Lissu : Naikubali dhambi ya kushiriki kumfanya Lowassa kuwa mgombea wa CHADEMA 2015

Lissu : Naikubali dhambi ya kushiriki kumfanya Lowassa kuwa mgombea wa CHADEMA 2015

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Mgombea nafasi ya mwenyekiti wa CHADEMA ndugu Tundu Lissu, jana katika mdahalo uliorushwa na Star TV ukiongozwa na mwandishi wa habari Chief Odemba. Alisema kuwa anaikubali dhambi ya kushiriki kumfanya Lowassa kuwa mgombea wa CHADEMA mwaka 2015.

Maneno hayo yalitokana na swali aliloulizwa na Nyanda kuwa, CHADEMA ilimuita Lowassa fisadi kwa miaka saba, lakini cha ajabu chama hicho kikamfanya kuwa mgombea wa urais wa chama hicho na Tundu Lissu akiwa mshiriki mkubwa ndani ya chama katika kufanya hilo.

Lissu akajitetea kuwa dhambi hiyo yeye anakubali kuibeba, ila akaendelea kujitetea kuwa Kiukweli kabisa yeye na Mnyika walikuwa ni watu wasiomkubali Lowassa kabisa isipokuwa Walifichwa kuhusu Ujio wake mpaka dakika ya mwisho kabisa ya Ujio wake.

Walikuja kuambiwa kuwa Lowassa anaingia CHADEMA kuwa mgombea siku moja kabla ya mkutano wa kamati kuu. Na kwenye mkutano wa kamati kuu Majority ya Wajumbe waliunga mkono Lowassa kuingia CHADEMA na kuwa mgombea. Akasema na yeye akaamua kwenda na wengi. Hata hivyo amekiri dhambi hiyo.
 
Hapa ndipo nilipo ona siasa za bongo sio za kuzichukulia serious.
Ulaghai ni mwingi sana. Kwamba mmeambiwa lowasa anakuja, na atakuwa mgombea urais siku moja kabla ya kamati kuu kukaa, kwanini hakuhoji huo ugombea lowasa alipewa na nani kama kamati ilikuwa haijakaa.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Bado hawajasema.Mtasema ukweli safari hii.Jini kashatoka kwenye chupa.Kumrudisha sio rahisi.Kila mmoja atasimulia makosa yake.
 
Tumbo street, kwa hiyo anataka kusema mzee Slaa alikuwa sahihi kuliko majority
Kuna mambo hawawezi kuyasema, lowasa alinunua ugombea urais, na lissu ni mmoja wa waliopokea gawio kwenye pesa ya lowasa.
 
  • Kicheko
Reactions: Tui
Back
Top Bottom