Lissu ameshinda kwa asilimia 2 dhidi ya Mbowe. Ni kashfa ya Abdul imehusika au ilikuwa ni muda wa Mbowe kuondoka?

Lissu ameshinda kwa asilimia 2 dhidi ya Mbowe. Ni kashfa ya Abdul imehusika au ilikuwa ni muda wa Mbowe kuondoka?

Eli Cohen

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2023
Posts
4,460
Reaction score
13,715
2% ni ndogo sana, lakini ndio hio ilioamua ushindi.

Je hizi tuhuma alizotoa lissu dhidi ya wenje ndio zimecheza part kubwa ya "narrow win" yake au ni basi watu angepata support ya kushinda pasipokuwa na scandal ile.
 
Mbowe amefanya kazi kubwa kujenga chadema.. no wakati umeamua.. wanachama wanataka sura mpya na techniques mpya kukabili chama dola hasa kwenye uchaguzi
Sawa sawa mkuu
 
Lissu kuwa mwenyekiti, ni mfumo umeamua.. ulinzi ulikuwa tight sana.. tunawapongeza vyombo vyote vya usalama..hawakuingilia kabisa mtifuano wa uchaguzi.. watu/raia walikuwa huru,hadi wengine walilala viwanja vya mlimani City..
 
Lissu kuwa mwenyekiti, ni mfumo umeamua.. ulinzi ulikuwa tight sana.. tunawapongeza vyombo vyote vya usalama..hawakuingilia kabisa mtifuano wa uchaguzi.. watu/raia walikuwa huru,hadi wengine walilala viwanja vya mlimani City..
Hakika
 
2% ni ndogo sana, lakini ndio hio ilioamua ushindi.

Je hizi tuhuma alizotoa lissu dhidi ya wenje ndio zimecheza part kubwa ya "narrow win" yake au ni basi watu angepata support ya kushinda pasipokuwa na scandal ile.
……pia ndiye alishamuandalia shimo la kupoteza urais.
 
Uchaguzi wa chadema ulivyoendeshwa,hadi mamlaka wakashindwa kumpitisha mtu wao..iwe ni welcome call kwa ccm na SSH.. kuna jambo litatokea uchaguzi mkuu 2025..
 
2% ni ndogo sana, lakini ndio hio ilioamua ushindi.

Je hizi tuhuma alizotoa lissu dhidi ya wenje ndio zimecheza part kubwa ya "narrow win" yake au ni basi watu angepata support ya kushinda pasipokuwa na scandal ile.
Muda uliwadia
 
2% ni ndogo sana, lakini ndio hio ilioamua ushindi.

Je hizi tuhuma alizotoa lissu dhidi ya wenje ndio zimecheza part kubwa ya "narrow win" yake au ni basi watu angepata support ya kushinda pasipokuwa na scandal ile.
Me nadhani hiyo scandal ya Abdul ndo imempandishia kura Mbowe na kumpunguzia Lissu kura. Nikiwa namaanisha kama kweli baadhi ya wajumbe walilamba maokoto ya Abdul kupitia kwa bwana Mbowe hivyo kushawishika kumpigia Mbowe
 
2% ni ndogo sana, lakini ndio hio ilioamua ushindi.

Je hizi tuhuma alizotoa lissu dhidi ya wenje ndio zimecheza part kubwa ya "narrow win" yake au ni basi watu angepata support ya kushinda pasipokuwa na scandal ile.

Hudhani %2 ilikuwa ni psychological warfare na kuwa huyo ndugu wangeweza kusema kashinda kwa kura 1?

Kwani cuf maalim hawakuwa wakishindwa hata kwa nusu kura isiyokuwa na maelezo mpigaji ni nani?

Gh1FxbQXQAAf6RI.jpeg


Au ushindi hubadilika zikuwa % ngapi ndugu?
 
Ila nimesikitika sana kwa mbowe kuzidiwa 2% tu my expectation ilikuwa mbowe asipate hata kura 1 ,kwa kuzidiwa kwa 2% tu inaonyesha kumbe fascist mbowe alikuwa ana jeshi la wahuni wenzake
 
Huko CCM wameshindwa hata kushindana kwenye fomu ya ugombea urais ni mtu anatoa jina kwenye mkoba anajipitisha.

Chadema wamepishana 2% kura zimepigwa live mbele ya camera za wanahabari na mshindi ameonekana na aliyeshindwa ameonekana.
IMG_5053.jpeg
 
KWA NINI FAM TONGE ^LIMEMNYANG'ANYWA^?
1. Corruption scandal
2. Muda wa mabadiliko umebisha hodi
3. Poor combination ya Mbowe na Wenje.

