Ligi Kuu Vodacom: Leo tar 22/2/2015

Sisi ndo Stand United CHAMA la Wana!! Tumechinja mnyama Kambarage! Na tunabaki Ligi Kuu tuwafundishe Mpira wale Waruga ruga wa Maganzo!
CC. Masuke , Makoye Matale , Amavubi na wengine wengi
Yes! Yes! Yes! Yes! Yes?


Ole wenu ninyi ambao mmeshiba sasa, kwa kuwa mtaona njaa, ole wenu ninyi mnaocheka sasa, kwa kuwa mtaomboleza na kulia.
 
Ndala lazima akalishwe.. Simba Sc ushindi kama kawa.

wewe mvua kambale pale bwawani jangwani leo kule mbeya unachezea kichapo

Hii mechi hisia zangu zinaniambia tunashinda kabisa na sio tu kurudisha goli.

Kwani mkishinda si mfurahi nyie mkuu....mlicheza na simba au mbeya city?....subirini mechi tukutane mtufunge ndio mnaweza kuiongelea simba.

Mkuu Freeland pole sana. Wewe huna makuu kama wenzako. Hata hivyo kwa hali ilivyo safari hii lazima mkae kitako.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Freeland pole sana. Wewe huna makuu kama wenzako. Hata hivyo kwa hali ilivyo safari hii lazima mkae kitako.

Mkuu....Simba inapitia wakati mgumu sana kimpira...lazima tukubali nyakati zimebadilika
Vipindi kama hivi kwenye mpira ni vya kawaida hua vinatokea kwenye timu zote.
Tatizo la timu yetu haina fighting spirit...yaani unaona kabisa hakuna ile nguvu ya ku push ushindi.
Kuna tatizo la msingi la kufanyiwa kazi....Lakini pia lazima tukubali ushindani sasa ni mkubwa.
Hongereni yanga ....walau nyie mko kwenye form kwa ligi yetu....kibongo bongo mnajitahidi
 

Mkuu Freeland baada ya lile Bonanza la Mapinduzi mlijiaminisha kuwa timu yenu ni nzuri. Hebu rejea hii post yangu wakati mlipokuwa mnatesa, linganisha na yale yaliyotokea kule Mbeya! https://www.jamiiforums.com/sports/785684-live-update-mapinduzi-cup-8-01-2015-a-13.html#post11608211
 
Mkuu Freeland pole sana. Wewe huna makuu kama wenzako. Hata hivyo kwa hali ilivyo safari hii lazima mkae kitako.
Ni upepo tu mkuu utapita na furaha itarejea, kawaida kwenye familia kama mti mkubwa wa kivuli ukishaanguka inahitaji muda na rasilimali nyingi kukuza mti mwingine, hasa kama dhamira ya kukuza huo mti ipo.

Ninachoona kwenye familia yetu dhamira ya kweli ya kukuza mti kwa sasa ni ndogo, kuna mgawanyo wa majukumu, wengine kuleta mche wa mti mzuri, wengine kuchagua sehemu nzuri ya kupanda huo mche, wengine kuchimba shimo la kupandia, wengine kupanda huo mche, wengine kuweka mbolea na wengine kumwagilia maji asubuhi na jioni.

Huenda kuna wengine hawatimizi majukumu yao vizuri, tutafanya juu chini kujua tatizo liko wapi maana hatuoni mti wetu ukikua kama tulivyotarajia, hatujajua mti umedumaa labda si aina ile tuliyoitaka tutahangaika na aliyeleta mche, kama tatizo ni sehemu ulipopandwa au shimo halikuchimbwa vizuri au aliyeweka mbolea hakuweka vizuri au pengine haumwagiliwi maji tutajua tatizo liko wapi na kulitatua na hatimaye mti wetu utakuwa mkubwa na kivuli kitarejea kwenye familia yetu ngoja kwa sasa wakati tunajua tatizo tukae juani ili tujue uzuri wa kuwa na mti mzuri na mkubwa wa kivuli.
 
Last edited by a moderator:

Mkuu.....Nikurekebishe kwanza...lile halikuwa bonanza.....Yalikua ni mashindano ya Kombe la Mapinduzi yanayochezwa kila mwaka kwa mwaka wa nane sasa ili kuyaenzi mapinduzi ya Zanzibar.

