Mkuu licorice root ni dawa ya kiarabu na wahindi pia wanayo ni dawa ya kutibu maradhi mengi mwilini. Kwa kiswahili licorice root ni Mizizi ya Arkisusi kama upo mjini Dares-Salaam nenda maeneo ya karibu ya Soko kuu la Kariakoo mtaa wa mkunguni na nyamwezi kuna wanaouza dawa za kiarabu aka Dawa za kisuna ulizahiyo dawa Arkisusi aka (licorice root) angalia nitaiweka ahpo pichani kw achini utaweza kuipata .Mimipia katika dawa zangu huwa ninaitumia sana kutibu maradhi mengi tu. ninakuwekea baadhi ya amtibabu yanayotibiw ana hiyo dawa ya licorice root aka Arkisusi
GESI TUMBONI (COLIC): Ikiwa mtu atakula kwa wingi vyakula vinavyoleta gesi halafu vyakula hivyo visisagike vizuri tumboni, hukusanya gesi tumboni na kufanya mingurumo humo na kumsababishia maumivu, humkosesha mtu utulivu na kumfanya kutoka jasho na machovu bila ya kufanya kazi. Mtu hujisikia mara kwa mara aende haja kubwa na akienda hapati choo. Pia humsababishia mtu kuumwa kwa mgongo au kiuno. Ikiwa gesi hii itakosa kutoka kwa njia ya haja kubwa, basi yaweza kupanda juu na kufanya presha sehemu au karibu ya moyo na kusababisha maumivu ya moyo.
TIBA: Chukua asali robo lita , unga wa arki susi vijiko vitatu vikubwa na unga wa habat soda vijiko viwili vikubwa. Koroga zote pamoja kwa kijiko. Chukua vijiko viwili vya mchanganyiko huu ukoroge ndani ya kikombe cha maji ya moto halafu yakishapoa unywe kikombe kimoja kutwa mara mbili asubuhi na jioni.
View attachment 424805