Linah na jingles za clouds, shikamoo

sixgates

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2011
Posts
3,979
Reaction score
1,665
Hapa jamvini tunawazungumzia sana wakina chibu monde, mara kiba. hadi tunawasahau akina omy dimpoz...

Ila mnikubalie hapa katikati ni kama ndege mnana Linnah sanga alikumbwa na mauza uza, tuliokuwa tunampenda tukasema ndo kapotea.

Bahati nzuri clouds wakaja na kampeni ya malkia wa nguvu ambapo linah ndo ametumika katika jingles zote.

Nyota yake imerudi upya baada ya kuwa balozi wa kampeni hiyo ambayo kiukweli mawingu wamejipanga kwenye ubunifu hadi kufanikiwa kuiteka siku ya wanawake duniani.

Huo wimbo nadhani hata kama ni wa Clouds bado umempa kiki sana hauchoshi.
 
Ngoja niitafute, au km unayo itume hapa mkuu
 
Yaa nyimbo nzuri, ila mpangilio wa mavazi na mazingira haviendani, linah angevaa kitamaduni pale nje ya ile nyumba ya msonge, au angeimba nje ya nyumba ya maana huko masaki kwa mavazi haya aliyo vaa. Ila kazi nzuri.
 
Yaa nyimbo nzuri, ila mpangilio wa mavazi na mazingira haviendani, linah angevaa kitamaduni pale nje ya ile nyumba ya msonge, au angeimba nje ya nyumba ya maana huko masaki kwa mavazi haya aliyo vaa. Ila kazi nzuri.
Huo utamaduni umebaki kwenye fikra tu! Kuna haja gani ya kuvaa kitamaduni Wakati Watanzania wenyewe sio watamaduni, tumejaa u-fake tu, hata vazi la kutu identify hatuna! Muache Lina avae atakavyo, SISI HATUNA UTAMADUNI, mambo ya utamaduni yalikoma 1999!
 
Wangeacha audio tu, video wamevurunda na Lina hana mvuto! She's trying soooo hard kuwa beyoncé.
Bora umeliona hilo, havina uhalisia kabisa kati ya muimbaji na mazingira. Nimeambiwa nimuache Linah kisa nchi haina vazi lla Taifa na utamaduni ulikoma 1999! Aisee nimeshindwa kumjibu.
 
Nilimuona Valentine day pale escape 1 walikua wanaimba live alifunikwa vibaya na Ruby,Alice na Maua Sama!Linah ni mwimbaji wa kawaida aliyepewa airtime na wadau wanaoamua nani atoke!kwa walioona lile Onesho la valentine wamenielewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…