SI KWELI Lissu akiri kufukuzwa Ofisini na Mbowe

SI KWELI Lissu akiri kufukuzwa Ofisini na Mbowe

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu, amesema Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe amemzuia kwenda katika ofisi kutokana na yeye kueleza ubadhirifu unaofanywa ndani ya chama.

Pia Lissu amesema sababu nyingine ya kuzuiwa kwenda katika ofisi hizo ni kutokana na kutoa siri za vikao ndani ya chama, na kumueleza ukweli kuhusu kitendo cha kuanzisha taasisi nyingine ndani ya CHADEMA.

Aidha Mwanahalisi ina nakala rasmi ya barua ya siri ambayo Mbowe amemwandikia Lissu kwa kumpiga zuio la kwenda ofisini.
IMG_20240907_181246_953.jpg
 
Tunachokijua
Tundu Lissu ni Mwanasheria ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema lakini pia aliwahi kuwa mbunge wa jimbo la Singida mashariki mwaka 2010 hadi mwaka 2020

Kupitia kipindi cha Dakika 45, cha ITV Agosti 26, 2024 Lissu akielezea uhusiano wake na mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe aliwahi kusema uhusiano wake na Mwenyekiti ni mzuri na hawajawahi kugombana lakini kupo kutofautiana kwa misimamo ya kisiasa akisema kuwa ni jambo la kawaida kutokana na kuwa wao ni watu wawili wenye mitazamo tofauti, na watu hutumia mwanya huo kukuza mambo na kuonesha kama kuna mgogoro baina yao.

Mapema leo, Septemba 7, 2024, kumekuwa na taarifa ambayo imekuwa ikisambaa mtandaoni ikimtaja makamu mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu kuwa amekiri kuzuiwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe kwenda ofisini kutokana na kueleza ubadhirifu unaofanywa ndani ya chama hicho.

Sehemu ilipochapishwa taarifa hiyo ni hapa, hapa na hapa.

Ukweli wa jambo hili upoje?
Ufuatiliaji wa kimtandao uliofanywa na JamiiCheck umebaini Lissu hajazungumza maneno haya.

Mathalani, kwa kutumia Keyword Search ("Amemzuia kwenda katika ofisi") kama sehemu ya maneno yanayopatikana kwenye ujumbe huo, JamiiCheck haikupata ushahidi muhimu unaoelekea kwenye kurasa rasmi za Mwanahalisi, CHADEMA, Lissu mwenyewe, mtu au chombo chochote cha habari cha kuaminika.

Kwa kutumia Google Reverse Image Search, JamiiCheck imebaini kuwa ujumbe huu haujawahi kuchapishwa kwenye kurasa za mitandao ya kijamii ya Mwanahalisi Digital kama inavyodaiwa kwani hakuna kumbukumbu rasmi zinazoonesha historia ya ujumbe huo kuwahi kuchapishwa mtandaoni na ukurasa huo.

Kwa kurejea mpangilio wa utengenezaji wa Graphics zinazotumiwa na ukurasa wa Mwanahalisi digital, JamiiCheck imegundua mapungufu kadhaa ya Graphic inayosambaza uzushi huo ikiwemo kukosekana kwa mstari mweupe unaotenganisha sehemu ya juu ya maneno ‘Mwanahalisi Digital” na sehemu ya chini unapoandikwa ujumbe wa picha husika. Pia, Aina ya mwandiko (fonts) unaotumiwa na gazeti la mwanahalisi ni tofauti na ule unaoonekana kwenye ujumbe unaosambazwa mtandaoni.

Aidha, Septemba 7, 2024, muda mfupi baada ya kusambaa kwa taarifa hii, Kurasa rasmi za Mwanahalisi zilikanusha kuhusika nayo, na kuwaomba watu waipuuze kwani ilianzishwa na watu wenye nia ovu ili kufanikisha malengo yao binafsi.

