Boran Jakutay
Senior Member
- Apr 8, 2023
- 110
- 259
Kijana aitwaye Hassan Ally Mnali (32) Mkazi wa Mtaa wa Jamhuri, kata ya Msinjahili, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi amefariki baada ya kujinyonga usiku ikidaiwa kuwa kabla ya kujiua alikuwa akilalamika kuna Watu wanamvuruga.
Ndugu wa Marehemu wanasema hawafahamu sababu ya kujinyonga lakini mdogo wa marehemu Rashid Ally Mnali anasema kuwa kaka yake hakuwa sawa kiakili kwa madai kuna Watu wanamvuruga.
Shuhuda wa tukio hilo Salma Stambuli anasema alishtushwa usiku na kelele za Mama wa Marehemu akimtaka kufika Nyumbani kwake kumpatia msaada ambapo baada ya kufika alimkuta Hassan ameshafanya maamuzi hayo.
Chanzo: Millard Ayo
Ndugu wa Marehemu wanasema hawafahamu sababu ya kujinyonga lakini mdogo wa marehemu Rashid Ally Mnali anasema kuwa kaka yake hakuwa sawa kiakili kwa madai kuna Watu wanamvuruga.
Shuhuda wa tukio hilo Salma Stambuli anasema alishtushwa usiku na kelele za Mama wa Marehemu akimtaka kufika Nyumbani kwake kumpatia msaada ambapo baada ya kufika alimkuta Hassan ameshafanya maamuzi hayo.
Chanzo: Millard Ayo