Live Orientation: kwa wale wa UDSM

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Kwa mwaka wa kwanza wote ambao mwaka huu wataitwa 'Tindikali' kama sisi tulivyoitwa 'Tsunami' mwaka 2005,wanaweza kuniuliza jambo lolote kuhusu UDSM ilimradi tu liwe la kumjenga na kumuimarisha muulizaji.

Karibuni!
 
Mkuu the choosen,

Awali ya yote nikupe pongezi kwa kutumia muda wako na raslimali kuja kutoa mwanga kwa vijana kuhusu chuo chao UDSM.

Kama kweli vijana watatumia fursa hii na kuuliza mambo mbalimbali, ni ukweli usio pingika kuwa vijana watakuwa na taarifa nyingi na za muhimu kuhusu chuo chao.

Nitoe wito kwa vijana wote wa mwaka wa kwanza watarajiwa; ni vyema mkaichangamkia hii fursa kwa kuuliza maswali, chuo kikuu kuna changamoto nyingi sana, hivyo ni wakati wenu huu kuuliza ili mtambue ni namna gani mtapambana na changamoto za chuo na kufanikiwa kuhitimu ili muweze kufanikisha ndoto na malengo yenu.

Ni hayo tu vijana.
 
Last edited by a moderator:
Asante Mkuu
 
1Wakati wa kuripoti hapo napaswa kuja na kiasi gani cha fedha ili nilipe malipo ya direct?2.Nikilipia pesa ya accomodation,je nitapata room baada ya muda gani?
 
1Wakati wa kuripoti hapo napaswa kuja na kiasi gani cha fedha ili nilipe malipo ya direct?2.Nikilipia pesa ya accomodation,je nitapata room baada ya muda gani?
Asante kwa swali lako zuri.1. Kiasi cha fedha cha kuja nacho chategemeana na daraja la mkopo utakalokuwa nalo.Mfano,kama una daraja A ambalo ni asilimia 100,huitaji kuwa na kiasi chochote cha malipo hayo. Labda uje na kiasi cha fedha za kujikimu wakati unasubiria mkopo wako yaani fedha za malazi na chakula aka Boom
2. Chuo kina utaratibu wa kupanga vyumba kwa mwaka wa kwanza haraka iwezekanavyo.Hii ni kwakuwa mwaka wa kwanza huwa na asilimia kubwa ya kupata chumba isipokuwa tu kama vyumba ni vichache.Kuna hosteli za Mabibo na za Chuoni pale yaani Main Campus.Hivyobasi,chumba utakipata mara tu baada ya kulipia chumba husika. Hapo ndipo hela zako za kujikimu toka nyumbani zinapofanya kazi njema ya kukuharakishia kupata chumba.Asante
 
Process za kubadilisha course frm computer science to mining engeenering
Swali zuri princess J. Kwanza jua kuwa kozi husika ziko Koleji tofauti. Ya kwanza ipo CoICT na ya pili iko CoET.Lakini,waweza kubadili kozi zako kwa kuandika barua kwa Mkurugenzi wa Shahada za Awali na kujibiwa.Lakini lazima uwe na sifa za kozi husika unayotaka kuhamia.Pia lazima kuwe na nafasi ya wewe kuhamia kozi husika-Mining Engineering.Asante
 
Last edited by a moderator:
Ndugu the choosen katika kujibu swali la thema umesahau swali lake la direct costs ambazo ni medical fee 50000, caution money 20000, DARUSO fee 5000 etc ambavyo havihusiani na mkopo. Kama una bima ya afya ukiionesha basi haulipi hiyo Medical fee.

Mwaka wa kwanza wote watapewa chumba campus na mabibo.
 
Mkuu Mabulangati,asante kwa hilo.Lakini,DARUSO fee hukatwa moja kwa moja na chuo
 
Last edited by a moderator:
Huingizwa kwenye account ya chuo na haihusiani ya bodi ya mikopo, ndiyo maana inaitwa direct cost. Boom anapewa mwanafunzi hivyo chuo hakina access nayo na mwafunzi anasaini kama meals and accommodation allowance.

Hivyo mkuu hiyo ni ya muhimu sana.
 
choosen me nlikua naomba kujua kutoka kwako kuhusu hii course BA in economics ya apo ud coz nasikia kua department yake sio nzur na wanabana sana maksi cjui kuna ukweli ndani yake
 
Mkuu mimi nimechaguliwa Education na ninataka kubadili sasa kuna tangazo wanadai wale wa Education hawaruhusiwi kuhama kozi. Je hii ilikuwepo miaka yote au imeanzia kwetu? Je Inawezekana ikawa ni njia yakupunguza wingi wa maombi ila wanaruhusu chinichini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…