuripoti tukio la RC kumlawiti mwanafunzi wa SAUT

LHRC yatoa tamko kulaani kitendo cha mwandishi kukamatwa, inasemekana ndiye wa kwanza kuripoti tukio la RC kumlawiti mwanafunzi wa SAUT

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
TAARIFA KWA UMMA

KUKEMEA UDHIBITI WA UHURU WA HABARI NA UNYANYASAJI WA WAANDISHI WA HABARI

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimepokea kwa masikitiko taarifa za kukamatwa kwa mwandishi wa habari, Bi. Dinna Maningo, aliyekamatwa nyumbani kwake Tarime, mkoani Mara, Juni 13, 2024 saa mbili usiku. Bi. Dinna amekuwa akishikiliwa katika kituo cha polisi Tarime bila tuhuma zilizosababisha kukamatwa kwake kuwekwa wazi. Leo, Bi. Dinna amesafirishwa kuelekea Mwanza, na mpaka sasa hakuna taarifa zozote kuhusu tuhuma zake zilizowekwa wazi. Kushikiliwa kwa mwandishi huyu kunaenda kinyume na Katiba na sheria za nchi hii pamoja na misingi ya demokrasia na uhuru wa habari. Kushikiliwa kwake pasipo taarifa za tuhuma zinazosababisha kushikiliwa kwake kunavunja haki zake za kikatiba kama zilivyoainishwa katika ibara ya 15-17 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika jamii ya kidemokrasia, uhuru wa vyombo vya habari ni nguzo ya uhuru wetu, inayohakikisha uwazi na uwajibikaji ndani ya taasisi zetu. Kuwekwa kizuizini kwa mwandishi wa habari bila mashtaka rasmi kunavunja misingi hii muhimu na kuibua maswali makubwa kuhusu dhamira ya kufuata sheria na haki. Tunatoa wito kwa mamlaka zilizomshikilia kumwachilia huru Bi. Dinna Maningo mara moja au kumshtaki kwa kosa maalum, kama sheria inavyotaka. Kumshikilia mwandishi wa habari bila tuhuma wazi sio tu kunakiuka haki zake bali pia kunatuma ujumbe wa kutisha kwa wanahabari wengine wanaojitahidi kuwafahamisha umma.

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinasimama pamoja na Bi. Dinna Maningo na waandishi wa habari wote wanaokabiliwa na unyanyasaji na vitisho visivyo vya haki katika harakati zao za kutafuta ukweli. Tunatoa wito kwa mamlaka husika kufuata misingi ya haki na uwazi, ambayo ni muhimu katika kudumisha imani ya umma kwa vyombo vya utekelezaji wa sheria na kulinda maadili yetu ya kidemokrasia.

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kitaendelea kufuatilia hali hii kwa karibu hadi suluhisho la haki na la kweli litakapopatikana.

Imetolewa leo tarehe 14/06/2024;

Dkt. Anna Henga
Mkurugenzi Mtendaj

====

Pia soma: MCL: Mkuu wa Mkoa adaiwa kumlawiti mwanafunzi wa SAUT
 

Attachments

Hawa walimtishia Oscar Oscar na yeye hata hajajali akaendelea kujibwagazua.

Wakae kwa kutulia hawana sumu
 
Wameanza kubweka, lakini hawaumi.

Kweli CCM kubwa kuliko serikali.

Polisi hamuwezi kushughulikia uhalifu, wasamalia wema wanafichua, badala mshukuru mnataka kuwaadhibu na kuwasababishia usumbufu.
 
Na Mm nalaani kitendo cha RC kukamatwa bila uthibitisho wa video akiwa anajilia kijambio
 
Aisee! Mama anaminya demokrasia kinoma.
TAARIFA KWA UMMA

KUKEMEA UDHIBITI WA UHURU WA HABARI NA UNYANYASAJI WA WAANDISHI WA HABARI

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimepokea kwa masikitiko taarifa za kukamatwa kwa mwandishi wa habari, Bi. Dinna Maningo, aliyekamatwa nyumbani kwake Tarime, mkoani Mara, Juni 13, 2024 saa mbili usiku. Bi. Dinna amekuwa akishikiliwa katika kituo cha polisi Tarime bila tuhuma zilizosababisha kukamatwa kwake kuwekwa wazi. Leo, Bi. Dinna amesafirishwa kuelekea Mwanza, na mpaka sasa hakuna taarifa zozote kuhusu tuhuma zake zilizowekwa wazi. Kushikiliwa kwa mwandishi huyu kunaenda kinyume na Katiba na sheria za nchi hii pamoja na misingi ya demokrasia na uhuru wa habari. Kushikiliwa kwake pasipo taarifa za tuhuma zinazosababisha kushikiliwa kwake kunavunja haki zake za kikatiba kama zilivyoainishwa katika ibara ya 15-17 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika jamii ya kidemokrasia, uhuru wa vyombo vya habari ni nguzo ya uhuru wetu, inayohakikisha uwazi na uwajibikaji ndani ya taasisi zetu. Kuwekwa kizuizini kwa mwandishi wa habari bila mashtaka rasmi kunavunja misingi hii muhimu na kuibua maswali makubwa kuhusu dhamira ya kufuata sheria na haki. Tunatoa wito kwa mamlaka zilizomshikilia kumwachilia huru Bi. Dinna Maningo mara moja au kumshtaki kwa kosa maalum, kama sheria inavyotaka. Kumshikilia mwandishi wa habari bila tuhuma wazi sio tu kunakiuka haki zake bali pia kunatuma ujumbe wa kutisha kwa wanahabari wengine wanaojitahidi kuwafahamisha umma.

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinasimama pamoja na Bi. Dinna Maningo na waandishi wa habari wote wanaokabiliwa na unyanyasaji na vitisho visivyo vya haki katika harakati zao za kutafuta ukweli. Tunatoa wito kwa mamlaka husika kufuata misingi ya haki na uwazi, ambayo ni muhimu katika kudumisha imani ya umma kwa vyombo vya utekelezaji wa sheria na kulinda maadili yetu ya kidemokrasia.

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kitaendelea kufuatilia hali hii kwa karibu hadi suluhisho la haki na la kweli litakapopatikana.

Imetolewa leo tarehe 14/06/2024;

Dkt. Anna Henga
Mkurugenzi Mtendaj

====

Pia soma: MCL: Mkuu wa Mkoa adaiwa kumlawiti mwanafunzi wa SAUT
kinoma.
 
Back
Top Bottom