residentura
JF-Expert Member
- Mar 1, 2017
- 8,146
- 11,434
Ni "hawaimudu" na sio " awahimudu".Mimi najua sampuli ya wachangiaji wa clubhouse na uelewa wao
wa siasa.
Vita yangu ya siasa awahimudu, duh.
Mimi nilishatoka huko uelewi somo tu. A/H sio kigezo cha akili.Ni "hawaimudu" na sio " awahimudu".
Neno moja la kiswahili, tena la kawaida huwezi kuliandika, hiyo vita ya siasa utaiwezea wapi!!???
Huwezi kuwa na hoja kama huwezi kuijenga hiyo hoja ikaeleweka.Mimi nilishatoka huko uelewi somo tu. A/H sio kigezo cha akili.
Jenga hoja
Huna uwezo tulia pembeni.
Tuzo ilitolewa na BAWACHA si FAM. Hivi ninyi wagombea wa nafasi ya m/kiti Taifa Chadema ni shetani Gani anawavuruga Hivyo? Mimi ningependa mfanye UCHAGUZI wa kidemokrasia na isimamiwe na Watu wanaokubalika hasa wasio na masilahi na chama au TLS. Tupate matokeo sahihi Kwa kutumia sanduku la kura na si vinginevyo.Wadau hamjamboni nyote?
Jisomeeni wenyewe hapo chini kwa kiswahili
Jambo TV
Akizungumza kupitia mtandao wa Clubhouse usiku huu, Lissu ameeleza kuwa Rais Samia alialikwa na Mbowe kushiriki katika mkutano wa Baraza la Wanawake la CHADEMA (BAWACHA), na walijulishwa tu kuwa mwaliko huo umetoka kwa Mwenyekiti.
Ameongeza kwa kusema kuwa, walishangaa kuona tuzo ikitolewa kwa Rais Samia bila kujulishwa mapema, huku kamati kuu ya chama hiyo ikiwa haijakaa kujadili suala hilo.
"Yalikuwa ni maamuzi ya Mwenyekiti pekee yake kwa haya mambo mawili. Hakuna kikao kilikaa kamati kuu kumwalika Rais Samia au kumpa tuzo," alisema Lissu, akimtaka Mwenyekiti Mbowe kuhojiwa kwa nini alitoa tuzo hiyo na kumleta Samia, wakati chama cha CCM kilikuwa hakijakubali chochote kuhusu maridhiano kati ya pande hizo.
Lissu amekumbusha kwamba masharti ya mwanzo ya maridhiano kati ya CHADEMA na Serikali yalikuwa na vipengele maalum, na kwamba anajiuliza ikiwa hatua ya kutoa tuzo kwa Rais Samia ni matokeo ya maridhiano hayo.?
Tuzo hiyo, aliyopewa Rais Samia Suluhu Hassan, ilitolewa na Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) mnamo Machi 08, 2023, kwa kumpongeza kwa juhudi zake za kuboresha na kuimarisha demokrasia nchini, huku akihusishwa na amani, upendo, na mshikamano.
Tuzo hiyo ilikabidhiwa kwa Rais Samia na Mwenyekiti Freeman Mbowe kwa niaba ya BAWACHA wakati wa Kongamano la Siku ya Wanawake lililofanyika mjini Moshi.
Makosa ya kisarufi na kifasihi yanayojirudia ni uthibitisho wa " slow learning".Mimi nilishatoka huko uelewi somo tu. A/H sio kigezo cha akili.
Jenga hoja
Huna uwezo tulia pembeni.
Kwa nini Lisu hajuongea wakati huo ?Wadau hamjamboni nyote?
Jisomeeni wenyewe hapo chini kwa kiswahili
Jambo TV
Akizungumza kupitia mtandao wa Clubhouse usiku huu, Lissu ameeleza kuwa Rais Samia alialikwa na Mbowe kushiriki katika mkutano wa Baraza la Wanawake la CHADEMA (BAWACHA), na walijulishwa tu kuwa mwaliko huo umetoka kwa Mwenyekiti.
Ameongeza kwa kusema kuwa, walishangaa kuona tuzo ikitolewa kwa Rais Samia bila kujulishwa mapema, huku kamati kuu ya chama hiyo ikiwa haijakaa kujadili suala hilo.
"Yalikuwa ni maamuzi ya Mwenyekiti pekee yake kwa haya mambo mawili. Hakuna kikao kilikaa kamati kuu kumwalika Rais Samia au kumpa tuzo," alisema Lissu, akimtaka Mwenyekiti Mbowe kuhojiwa kwa nini alitoa tuzo hiyo na kumleta Samia, wakati chama cha CCM kilikuwa hakijakubali chochote kuhusu maridhiano kati ya pande hizo.
