Lipumba: Wanawake nchini hawapati huduma bora wakati wa kujifungua, nichagueni kuwa rais nitatoa huduma bora ya afya na kudhibiti vifo vya wajawazito

Lipumba: Wanawake nchini hawapati huduma bora wakati wa kujifungua, nichagueni kuwa rais nitatoa huduma bora ya afya na kudhibiti vifo vya wajawazito

CUF Habari

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2019
Posts
239
Reaction score
234
IMG_20200926_115110_433.jpg
WANAWAKE NCHI HII HAWAPATI HUDUMA BORA WAKATI WA KUJIFUNGUA NICHAGUENI KUWA RAIS WA NCHI HII NITATOA HUDUMA BORA YA AFYA NA KUDHIBITI VIFO VYA WAJAWAZITO NA WATOTO."PROF.LIPUMBA

BUKOBA MJINI


Nitahakikisha kuwa Bajeti ya Wizara ya Afya inapanda na kufikia asilimia 15 ya
Bajeti ndani ya miaka 10 ijayo. Ongezeko la bajeti litawezesha katika kuandaa miundombinu ya kisasa, wataalam, vifaa tiba na vipimo vya kutosha kwa
maradhi yote.

Aidha ongezeko la bajeti litawezesha kutenga fungu maalum kwa ajili ya kukabili maradhi ya milipuko kama COVID-19 kwa kadri yatakavyojitokeza. Ili kuhakikisha kuwa kila raia ana haki na anapata
huduma za msingi za afya, Serikali ya umoja wa kitaifa chini ya CUF itahakikisha asilimia 70 ya Watanzania wote wana Bima ya Afya ifikapo 2025 na asilimia 100 ifikapo 2028.

Hatua maalumu zitachukuliwa kuhakikisha
kuwa huduma za uzazi bila malipo zinapatikana kwa kila mama mjamzito ili
kupunguza vifo vingi vinavyotokea ambavyo vinadhibitika.

"Hii miaka mitano hali ya maisha ilivyokuwa ngumu, vijana wa Katoro mmetubadilishia msemo mnasema vyuma vimekaza, sasa ndugu zangu mwenye glisi (Grease) ya kulegeza hivyo vyuma vilivyokaza ni Prof.Ibrahim Haruna Lipumba"

"Hali ya umasikini inazidi, mzunguko wa fedha unazidi kupungua, vijana wa Katoro mnazeeka kabla ya wakati wenu". Prof Ibrahim Lipumba
 
View attachment 1581981WANAWAKE NCHI HII HAWAPATI HUDUMA BORA WAKATI WA KUJIFUNGUA NICHAGUENI KUWA RAIS WA NCHI HII NITATOA HUDUMA BORA YA AFYA NA KUDHIBITI VIFO VYA WAJAWAZITO NA WATOTO."PROF.LIPUMBA

BUKOBA MJINI


Nitahakikisha kuwa Bajeti ya Wizara ya Afya inapanda na kufikia asilimia 15 ya
Bajeti ndani ya miaka 10 ijayo.

Ongezeko la bajeti litawezesha katika kuandaa
miundombinu ya kisasa, wataalam, vifaa tiba na vipimo vya kutosha kwa
maradhi yote.

Aidha ongezeko la bajeti litawezesha kutenga fungu maalum
kwa ajili ya kukabili maradhi ya milipuko kama COVID-19 kwa kadri
yatakavyojitokeza.

Ili kuhakikisha kuwa kila raia ana haki na anapata
huduma za msingi za afya, Serikali ya umoja wa kitaifa chini ya CUF
itahakikisha asilimia 70 ya Watanzania wote wana Bima ya Afya ifikapo 2025
na asilimia 100 ifikapo 2028.

Hatua maalumu zitachukuliwa kuhakikisha
kuwa huduma za uzazi bila malipo zinapatikana kwa kila mama mjamzito ili
kupunguza vifo vingi vinavyotokea ambavyo vinadhibitika.
Ale kwanza alizolipwa na CCM 2015. Mwenzake Dr mihogo yuko majuu huko anakula kiyoyozi
 
Back
Top Bottom