Pia, Chanzo chetu cha kuaminika kimethibitisha kuwa Lissu karibu wiki ya 3 hayupo ndani ya nchi, na hivyo kutupa uhakika zaidi juu ya uzushi wa taarifa ya Lissu kufukuzwa au kuzuiwa kuingi ofisini na Mbowe.
mbowe saccos hiyo lissu anaingilia mambo ya watu kapigwa kibutiiiiii
 
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (𝘾𝙃𝘼𝘿𝙀𝙈𝘼) Tundu Lissu, amesema 𝑴𝒘𝒆𝒏𝒚𝒆𝒌𝒊𝒕𝒊 𝒘𝒂 𝒄𝒉𝒂𝒎𝒂 𝒉𝒊𝒄𝒉𝒐 𝑭𝒓𝒆𝒆𝒎𝒂𝒏 𝑴𝒃𝒐𝒘𝒆 𝒂𝒎𝒆𝒎𝒛𝒖𝒊𝒂 𝒌𝒘𝒆𝒏𝒅𝒂 𝒌𝒂𝒕𝒊𝒌𝒂 𝒐𝒇𝒊𝒔𝒊𝒏𝒊 𝒌𝒖𝒕𝒐𝒌𝒂𝒏𝒂 𝒏𝒂 𝒚𝒆𝒚𝒆 𝒌𝒖𝒆𝒍𝒆𝒛𝒂 𝒖𝒃𝒂𝒅𝒉𝒊𝒓𝒊𝒇𝒖 𝒖𝒏𝒂𝒐𝒇𝒂𝒏𝒚𝒘𝒂 𝒏𝒅𝒂𝒏𝒊 𝒚𝒂 𝒄𝒉𝒂𝒎𝒂.)

Pia Lissu amesema sababu nyingine ya kuzuiwa kwenda katika ofisi hizo ni kutokana na kutoa siri za vikao ndani ya chama, na kumueleza ukweli kuhusu kitendo cha kuanzisha taasisi nyingine ndani ya CHADEMA.

Aidha Mwanahalisi ina nakala rasmi ya barua ya siri ambayo Mbowe amemwandikia Lissu kwa kumpiga zuio la kwenda ofisini.
===========
Habari kama hizi mnawaandikiaga watu wa namna gani?! Na huwa wanaamini hizi taarifa?
 
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (𝘾𝙃𝘼𝘿𝙀𝙈𝘼) Tundu Lissu, amesema 𝑴𝒘𝒆𝒏𝒚𝒆𝒌𝒊𝒕𝒊 𝒘𝒂 𝒄𝒉𝒂𝒎𝒂 𝒉𝒊𝒄𝒉𝒐 𝑭𝒓𝒆𝒆𝒎𝒂𝒏 𝑴𝒃𝒐𝒘𝒆 𝒂𝒎𝒆𝒎𝒛𝒖𝒊𝒂 𝒌𝒘𝒆𝒏𝒅𝒂 𝒌𝒂𝒕𝒊𝒌𝒂 𝒐𝒇𝒊𝒔𝒊𝒏𝒊 𝒌𝒖𝒕𝒐𝒌𝒂𝒏𝒂 𝒏𝒂 𝒚𝒆𝒚𝒆 𝒌𝒖𝒆𝒍𝒆𝒛𝒂 𝒖𝒃𝒂𝒅𝒉𝒊𝒓𝒊𝒇𝒖 𝒖𝒏𝒂𝒐𝒇𝒂𝒏𝒚𝒘𝒂 𝒏𝒅𝒂𝒏𝒊 𝒚𝒂 𝒄𝒉𝒂𝒎𝒂.)

Pia Lissu amesema sababu nyingine ya kuzuiwa kwenda katika ofisi hizo ni kutokana na kutoa siri za vikao ndani ya chama, na kumueleza ukweli kuhusu kitendo cha kuanzisha taasisi nyingine ndani ya CHADEMA.

Aidha Mwanahalisi ina nakala rasmi ya barua ya siri ambayo Mbowe amemwandikia Lissu kwa kumpiga zuio la kwenda ofisini.
===========
Hata kama Habari hii itakuwa ya kweli, usaliti ni jambo la kawaida kabisa miongoni mwa Wanasiasa waliopo kwenye Vyama vya Siasa.
That's why Watu wa kawaida wasiofungamana na vyama vya Siasa wanataka Katiba Mpya iliyo nzuri kwa hapa Tanzania, Katiba itakayoruhusu Wanasiasa huru na Wagombea huru katika nafasi mbalimbali za Uongozi bila ya kuwa na Itikadi za Vyama vya Siasa.
 
Kuamini katika vyama pinzani ni kujitafutia msongo wa mawazo na kifo Cha mapema.
 
