Ligi ya mikoa ya mpira wa miguu iliwahi kuwepo hapa Tanzania?

lloydsam

Member
Joined
Nov 8, 2015
Posts
42
Reaction score
55
Namaanisha mfano wa timu hixo ni kama.. Tanga FC, Arusha FC, Mwanza Fc, Dar Es Salaam FC

Wadau, naomba kujuzwa kama tuliwahi kuwa na Ligi ya mikoa ya mpira wa miguu, na kama ilikuwepo.. Ilikuwa katika mfumo gani, Timu zake zilikuwa ni zipi, FIFA ilikuwa inahusika??? Ilikuwq ligi ya timu ngapi, Kombe lake lilikuwa nini, ilianzishwa wakati gani na Kwanini haipo tena kwasasa?
 
Hiyo ligi ipo kwa muda mrefu tu na inaanzia ngazi ya wilaya ili kumpata bingwa wa mkoa ambaye atashindanishwa na mabingwa wenzake wa mikoa mingine. Washindi wanaingia ligi daraja la pili kama sikosei.
Timu yoyote ile hata ya mtaani kwako ikijisajili kwenye chama cha mpira wa miguu cha wilaya, ikikidhi vigezo na masharti ina sifa ya kushiriki. Fifa haihusiki na hivi viligi vidogo vidogo! Tff ndiye mlezi na msimamizi wao. Mimi ni mdau tu wa michezo na shabiki mwaminifu wa timu ya wananchi Tanzania.
 
Iliwahi kuwapo na kama sikosei mara ya mwisho ilifanyika 2010 hivi!!. Na fainali ilikuwa ni timu ya Mwanza bila shaka na Ilala au Kinondoni ambazo zilichukuliwa kama mikoa.!!

Vivitio vikubwa katika ligi ile ilikuwa ni wachezaji wa Ligi kuu waliowakilisha mikoa yao huku Kigoma ikiwa na wachezaji wengi wa Ligi kuu, kina Kaseja na wengineo!!

Nimejaribu kukumbuka japo sina hakika sana na kumbukumbu ila Ligi ilikuwepo na ilikuja kumezwa na Copa Coca Cola ambayo nayo ilikuwa ni Ligi ya Mikoa kwa vijana
 
Ligi ya mikoa ilikuwepo tangu miaka ya sabini hadi miaka ya tisini ilipositishwa kwa sababu ya ukata kama sikukosea.Mara ya mwisho kuisikika ni 2010 ambapo kama alivyoshuhudia mdau hapo juu, ilihusisha timu ya Mwanza na Dar es salaam. Miaka hiyo ligi ikifahamika kama kombe la Taifa, ilianzia ngazi ya wilaya bila kuhusisha kabisa klabu za mpira..... inangawa zilitoa wachezaji wake kushiriki.

Kombe la Taifa kama ilivyojulikana ndio ilikuwa kitalu cha kupata wachezaji wa kuunda timu ya Taifa. Mikoa iliyokuwa mbele kama chimbuko la wachezaji wenye vipaji ilikuwa ni Kigoma, Tanga, Morogoro, Shinyanga na Tabora. Wachezaji wenye vipaji waliweza kuonekana katika wilaya zilizokuwa mbele kwenye ushiriki wa michezo ya UMISETA, Michezo ya mashirika na majeshi..... Imebakia historia tu baada ya kuelekeza nguvu kubwa kwenye klabu za mpira wa miguu.
 
Hizi timu zilikuwepo ndio lakini mambo yalifanywa kisiasa zaidi na vision yake (nadhani) ilikuwa ni kuleta 'umoja wa kitaifa' badala ya kuleta ushindani wa mpira ambao ungepelekea maendeleo ya mchezo wenyewe.
Ukiangalia kombe la sasa la shirikisho ndilo linareflect hayo mashindano ya kitaifa (Lweru eagles, Mwanza Heroes, Mzizima Unite nk) lakini tatizo za hizi timu ilikuwa ni kuishia kupeana mikono na wanasiasa. Alafu ilikuwa kama 'combaini' za mikoa na kwa maana hiyo mikakati ilikuwa haioni mbali zaidi ya siku 365! Zingelikuwa ni clubs za kudumu mpira wetu usingekuwa umepoteza vipaji vingi kama vilivyopotea, naamini Samatta angelikuwa na wenzie wengi tu.
 
Ipo Kama Sikosei Singida(kindai) Alikuwa Bingwa Wa Mwisho Yalipo Rudishwa,kocha Akiwa Matola Selemani Wa Lipuli Daq Zilitoka Timu Mbili Temeke, Kinondoni Kama Mikowa Kisoka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…