Likizo zisizo na malipo

Likizo zisizo na malipo

kanewi

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2012
Posts
298
Reaction score
200
ndugu wanaJF naomba mnisaidie kuhusu sheria za kazi zinasemaje kwa hii tetesi ninayo isikia,.Mimi ni mtumishi wa MAMLAKA YA RELI YA TANZANIA NA ZAMBIA(TAZARA) ambapo kwa kipindi kirefu sana imekuwa ikijiendesha kwa hasara inayo sababishwa na urasimu pamoja na rushwa inayo lipelekea kushindwa kilipa mishahara ya watumishi kwa mda mrefu sana ikafika kipindi ambapo Waziri Nundu alifikia kipindi cha kuwasimamisha wakurugenzi saba kwa tuhuma mbalimbali lkn waziri alietangulia Dr Mwakyembe aliwarudisha kwa kigezo cha kukiukwa kwa taratibu za kisheria,sasa kuna tetesi kuwa Mamlaka imeshindwa kujiendesha na kukwama kwenye masuala muhimu ya kiutawara ambapo inazamilia kutoa likizo kwa baazi ya wafanyakazi wake bile malipo,.naomba mnisaidie kwa wanasheria kuhusu suala la Mwajiri kumsimamisha mafanyakazi wake mwenye mkataba wa kudumu na shirika kusimamishwa bila ya malipo,.
 
hiyo haipo kabisa ndg, utalipwa nusu mshahara kama kuna issue, bila malipo haipo hiyo
 
Hata nusu mshahara hulipwa pale palipo na matatizo kwa mfanyakazi mfano kuumwa au kusimamishwa kazi lakini kwa hili atalipwa malimbikizo ya mshahara pale atakaporudishwa kazini.. Refer Labour Law Rules
 
Mwajiri hawezi kukupa likizo bila malipo unless unaomba mwenyewe. Anapaswa akustaafishe kazi na kukulipa haki zako kutegemeana na mkayaba wa hiari. Tatizo hao viongozi wenu trl wameshakuwa wachumia tumbo, hawaangalii tena chama cha wafanyakazi wanampamba mhindi!

Poleni aisee. Mpigie kura tena ccm 2015 eeh.
 
Mwajiri hawezi kukupa likizo bila malipo unless unaomba mwenyewe. Anapaswa akustaafishe kazi na kukulipa haki zako kutegemeana na mkayaba wa hiari. Tatizo hao viongozi wenu trl wameshakuwa wachumia tumbo, hawaangalii tena chama cha wafanyakazi wanampamba mhindi!

Poleni aisee. Mpigie kura tena ccm 2015 eeh.

hii ni mamlaka inamilikiwa na mataifa mawili tanzania na zambia kwa 50% share mhindi hamna humu lkn serikali yatu inashindwa kutoa matamko kuhusiana hili na taharifa zinawafikia kila siku lakini naibbu waziri nazani ndo alietoa pendekezo hili,.thax kwa ushauri huu ila kama kuna labour law nyingine naomba mnisaidie,vipi waziri KABAKA anausikaje na suala hili?
 
Back
Top Bottom