Life time usage of viagra

Life time usage of viagra

Habarini za kwenu wana jamvi, ebwana naomba kujua kuna uwezekano wa lifetime usage ya viagra? ,na je side effects ya hizi blue pills(viagra) ni zip endapo zitatumika for life time?, na je kuna dawa ya asili ambayo inaweza tibu erectile dysfunction (ED)? please, i need your views on this.
[h=1]Topic: Mume aliyefia gesti akiwa na mke wa mtu alimeza viagra[/h]

attachment.php


Gladness Mallya na
Haruni anchawa
MIEZI michache baada ya mwanaume aliyetambulika kwa jina la Hamad Kipondo kufia gesti akiwa na mke wa mpangaji mwenzake, Latifa Seleman siri imevuja kuwa alimeza dawa za kuongeza nguvu za kiume ‘viagra’.
attachment.php


Mwili wa Hamad Kipondo aliyefia gesti ukiingizwa kwenye gari.

MUME HAKUWA MHUNI!
Akizungumza na Amani kwa majonzi mazito hivi karibuni, mjane wa marehemu aitwaye Salma Abdallah ambaye ni Muuguzi Mwandamizi wa Hospitali ya Chadibwa, Ukonga Ilala jijini Dar es Salaam alisema mumewe hakuwa na tabia ya uhuni na siku ya tukio ilikuwa mara ya kwanza kukutana na mwanamke huyo.


attachment.php


Viagra.

CHANZO CHA KIFO
Kwa mujibu wa mwanamke huyo, ripoti iliyotolewa na daktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambaye ndiye aliyeufanyia uchunguzi mwili wa marehemu, ilionesha kuwa Hamad alitumia dawa za kuongeza nguvu za kiume ‘viagra’ ndiyo maana mauti yalimkuta ghafla.

attachment.php


Mwanamke aliyekuwa na marehemu gesti.
“Mume wangu alipata ajali mbaya mwanzoni mwa mwaka huu, akapata tatizo la presha na nguvu za kiume kupungua.
“Hivyo kwa mujibu wa ripoti ya daktari mtu ambaye ana presha akitumia dawa za kuongeza nguvu za kiume, hasa viagra uwezekano wa kupoteza maisha ni mkubwa. Ripoti ilisema presha ilimpanda mume wangu wakati wa tendo akafa.

attachment.php


Mke wa marehemu akifarijiwa na waombolezaji.

MWANAMKE ALIYEKUWA NA MAREHEMU AACHIKA
Kwa mujibu wa mjane huyo, mwanamke aliyekuwa gesti na mumewe siku ya tukio, Latifa aliachika kwa mumewe baada ya kutokea kwa tukio hilo kwani mume wake alimweleza hataki kumuona nyumbani kwake, kwa sasa anaishi kwa baba yake Majoe jijini Dar.

attachment.php

Mwili wa
marehemu ukiwa kwenye gari.


ILIKUWA SIKUKUU YA IDD EL FITR

Hamad alifikwa na mauti siku ya Idd Pili akiwa katika gesti moja iliyopo Kiwalani, Dar es Salaam ambapo alikuwa na mwanamke huyo.

Mazishi ya Hamad yalifanyika katika Makaburi ya Temeke, Dar huku ndugu wa marehemu wakimfutia kesi mwanamke huyo wakisema wanamwachia Mungu.


Waombolezaji wakiwa na mke wa marehemu.


DOO INASIKITISHA SANA POLENI SANA WAFIWA WABONGO MUSITUMIE VIAGRA JAMANI . VIAGRA VINAUWA JAMANI TUMIENI

DAWA ZA MITISHAMBA ANAZO TANGAZA MZIZIMKAVU HAZINA MADHARA SHAURI YENU. Ukitaka Dawa na ushauri wangu bonyeza hapa.
Mawasiliano

 
Back
Top Bottom