Lini CCM itatoka madarakani?

Ni suala la muda tu japo sijui itachukuwa muda gani. Unajua CCM itaondolewa na nani? Itaondolewa na jeshi inayozidi kulitengeneza yenyewe. Trust me. Angalia haya makundi. 1. Bodaboda 2. Machinga 3. Umati wa vijana usio na ajira. Haya makundi ni hatari sana na ni suala la muda tu. Itahitajika ''cheche'' ndogo sana kuwasha moto ambao unaweza kuchukuwa miaka 20 kuutuliza, na Tanzania haitakuwa tena hii ya sasa. Siku zote mabadiliko yanayokuja kwa njia hii huyumbisha nchi kwa muda mrefu na likitokea tatizo dogo tu wananchi hutumia njia za vurugu kulitatua.
 
Itoke ili iweje? Ili Iongoze chama gani, umezoea spoon feeding siyo? Pambana ushawishi wananchi upewe fursa ya kuongoza serikali. Sasa chama km CHADEMA ndiyo kiongoze nchi, kweli? Hamko serious, nchi siyo kikoba.
 
1. Katiba mpya itokanayo na Rasimu alosimamia Judge WARIOBA ndo itasababisha CCM itoke madarakani Kwa njia ya AMANI.

2. Njia ngumu ya maandamano yasiyo na kikomo.
3. Siku ambayo vyombo vya dola (polisi, jeshi, usalama) wakikataa kutumika kuiba kura, huo ndio utakuwa mwisho wa ccm.

4. Siku kizazi cha 90,2000, 2010 kikiwa kwenye mifumo mbalimbali ya kiserikali na kwenye vyombo vya dola. Maana wanapata tabu sana na ukosefu wa ajira na hali ngumu. Hao madogo wakiwa wengi sana na wakapenyapenya kwenye mifumo mbalimbali ya taifa hili ccm lazima watoke madarakani hata kwa passive resistance, na ndio itakuwa mwisho wa ccm.


5. Mapinduzi ya kijeshi. Yaani inapigwa mijegeje ikulu, nchi yote kimyaaaaaaaaaaaa. Hakuna mtu kutoka wala kuingia. Halafu tbc na tv zooooote, online tv za YouTube zooooote na radio zoooote zinakata matangazo na zinajiunga live toka ikulu, halafu njemba zenye mijegeje zinatoa hotuba kuwa tumepindua na leo ndio mwisho wa ccm.




NB: wapinzani elekezeni nguvu zenu pia kwenye vyombo vya dola. Wanajeshi, polisi, usalama. Mkielekeza nguvu huko na mkapata uungwaji mkono wa hao watu. Ccm ni wepesi kuliko manyoya
CC: Erythrocyte Mshana Jr fikisheni ujumbe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…