SI KWELI Lissu ameitwa na kamati kuu CHADEMA kwa kuvujisha siri za chama

SI KWELI Lissu ameitwa na kamati kuu CHADEMA kwa kuvujisha siri za chama

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
TAARIFA INAYODAIWA KUTOLEWA NA TBC SI YA KWELI.jpg
 
Tunachokijua
Tundu Lissu ni Makamu mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa ambaye pia ametangaza nia ya kugombea uenyekiti wa CHADEMA kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika January, 2025.

Tangu Lissu alipotangaza nia ya kugombea nafasi hiyo dhidi ya Mwenyekiti anayemaliza muda wake ambaye naye pia ni mgombea wa nafasi hiyo Freeman Mbowe kumekuwepo na mivutano mikali baina ya wafuasi wa viongozi hao na wakati mwingine pia baina yao wenyewe wagombea kupitia mahojiano mbalimbali wanayokuwa wakiyafanya kwenye vyombo mbalimbali vya habari na majukwaa mengine. Tazama hapa, hapa, hapa na hapa

Tarehe 31/12/2024 kumeibuka barua ambayo imekuwa ikisambazwa katika mitandao ya kijamii ikieleza kuwa siku ya jumatatu ya tarehe 6/01/2025 kamati kuu ya CHADEMA itafanya kikao maalumu kwa ajili ya kumjadili Lissu ambaye ni Makamu mwenyekiti kwa kuvujisha taarifa za ndani ya chama na kutoa kauli na tuhuma za uongo zinazotolewa mitandaoni dhidi ya viongozi mbalimbali wa chama.

Uhalisia wa barua hiyo upoje?

JamiiCheck imefanya ufuatiliaji kuhusu barua hiyo iliyowasilishwa na mdau wa JamiiCheck.com akihitaji kupata uhlisia wake ikiwa na grafiki ya TBC digitial inayomilikiwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na kubaini kuwa taarifa hiyo si ya kweli na haijatolewa na TBC digital.

JamiiCheck imefanya ufuatiliaji wa kimtandao na kubaini kuwa taarifa ama barua hiyo haijachapishwa katika kurasa za mitandao za TBC digital kama inavyoonekana kwenye grafiki hiyo. Lakini pia ufuatiliaji wa kimtandao katika kurasa za mitandao ya kijamii ya CHADEMA tumebaini kutokuwepo kwa barua wala taarifa kuhusiana na kuwepo kwa kikao hiko na kwa siku ya leo 31/12/2024 CHADEMA wamechapisha taarifa kuhusu kuachiwa huru kwa George Sanga na wenzake ambapo wameandika katika ukurasa wao wa X;

“Leo Desemba 31, 2024 Mahakama Kuu - Njombe imewaachia huru George Sanga na wenzake baada kukaa gerezani kwa siku 1555 kwa tuhuma za mauaji.” Tazama hapa na hapa

Aidha tumefuatilia katika ukurasa wa mtandao wa X zamani ikijulikana kama Twitter wa Katibu mkuu wa CHADEMA John Mnyika ambaye pia katika kurasa zake hajaandika wala kuchapisha barua hiyo.

Mkurugenzi wa itifaki, mawasiliano na mambo ya nje wa CHADEMA Jon Mrema kupitia ukurasa wake wa X amekanusha taarifa hiyo na kuwataka wananchi waiipuuzie kwa kuwa ni uzushi. Tazama hapa
Kampeni zimepamba moto. Sisi wa nje tunasubiri matokeo tu
 
HUU MPASUKO NDANI YA chadema UNAMASLAI MAPANA KWA TAIFA

WACHA VYUMA VISAGANE
 
hata kwa zito kabwe lilitengenezwa zengwe mpaka zito akasalimu amri akakimbia na kwenda kuanzisha chama chake.
 
Tundu
Slaa
Anzisheni timu mpya,
 
Hii taarifa siyo official, haipo kwenye chanzo chochote cha CHADEMA.
 
Back
Top Bottom