Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Mbunge wa Jimbo la Mchinga, Mhe. Salma Rashid Kikwete, ameshiriki katika zoezi la uandikishaji wa wakazi lililofanyika kijijini Ruvu, kitongoji cha Makasini, kata ya Mchinga, Jimbo la Mchinga, mkoani Lindi.
Soma pia: Freeman Mbowe ajiandikisha Uchaguzi Serikali za Mitaa
Akizungumza na viongozi wa chama pamoja na wananchi wa kijiji cha Ruvu leo, tarehe 17 Oktoba 2024, baada ya kushiriki zoezi hilo, Mhe. Salma Kikwete aliwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la mkazi na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji, na vitongoji utakaofanyika tarehe 27 Novemba 2024.
Aidha, alitumia fursa hiyo kuwahimiza wanawake wa jimbo la Mchinga kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi za uongozi zilizotangazwa kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji, na vitongoji.
Soma pia: Freeman Mbowe ajiandikisha Uchaguzi Serikali za Mitaa
Akizungumza na viongozi wa chama pamoja na wananchi wa kijiji cha Ruvu leo, tarehe 17 Oktoba 2024, baada ya kushiriki zoezi hilo, Mhe. Salma Kikwete aliwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la mkazi na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji, na vitongoji utakaofanyika tarehe 27 Novemba 2024.
Aidha, alitumia fursa hiyo kuwahimiza wanawake wa jimbo la Mchinga kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi za uongozi zilizotangazwa kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji, na vitongoji.