ward41
JF-Expert Member
- Apr 3, 2022
- 749
- 2,533
Ligi ya Ukraine imerudi rasmi leo kwa mara ya kwanza tangu Urusi ilipoivamia Ukraine mwezi Februari mwaka huu.
Kutokana na sababu za kiusalama, mashabiki hawakuruhusiwa kuhudhuria mechi ya kwanza iliyochezwa kati ya timu za Shakhtar na Metalist katika uwanja wa Kyiv Olympic.
Hifadhi za dharura zenye kuzuia mabomu zimewekwa tayari karibu na uwanja ikiwa zitahitajika.
Nahodha wa timu ya Shakhtar ameeleza kuwa "tunazo kanuni zetu ikiwa kengele italia wote tutaenda kwenye mahandaki"
"Tuko tayari, tuna nguvu, na nafikiri tutaionyesha dunia kuwa bado tupo, na kama wanavyofanya askari wetu nasi tunapambana kwa ajili ya Ukraine."
Kutokana na sababu za kiusalama, mashabiki hawakuruhusiwa kuhudhuria mechi ya kwanza iliyochezwa kati ya timu za Shakhtar na Metalist katika uwanja wa Kyiv Olympic.
Hifadhi za dharura zenye kuzuia mabomu zimewekwa tayari karibu na uwanja ikiwa zitahitajika.
Nahodha wa timu ya Shakhtar ameeleza kuwa "tunazo kanuni zetu ikiwa kengele italia wote tutaenda kwenye mahandaki"
"Tuko tayari, tuna nguvu, na nafikiri tutaionyesha dunia kuwa bado tupo, na kama wanavyofanya askari wetu nasi tunapambana kwa ajili ya Ukraine."