Elections 2010 Lisa M Rockerffeller urge Tanzanians to reject Kikwete a 2nd Term

Status
Not open for further replies.

Lisa M Rockefeller T. So if your leaders let people into the country to mine your gold and a throw away price, that is not a question for me to answer, it is you and your leaders to answer... what did your leaders get in return for letting barrick into Tanzania, and what did you get a common man apart from the craters? I am sure you are a indian, do you pay taxes in Tanzania@Thakur?See More
43 minutes ago
 

Kaka tukitokea katika hoja yako naomba nikujibu kama ifuatavyo:
- Americans particularly politicians they are after their country interests (patriotism) but sikubaliani nawe kwa individuals americans ambao they will like to see maisha mazuri mahali. Mfano nakupa Bill Gates anamwaga kila siku mabilioni Tanzania katika project za malaria na ukimwi. Hivyo sikubaliani na mtazamo wako kuwa mzungu anapokosoa utawala wetu. Hiyo ni uzalendo wa hali ya juu pengine kutushinda sie ngozi nyeusi ambao uzalendo wetu wengi ni after pesa (wakenya wanasema Chapaa).

- Kuhusu mkwawa aliuwawa usitake kugusa machungu ya watu for sympathetic support mbona wakati wa mkoloni kulikuwa na matarishi weusi kama sie waliokuwa kazi yao kwenda kupeleka siri za waafrika kwa wazungu? Binafsi naona sawa mzungu kutukosoa kwasababu by the way wao ndio wanatupa pesa za kuishi hapa mjini (for your information 40% of our national budget comes from donors who happens to be wazungu). Hivyo wana haki kama sie kutukosoa wanapoona kodi zao zinaenda sipo.

Lete hoja nyengine kaka!!!
 
- Ni afadhali nisikilize hoja za Mtikila au Dr. Slaa, kuliko huyo Mkoloni ajali mambo ya taifa lake ya Tanzania atuachie wenyewe!

William!

Huwezi kuuzungumzia Ukoloni wa Lisa wakati kibindoni una Green Card ya Nchi yake
 
Acha Unafiki wewe, Mmewafukuza huku Mnamiliki Passport zao, Shame on you

- Similiki passport ya taifa lolote bro zaidi ya taifa langu Tanzania, samahanai sana personal hazina nafasi hapa tunajadili ishus muhimu za taifa hasa dakika hizi za mwisho kabla ya uchaguzi, tusiharibiwe amani yetu na hawa wakoloni.

William.
 

CCM bana na wapambe wake kwa conspiracy theory tu mwisho!!! Kila la kheri mkuu lakini jiulize anayoyasema ni kweli au si kweli?
 
Huu ni upumbavu sana kutetea kunyonywa nchi yetu eti tuna haki ya kuamua kugawa vyetu. Hoja ni mufilisi sana na ndizo zimetufikisha hapa. Tunakaribisha mawazo ya kujenga yawe ya kutoka ndani au nje. Nampongeza sana Lisa kumpa vipande vyake Kikwete na wale wote ambao wanachekelea nchi yetu kunyonywa kama mazuzu.
 

'Wazungu' wasingeweza kutuibia bila ya ushirikiano wa magavana na machifu wao akina JK , Sani Abacha et al.
 

Mdondoaji hao Ndivyo walivyo

Wazungu Wakitusifia, Tunapiga hadi Simu kwenye Kampeni kuwakoga wapiga Kura ila Wazungu hao hao wakituchamba tunawaita kila aina ya majina Mabaya

Heri Mzungu akutukanaye na kukuonesha Udhaifu wako kuliko Mzungu anayekusifia ili akunyonye
 

Na lini utawaambia mafisadi wa thithiem warudishe pesa nyingi walizotuibia Watanzania? au huzijui? 😛eace:😛eace:😛eace:
 
Huyo Malecela rais wake ni Obama au Kikwete? Hawa watu tayari wameshafaidika na Nafasi za baba zao sasa wakiona kuna watu wanakomaa nao wanaona kama maslahi yao yanaingiliwa, wameshazoea kuponda Kodi zetu tu

- Rais wangu ni Dr. Kikwete, sina tatizo siasa za taifa langu kukomaliwa na kina Slaa, Mtikila na wengineo lakini sitaki siasa zangu kuingiliwa na mzungu mkoloni, hapa tunajadili taifa sio binafsi maana hazina nafasi hapa kwenye uwanuja wa Great Thinkers!