Na ukweli ni kwamba Simba ndiyo ilikua bora katika mashindano hayo na ilichukua Kombe....Sasa ujue mambo hua yanabadilika

Timu yetu japo ina changamoto za kawaida lakini sio mbooooovuuuu kihivyo kama picha unayotaka wewe kuionesha hapa...Pamoja na ubovu huu unaoudhania lakini hata ninyi (Mnaodhani mko bora sana kwa sasa) hamnao uwezo wa kuifunga hii simba mbovu.

Ubovu wetu ni relative,Kwa maana ya kwamba tumeshindwa ku meet expectations.
Tutalishughulikia tatizo la Msingi......Tutarudi kuwa sawa tu...lakini kwa ubingwa wa ligi kuu hatutauchukua
 

Huo mti usiwe wa 'kivuli' (mashabiki) tu bali uweze kutoa 'matunda' (magoli).
 
Mkuu hizo ni tafsiri zako, za kwangu zinabaki kama nilivyokusudia.

Sawa Mkuu, tukumbushane tarehe 27/02/2015 kabla ya Sabato kuingia nitafungua uzi maalum kwa ajili ya kukupongeza wewe kwa kufikisha umri wa miaka 7 hapa JF (28/02/2008 - 28/02/2015), hongera sana Mkuu.
 
Kwani mkishinda si mfurahi nyie mkuu....mlicheza na simba au mbeya city?....subirini mechi tukutane mtufunge ndio mnaweza kuiongelea simba.

Ahhh ahhh.! Hisia zako zinaniambia "Kumfunga YANGA ndio ubigwa KWENU." pongezi ziwafikie Mkuu.

Sisi ubigwa wetu ni VPL.

Uko simba hamna kitu mkuu, utakufa na presha mtani... Nenda AzamFC angalau kwa mkopo huenda ukanenepaga.
 

Nasikia bado mna kale ka msemo kenu "LIGI BADO CHANGA/MBICHI"...!
 
Ahhh ahhh.! Hisia zako zinaniambia "Kumfunga YANGA ndio ubigwa KWENU." pongezi ziwafikie Mkuu.

Sisi ubigwa wetu ni VPL.

Uko simba hamna kitu mkuu, utakufa na presha mtani... Nenda AzamFC angalau kwa mkopo huenda ukanenepaga.

No, no, no! Mkuu Freeland asiende Azam tutamkosa mtani mstaarabu sana, hebu angalia wale wa kinyume chake, wako wapi sasa? Wote wamesepa kabaki yeye tu na Mkuu Masuke. Mkuu Katavi naye namuona kwa mbali kanuna kwelikweli kwenye avatar yake sijui atakenua lini!
 
Last edited by a moderator:
Sawa Mkuu, tukumbushane tarehe 27/02/2015 kabla ya Sabato kuingia nitafungua uzi maalum kwa ajili ya kukupongeza wewe kwa kufikisha umri wa miaka 7 hapa JF (28/02/2008 - 28/02/2015), hongera sana Mkuu.

Mbona wako wengi sana wametimiza hiyo miaka saba hujawafungulia uzi? Nisikukatishe tamaa tutakumbushana mkuu. Miaka saba si haba kama ni mtoto anakaribia la nne kwa hawa wa siku hizi ila enzi zetu bado ni umri wa kuchunga ndama na kondoo, mbuzi wenyewe wanaweza kukuzingua na ukaishia kulambwa viboko.
 
Ahhh ahhh.! Hisia zako zinaniambia "Kumfunga YANGA ndio ubigwa KWENU." pongezi ziwafikie Mkuu.

Sisi ubigwa wetu ni VPL.

Uko simba hamna kitu mkuu, utakufa na presha mtani... Nenda AzamFC angalau kwa mkopo huenda ukanenepaga.

Mkuu pole sana...Bahati mbaya wengine sio mashabiki wa mihemko

Hiki kipindi ni cha mpito tu...Kinatokea hata kwa timu kubwa duniani huko....We are not an exception to that.

Naipenda sana simba na nitaendelea kuipenda siku zote........

Kuifunga Yanga sio ubingwa wa VPL lakini pia nataka utambue kuwa pamoja na "ubovu" wetu,timu yenu "bora" haina uwezo wa kutufunga
 

Asante kwa taarifa.
Ila Yanga hatuna mtazamo hasi, ya kwamba kumfunga simba ni compulsory.
Huwa tuna angalia mbele zaidi tena kimahesabu.

Ila mkuu, huwezi kumfunga YANGA unless umeenda visiwani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…