Lissu amekumbusha kwamba masharti ya mwanzo ya maridhiano kati ya CHADEMA na Serikali yalikuwa na vipengele maalum, na kwamba anajiuliza ikiwa hatua ya kutoa tuzo kwa Rais Samia ni matokeo ya maridhiano hayo.?
Tuzo hiyo, aliyopewa Rais Samia Suluhu Hassan, ilitolewa na Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) mnamo Machi 08, 2023, kwa kumpongeza kwa juhudi zake za kuboresha na kuimarisha demokrasia nchini, huku akihusishwa na amani, upendo, na mshikamano.
Tuzo hiyo ilikabidhiwa kwa Rais Samia na Mwenyekiti Freeman Mbowe kwa niaba ya BAWACHA wakati wa Kongamano la Siku ya Wanawake lililofanyika mjini Moshi.
Na lissu kasema kwa sababu kaulizwa kuwa mlimpa tuzo kuheshimu kwa uwongozi uliotukuka asingeulizwa asingeleta hiyo hojaMimi nilimshangaa sana Huyu mama kupewa tuzo wakati kafanya madudu mengi tu ambayo Kila mtanzania mwenye akili timamu anayajua
ni upumbavu wa kiwango cha juu sana mlimwalika wenyewe mkampa na tuzo mnachoma vitenge ili iweje? mnaonekana mburula tu
Nyerere na baba wa taifa hili alikikubali ichi chama kwamba kinaweza kuwa mbadala wa ccm , hatutakiwi kukichukia ,ilaNani kawafundisha ukorofi hawa ?
Akiwa yeye na nani? Maana maamuzi huwa yanatolewa na vikao vya kamati kuu kamati kuu haijatia baraka zake halafu unasema hoja nyepesi..hii hoja ni rahisi sana kuijibu.
..Mbowe anaweza kusema tuzo ililenga kumuonyesha Samia nia njema waliyokuwa nayo Chadema kuhusu maridhiano.
..Na kwamba tatizo sio yeye, bali Samia na Ccm ambao wamejibu matendo mema ya Chadema kwa ubaya.
..kuanza kumlaumu Lissu, na baadhi kumtukana, kana kwamba tunafurahia matunda ya maridhiano, na 4R, ni kutokujua kujibu hoja.
Akiwa yeye na nani? Maana maamuzi huwa yanatolewa na vikao vya kamati kuu kamati kuu haijatia baraka zake halafu unasema hoja nyepesi
Ndio maana sasa watu wanasema mwenyekiti bado ameganda kwenye siasa za kikwete wakati ccm uko haipo tena..sidhani kama Mwenyekiti alikuwa na nia mbaya.
..Wabaya ni Samia na Ccm ambao wameitikia wema wa Chadema kwa ubaya.
Sasa wewe hapo unaona kipi cha kuuliza swali kama hilo. Hukuelewa maelezo yaliyo tolewa?Bado unaamini huyu mtu anafaa kuwa mwenyekiti wa chama.
Predictable na wenzake wa clubhouse.
Kwa hali iliyo jifunua hadi hapa tulipo fikia sasa, Mbowe hana tofauti yoyote na hao wa CCM. Ni mshiriki anaye juwa kinacho fanyika..sidhani kama Mwenyekiti alikuwa na nia mbaya.
..Wabaya ni Samia na Ccm ambao wameitikia wema wa Chadema kwa ubaya.
Hafai kuwa kiongozi wa juu huyu banamdogo ana nongwa
Itabidi uongeze dua zako, Tundu Lissu aongoze CHADEMA; maana naona ndiyo unadhani itakuwa nafuu kwa huyo mnaye nyonya uchafu wake huko CCM.Hivi Jamaa wa hivi atakuwa asset au liability huko Chadema?
Chadema mchagueni huyu tuone Chadema itakuaje .
Nina uhakika Lisu akiwa Mwenyekiti wa Chadema ACT ndio itakuwa rasmi chama Kikuu Cha Upinzani
Walau nimesikia alichoongea.Sasa wewe hapo unaona kipi cha kuuliza swali kama hilo. Hukuelewa maelezo yaliyo tolewa?
Au tuseme, kwa maana yako wewe, Mwenyekiti wa chama anayefaa kwa sifa unazo zijuwa wewe ni anaye shabihiana na huyo anaye elezwa katika taarifa hiyo iliyo andikwa hapo? Anaye jifanyia tu mambo bila kushirikisha viongozi wenzake?