William.
 
- Similiki passport ya taifa lolote bro zaidi ya taifa langu Tanzania, samahanai sana personal hazina nafasi hapa tunajadili ishus muhimu za taifa hasa dakika hizi za mwisho kabla ya uchaguzi, tusiharibiwe amani yetu na hawa wakoloni.

William.

Huwezi kutenganisha Hoja na mtu ndio maana na wewe unakwenda personal na Lisa, Ungekuwa unapenda Kujadili Hoja Ungejadili Mantiki ya Kile Lisa alichokizungumza
 
- Similiki passport ya taifa lolote bro zaidi ya taifa langu Tanzania, samahanai sana personal hazina nafasi hapa tunajadili ishus muhimu za taifa hasa dakika hizi za mwisho kabla ya uchaguzi, tusiharibiwe amani yetu na hawa wakoloni.

William.
Mkulu 'Personal' unaruhusiwa wewe tu au?

Mbona umemhusisha Lisa na 'uwizi' wa Rocafela et c bila kujadili hoja zake?
 

Ahaa, Wakija akina Bush wakiwasifia Kilemba cha Ukoka Mnakenua Meno lakini akina Lisa wakiwachamba kwa Ufisadi wanakuwa Wakoloni
 

Waambie basi na mafisadi waliojaa thithiem ambao ndiyo chanzo cha umaskini mkubwa na kukosa kwa maendeleo katika nchi yetu watuachie nchi yetu badala ya kuendelea kuiba mabilioni ya shilingi kila awamu kuanzia awamu ya pili
 
Ninaunga mkono hoja za Lisa na ametuonyesha kile ambacho Kikwete huwa anafanya anapokuja huku nje. Ni mapenzi yake kwa nchi yetu kutaka tuache kunyonywa na kuongozwa na watu wasiostahili kutuongoza. Ninapinga wale wote wanaojifanya wazalendo huku wao ndio ambao kwa nasaba zao na uwezo mdogo wa wazazi wao ambao walikuwa viongozi wetu ndio waliosaini mikataba ya shanga kama ile ya Chifu Mangungo uko Usagara na Lewanika huko Zambia. Nitamtetea huyu dada kwa nguvu zangu zote na hawa ndio watu wa kushirikiana nao kupambana na viongozi uchwara wa nchi zetu pamoja na Benki ya Dunia na IMF.
 

Anachokiongea huyo dada ni confirmation ya kile tunachokiongea JF kila siku, nashangaa unamshambulia yeye badala ya kuona kumbe wengi blacks and whites wako fed up na Kikwete na CCM yake.

Unachofanya ni kukimbia hoja in the name of mkoloni. Humanity has no borders wala skin color mkuu na ndio maana dunia haikuwaachia Haiti wahangaike kivyao.

Watu wana uchungu na humanity sio wewe unaridhika na status quo eti kwa sababu wewe na familia yako mnanufaika. Selfishness inakusumbua ndugu yangu.
 
- Ni afadhali nisikilize hoja za Mtikila au Dr. Slaa, kuliko huyo Mkoloni ajali mambo ya taifa lake ya Tanzania atuachie wenyewe!

William!

Mkuu umesema vizuri. sometime kina mtikila lipumba na slaa wana hoja nzuri ila wale wanaotakiwa kusizikiliza na kuzifanyia kazi hawazisikilizi. Na nyie mlio karibu na Desicon Makers mnaogopa kutoa new ideas, challenge na kuwa critical hata pale mnapojua mko sahihi.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…