Mbali na corruption scandal, Wenje alipwaya sana kwenye hiyo nafasi. Hana uzoefu wa kimawasiliano. Anapaniki haraka. Anajibu kwa kuridhika (anakosa passion yake binafsi, tofauti na wagombea wengine). Anajibu kwa mashaka na kujichanganya mwenyewe. Hana analosimamia na kutetea. Haoni mbele, bali anahofia mbeleni.

Hajui kabisa kupangua hoja na kujichotea pwenti hata kama amekuwa implicated kwenye kashfa fulani. Kwa mfano, TAL aliulizwa kwa nini hakuwajibika kujiuzulu baada ya kuhusika kumpitisha mgombea Wenje ambaye wakati huohuo anamtuhumu kuwa ana viashiria vya rushwa? (Hoja nzito na yenye mashiko kabisa)!

Lakini mstari mmoja tu wa TAL ulitosha kuwashawishi wajumbe kukubaliana naye: ^Mimi siwezi kuwajibika kwa madhambi ya mtu mwingine!^ Japo kimsingi hakujibu swali aliloulizwa, lakini kwa kauli hiyo na msisitizo uliofuata, tayari alikuwa amechukua pointi 3 muhimu!

Kwa upande mwingine, Wenje kila akijaribu kujibu ndipo anaharibu sana. Mbaya zaidi, hasikilizi hoja na kuikata kwa sentensi ya kwanza wakati akiijibu. Mzungumzaji anapojibu hoja fulani, lazima sentensi ya kwanza iwe dhahiri shahiri kiasi cha kujibu kwa muhtasari utata wote ulioibuliwa. Kauli zinazofuata ni kama ufafanuzi tu. Sanaa hii TAL na FAM wameimudu barabara!

4. Matarajio hewa. FAM na wapambe waliingia uwanjani na ushindi wao. Kuna shabiki mmoja aliahidi wangepanda ushindi wa zaidi ya 90%!!! Huku ni kujiamini kupitiliza - ambako bila shaka kuliwafanya wajumbe wa kati (ambao wako kotekote) waamue kuegemea kwa TAL - kulikosababisha anguko lake mwishowe.

5. 20 + 1 years!!! If you know, you know! According to TAL: Mitano tena italeta kitu gani kipya?

6. PPP - percentage of personal purity. Wengi wajumbe walimwona FAM kama mostly Sisiemu kuliko CDM, wakati TAL, kama alivyosema mwenyewe, msimamo wake unajulikana kwa wote.

7. Sera sintofahamu na utendaji usioridhisha: suala tata la maridhiano, matumizi ya fedha za chama, hatua (gani?) zilizochukuliwa katika chaguzi za nyuma zinazoaminiwa kuporwa, uimarishaji wa chama hasa hivi karibuni, chama kujiendesha yenyewe, suala zito na nyeti la Katiba Mpya na athari yake kuhusu uchaguzi mkuu ujao, nk.

8. Kihoja FAM<<<<<TAL. Unaweza kuthibitisha hili vizuri kabisa kwa hotuba ya hawa miamba wawili wakati wakiomba kura. Zingatia utamu na mvuto wa maneno (ufasaha) na hoja za msingi. Hotuba zote zimetulia kiufasaha na kimantiki, lakini kihoja na kiushawishi, mmoja anapwaya sana.

9. Timing. Wajumbe wanahoji: Nini hasa kilichomfanya FAM kugombea tena - maana ni kana kwamba alikuwa ameshaamua kukaa pembeni, halafu baadaye akashinikizwa (na nani?!), ndipo akaitisha ile press nyumbani kwake, akatangaza kuwachwana (challenge) wapinzani wake ^kwa boksi.^ Hofu hiyo ya wajumbe ikajitafsiri kwenye matokeo.

10. Busara na uelewa wa TAL. Wengi walitegemea, siku ya uchaguzi TAL angehamaki na kuwaparua na kuwararua kwa jazba wapinzani wake mbele ya wajumbe.

Lakini mambo yakawa kinyume chake. Kama ambavyo FAM alitulia tuli na kuvaa uungwana wote wa mwanakondoo, TAL naye akapita mulemule. Japo hakulegea kimsimamo, alijivika sura ya uvumilivu na kuahidi umoja na ushirikiano hata kama angeshindwa.

Nadhani hiyo ilimpa TAL pointi nyingi mno. Wengi walihofia angekihama CDM (kama Mchungaji PM). Lakini kauli yake ya kubaki CDM hata ingetokea akashindwa, na pia ahadi ya kuendeleza mapambano yake kwa ajili ya kujenga chama, viliwapa tumaini kubwa wajumbe na kuwafanya wamwone kama kinara asiyepaswa kupotezwa kamwe!

11. Uwazi katika upigaji kura.
 
Back
Top Bottom