Ligi kuu ya England lazima iishe

kombaME

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2015
Posts
2,115
Reaction score
2,818
Ambacho hamkijui ile ligi watu wananunua tiketi za msimu mzima tena sio watu tu hadi mashirika huwalipia watu mbalimbali, haki za Tv hulipwa msimu mzima, matangazo, wadhamin na mambo mengi hufanywa Kwa msimu, sasa kufuta ligi maana yake ni epl ivunje mkataba, kwa kufanya hivyo italipa fedha nyingi sana na inaweza kufirisika kabisa, kwahiyo afe beki afe kipa ligi lazima ifike mwisho.

Tena ni heri ligi ichelewe kuisha uhairishwe msimu ujao kuliko kufuta msimu huu. Haiwezekani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ambacho hamkijui ile ligi watu wananunua tiketi za msimu mzima tena sio watu tu hadi mashirika ...

Yaani mtu hata kuandika hujui, eti habari za PL umezijua halafu sisi wote humu hatuzijui!
 
Hakuna ambae atapata faida kwenye hili janga la COVID19 labda watengeneza barakoa ambao ni chinese tofauti na hapo ni hasara kwa kila mtu hao Epl na hao watu wa tiketi sijui haki za Tv wengi wao wamekubali mambo yaishe ndio maana pale UK ligi za chini sana zimefutwa zote nadhani imebakia ligi kuu championship ila mashabiki wa Liver ndio wenye kutaka ligi isifutwe
 

Kumbuka pia kwenye mkataba kuna mambo yanaweza kuvunja mkataba. Mambo kama Vita,Majanga asilia na Gharika mbalimbali.

Hivyo kama Ligi itafutwa Hamna kudaiana hapo ni Gharika la Corona ndio Limesababisha. Natural Imeamua.
 
Mkuu siku nyingine Usianzishe uzi kama huna data Sawa??
 
Ukweli uliomchungu kwa mahasimu wa liverpool hawapendi kusikia ligi inaendelea au liverpool kapewa kombe, wasikie ligi imefutwa wanafurahi sana tena mno.

Ila uhalisia utabakia palepale game zitapigwa hata twice a week ndani ya mwezi mmoja na week 2 ligi imeisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…