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (𝘾𝙃𝘼𝘿𝙀𝙈𝘼) Tundu Lissu, amesema 𝑴𝒘𝒆𝒏𝒚𝒆𝒌𝒊𝒕𝒊 𝒘𝒂 𝒄𝒉𝒂𝒎𝒂 𝒉𝒊𝒄𝒉𝒐 𝑭𝒓𝒆𝒆𝒎𝒂𝒏 𝑴𝒃𝒐𝒘𝒆 𝒂𝒎𝒆𝒎𝒛𝒖𝒊𝒂 𝒌𝒘𝒆𝒏𝒅𝒂 𝒌𝒂𝒕𝒊𝒌𝒂 𝒐𝒇𝒊𝒔𝒊𝒏𝒊 𝒌𝒖𝒕𝒐𝒌𝒂𝒏𝒂 𝒏𝒂 𝒚𝒆𝒚𝒆 𝒌𝒖𝒆𝒍𝒆𝒛𝒂 𝒖𝒃𝒂𝒅𝒉𝒊𝒓𝒊𝒇𝒖 𝒖𝒏𝒂𝒐𝒇𝒂𝒏𝒚𝒘𝒂 𝒏𝒅𝒂𝒏𝒊 𝒚𝒂 𝒄𝒉𝒂𝒎𝒂.)

Pia Lissu amesema sababu nyingine ya kuzuiwa kwenda katika ofisi hizo ni kutokana na kutoa siri za vikao ndani ya chama, na kumueleza ukweli kuhusu kitendo cha kuanzisha taasisi nyingine ndani ya CHADEMA.

Aidha Mwanahalisi ina nakala rasmi ya barua ya siri ambayo Mbowe amemwandikia Lissu kwa kumpiga zuio la kwenda ofisini.
===========
Member tangu 2017, post 7 tu! ngoja tukudukue na kukuanika
 
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (𝘾𝙃𝘼𝘿𝙀𝙈𝘼) Tundu Lissu, amesema 𝑴𝒘𝒆𝒏𝒚𝒆𝒌𝒊𝒕𝒊 𝒘𝒂 𝒄𝒉𝒂𝒎𝒂 𝒉𝒊𝒄𝒉𝒐 𝑭𝒓𝒆𝒆𝒎𝒂𝒏 𝑴𝒃𝒐𝒘𝒆 𝒂𝒎𝒆𝒎𝒛𝒖𝒊𝒂 𝒌𝒘𝒆𝒏𝒅𝒂 𝒌𝒂𝒕𝒊𝒌𝒂 𝒐𝒇𝒊𝒔𝒊𝒏𝒊 𝒌𝒖𝒕𝒐𝒌𝒂𝒏𝒂 𝒏𝒂 𝒚𝒆𝒚𝒆 𝒌𝒖𝒆𝒍𝒆𝒛𝒂 𝒖𝒃𝒂𝒅𝒉𝒊𝒓𝒊𝒇𝒖 𝒖𝒏𝒂𝒐𝒇𝒂𝒏𝒚𝒘𝒂 𝒏𝒅𝒂𝒏𝒊 𝒚𝒂 𝒄𝒉𝒂𝒎𝒂.)

Pia Lissu amesema sababu nyingine ya kuzuiwa kwenda katika ofisi hizo ni kutokana na kutoa siri za vikao ndani ya chama, na kumueleza ukweli kuhusu kitendo cha kuanzisha taasisi nyingine ndani ya CHADEMA.

Aidha Mwanahalisi ina nakala rasmi ya barua ya siri ambayo Mbowe amemwandikia Lissu kwa kumpiga zuio la kwenda ofisini.
===========
Wewe ndio uliandika Mnyika ajiuzulu ukatibu Mkuu, Jamiicheck ikakudhalilisha, leo tena umekuja na lingine bado unachekewa tu! Sasa subiri!
 
Wewe ndio uliandika Mnyika ajiuzulu ukatibu Mkuu, Jamiicheck ikakudhalilisha, leo tena umekuja na lingine bado unachekewa tu! Sasa subiri!
Mbona vitisho vimekuwa vingi mzee?
Kama imekuuma si unaipisha tu ipite?
Huwezi kujua inaweza kuwa kweli au si kweli,
Au wewe ndio lisu? Au mbowe?
 
Back
Top Bottom