Ekyoma
JF-Expert Member
- Dec 30, 2015
- 2,177
- 2,804
LIPULI YAMTOA KWASI KWA TSH. MILIONI 25
Uongozi wa klabu ya Lipuli FC inayoshiriki ligi kuu Tanzania Bara umeridhia maombi ya klabu ya Simba ya kumsajili beki wake raia wa Ghana, Asante Kwasi, kwa ada ya uhamisho ya shiilingi milioni 25.
Taarifa iliyotolewa na idara ya habari na mahusiano ya Lipuli FC imeeleza kuwa tayari Simba imekamilisha taratibu zote za usajili zinazohitajika na hivyo kuanzia sasa Asante Kwasi ni mchezaji halali wa Simba SC.
“Uongozi wa Lipuli FC unakiri kupokea barua yenye ombi la kumtaka mchezaji tajwa hapo juu na kwa kauli moja umeridhia kumaliza sintofahamu hiyo kwa kumruhusu mchezaji Asante Kwasi kwenda Simba SC kwa ada ya uhamisho ya kiasi cha shilingi milioni 25,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.
Uongozi wa klabu ya Lipuli FC inayoshiriki ligi kuu Tanzania Bara umeridhia maombi ya klabu ya Simba ya kumsajili beki wake raia wa Ghana, Asante Kwasi, kwa ada ya uhamisho ya shiilingi milioni 25.
Taarifa iliyotolewa na idara ya habari na mahusiano ya Lipuli FC imeeleza kuwa tayari Simba imekamilisha taratibu zote za usajili zinazohitajika na hivyo kuanzia sasa Asante Kwasi ni mchezaji halali wa Simba SC.
“Uongozi wa Lipuli FC unakiri kupokea barua yenye ombi la kumtaka mchezaji tajwa hapo juu na kwa kauli moja umeridhia kumaliza sintofahamu hiyo kwa kumruhusu mchezaji Asante Kwasi kwenda Simba SC kwa ada ya uhamisho ya kiasi cha shilingi milioni 25,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.