Kipo chanzo kimoja cha habari kilisema kila lita moja ya mafuta kodi ya Serikali ni 540/=wadau wenye habari zaidi tusaidieni ili tupate majibu kwa usawabusara basi! Unajua kodi kwa lita ni sh ngapi? Mbona landlocked countries jirani na sisi bei chini?
Kipo chanzo kimoja cha habari kilisema kila lita moja ya mafuta kodi ya Serikali ni 540/=wadau wenye habari zaidi tusaidieni ili tupate majibu kwa usawa
Tatizo tulilonalo watanzania ni kwamba hatuna sera yoyote ya kupambana na mfumuko wa bei. Hivyo tunajiendea hovyo hovyo tu tofauti na nchi nyingine. Chombo kikuu serikalini cha kupambana na inflation ni benki kuu ambayo maelezo yote inapewa kutoka wizara ya fedha.
Tatizo tulilonalo watanzania ni kwamba tunapenda sana bidhaa za nje kuliko za nyumbani, bic ya kuandikia, chaki za kuandikia na madaftari vyote hutoka nje ya nchi na vikifika nyumbani bei yake huwa juu sana kulingana na ushuru wa forodha na kodi kadhaa baadaye. Nakubali bidhaa zetu za ndani wakati mwingine hazina ubora wowote wa kushindana na bidhaa za nje, hivyo basi mwathirika mkuu wa mfumuko wa bei ni end user (mtumiaji wa bidhaa) ambapo kimsingi ni mtanzania. Madhara mengine kwa ufupi ni pamoja na kushuka thamani ya pesa yetu, wafanyakazi kuhaha na kutokidhi mahitaji yao kwa kuwa inflation haiendani na nyongeza katika mishahara yao na hii ni indication kwamba uchumi wetu ni wa hovyo.
Nini kifanyike? Tuandae sera mahsusi na maalum kwa ajili ya tatizo hili na ifanyike control ya kila wiki 6 kufanya tathmini kuona kama sera imefanikiwa au lah!. Rais anaweza kuteau tume maalum kushughulikia zoezo hili na uzuri ni kwamba tunao wasomi wengi ambao wanaufahamu uchumi. Hapa akina Lipumba wana maoni ya kuliokoa taifa letu na matatizo haya. Vinginevyo tutaendelea na inflation itapanda na mwishowe tutakuwa na taifa kama lile la Zaire wakati wa Mobutu au uchumi kama wa zimbambwe, mimi nadhani keshokutwa tutachapisha noti mpya za elfu 20 na elfu 50 kupunguza circulation ya fedha mikononi mwa wananchi. Ni hayo niliyonayo ila naomba wana JF tuchangie maada hii kwa kina...
Sio petroli na diesel tu kila nyanja ya maisha hali ni mbaya sana.Aheri wewe unaye nunua Sh. 2200,mimi hapa nilipo nanunua Sh.2300!Nakubaliana na wewe,we must do something,sio kwa ajili yetu tu,lakini hata kwa ajili ya vizazi vijavyo.Ifike mahali tuseme enough is enough.
Kwani kenya wamefanya nini kupunguza bei ya mafuta?sisi kwa nini hatuwezi?maana hata hiyo kodi hapa tanzania hatuoni faida yake zaidi ya kulipa kesi serikali ilizoshindwa katika mikataba ya hovyo?pia baada ya kuuwawa osama bei soko la dunia imeshuka sana chini ya $100 per barell.
Sio lazima kujibu kila hoja kwa utetezi bila kuwa na uhakika na kile unachoandika. Au posho yako nikwa kila post unayo weka napa jamvini?wewe unajua bei ya mafuta kitika soko la dunia? au ndio kuropoka, kama mafuta yamepanda bei kwa wanaochimba je unategemea nini kwa nchi kama Tanzania.
jamani naomba nilete kilio changu kidogo! hivi huu ugumu wa maisha ni mimi mwenyewe ndo nnao u feel au ni watanzania wote???mbona kila mtu yupo kimya?
yan nimetoka kuweka mafuta saiv nimekuta lita moja ni 2,200 (yes elf mbili na mia mbili) hapo nilipo nasikia hazina haina hela na watu hawajalipwa mishahara. jaman hakuna anaye umia na hii hali mbona kimya???
Naomba msaada jamani hakuna lolote tunawezakufanya ili tubadili hii hali hata bei ya mafuta ipungue?mbona kenya wameandamana imeshuka sisi mbona tunaumia kimya kimya jaman????
Think BIG, kwani kuna hivi karibuni umesikia serikali imeongoza kodi kwenye mafuta? The rest serikali ya Tanzania haimiliki visima vya mafuta....
Hukukosea kujiita Nguli Jabali, mpaka mambo ya hewa chafu yote included, duuuuuh kisa woga. Ngoja CDM watishe maandamano, utasikia JK akilalama kama vile haoni.Kenya imekuwa rahisi si kwa vile wana viongozi bora la hasha wana wananchi wenye msimamo na wasiodanganyika, wale kubeba mapanga na kumgeuza mtu bucha ni kitendo cha sekunde. Na mgomo wao ule ungeelekea kumtoa presdaa wao madarakani akasoma alama za nyakati na akakumbuka lile timbwili la 2008 akashusha bei haraka. Hapa kwetu ni ngumu wananchi sisi tu waoga sana tukiandamana kikija kifaru tunazimia wote wengine wanaachia mpaka hewa chafu shauri ya woga wa kirungu na maji ya kuwasha. Hii nchi labda tuzaliane kwa wingi na waarabu tuondoe hii damu ya kimdebwedo.
Wanasubiri kupokezana vijiti vya ufisadi kwa hiyo uvumilivu unakuwa mkubwa sana, tehe tehe tehe.Hivi mtu ukiwa ccm hata uwezo wa kupambanua mambo unayeyuka?
Kupunguza kodi ya mafuta ya taa na diesel kenya,kutawapunguziaje inflation?...naomba elimu,kwa sababu hii naona kama imekaa kiunazi unazi vile!Majirani zetu Kenya wamepunguza kodi katika mafuta ili kuwasaidia wanunuzi na pia kupunguza ongezeko la mfumo wa bei (Inflation) lakini hii Serikali yetu ya kisanii hadi hii leo haijatoa tamko lolote lile kama itapunguza kodi katika bei za mafuta ili kuwasaidia watumiaji na kupunguza inflation. EWURA ni mzigo mwingine kwa Watanzania ambao hauna manufaa yoyote yale.
jaman hakuna anaye umia na hii hali mbona kimya???????
Imeshuka kwa 10% lakini EWURA hawana habari, Ila ikipanda tu, utawasikia wanapandisha bei!
Unatumia gari gani? ishi kwa wakati mwenzio mie nina ka cororola haka lita kumi siku tatu! tatizo mnajitutumua na madude makubwa alafu unalia mafuta. Uza gari lako na nunua Bajaji chupa ya soda utapiga misele wiki moja. Upo hapo! hacha kulia ndo hali halisi nenda mashariki au magharibi. Kwanza badilika mwenyewe mpaka tutakapo anza chimba mafuta yetu ndo mnunue hayo ma VOGUE!
wewe unajua bei ya mafuta kitika soko la dunia? au ndio kuropoka, kama mafuta yamepanda bei kwa wanaochimba je unategemea nini kwa nchi kama Tanzania.