Ligi kuu soka Tanzania bara yarejea

Ligi kuu soka Tanzania bara yarejea

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Joined
Sep 11, 2020
Posts
69
Reaction score
105
IMG_20210210_133235_955.jpg


Baada ya kusimama kwa muda ligi kuu soka Tanzania bara inarejea tena hiyo kesho tarehe 11 Februari, ambapo mchezo wa awali utakaopigwa saa 8: 00 mchana, utaikutanisha Kagera sugar dhidi ya Gwambina. Na baadaye Coastal union atamenyana na Azam Fc majira ya saa 10:00 jioni.

Ijumaa ya tarehe 12 kabumbu litaendelea kurindima ambapo Tanzania Prisons atakuwa mwenyeji wa KMC mchezo utachezwa saa 8:00, huku Ruvu shooting akimualika Ihefu mchezo utakuochezwa saa 10:00 za jioni.

Na wikiendi itaanza kwa michezo miwili, ambapo Mwadui Fc atashuka dimbani kukipiga na Biashara United majira ya saa nane mchana huku Mbeya city akipimana nguvu na watoto wa Jangwani Young Africans mchezo utaochezwa saa 10:00 jioni.
 
Ligi inaanza tutaanza kusikia makelele ya simba na Haji Manara!
 
Natamani Yanga tupate matokeo Kama ya round ya kwanza,maana yalikuwa yana vibe Sana goli linapatikana dk za mwishon MTU mpira unaangalia kwa umakin unamzid kocha
 
Back
Top Bottom