Live Update:Saba Saba trade fair:7/7/2013

King Kong III

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2010
Posts
56,205
Reaction score
79,515
Umofia kwenu wana JF,

Leo ndio kilele cha siku ya maonyesho ya saba katika uwanja wa Mwalimu Nyerere Trade Fair bara bara ya kilwa

Tujumuikeni wote kwenda kusupport wafanyabiashara!!

Angalizo:Kamanda Kova na Mwema tunaomba ulinzi wa kutosha isije ikatokea yale ya A-city,pia wadau mtoe taarifa kwa polisi endapo ukimuhisi mtu asomekisomeki vizuri au ana begi au fuko lililo kaa hovyo hovyo au lisiondena na tukio lenyewe.

Nawasilisha.
 
Kwani JWTZ hawatokuwepo? sina imani na polisi hivyo yeyote atakayemwona polisi haeleweki atoe taarifa wa JW au akimbie fasta kambi ya JKT ipo jirani tuu pale.
 
Njia ya kilwa ipo nyeupe kabisa nipo 77 watu wanaangia ndani,polisi nao wapo kwenye morning call getini.
 
Kwani JWTZ hawatokuwepo? sina imani na polisi hivyo yeyote atakayemwona polisi haeleweki atoe taarifa wa JW au akimbie fasta kambi ya JKT ipo jirani tuu pale.

Jeiwii wapo.
 
Nipo hapa tayari kwenye banda letu la nanihii. Leo atapita hapa Prime Minister. Kuhusu vikosi vya majeshi, ni kwamba vyote vina mabanda humu humu, achilia mbali na Police Post iliyopo hapo nje. Karibuni bidhaa zetu!
 
Watu wenye nia ya kujufunza hutembelea maonyesho siku za mwanzo, leo ni hakuna kitu ni fujo tu, na ukizingatia yale ni magurio na si maonyesho, kuna Docomentary moja nilipewa yenye maonyesho ya biashara kwa zaidi ya nchi 20 kwa kweli bongo hakuna maonyesho that is why unakuta watoto wamejazana humo, Ni maonyesho ya Tanzania pekee unayo weza kutana na haya, na ndo maana hata yale mabanda yenye vitu muhimu vya kujifunza hakuna watu, ila yale mabanda yanayo uza sijui vitu vya urembo na promotion sijui za nini ndo kuna watu nyomi, hata maonyesho ya Kilimo ni hivyo hivyo. Maonyesho ya kilimo unakuta yamejaa taasisi za Serikali ambazo zingine wala hazina uhusiano wa moja kwa moja na kilimo, Ila wako pale kula Posho

Maonyesho ya Bongo yametekwa na kampuni za simu, utakuta mabanda yao kila kona, unaweza zani ni maonyesho ya makampuni ya simu, na kibaya wako mule kuuza simu zao tu na kampuni moja unakuta ina mabanda ya kutosha mule
Ni full usanii, Tantrade wako kimapato zaidi
 
Nasikiliza pinda hapa akihutubia kwenye banda la kawawa
 
Kwani JWTZ hawatokuwepo? sina imani na polisi hivyo yeyote atakayemwona polisi haeleweki atoe taarifa wa JW au akimbie fasta kambi ya JKT ipo jirani tuu pale.

JWTZ wapo mtwara kuwatesa wanaodai haki yao
 
Pinda yupo home shopping center akitembelea banda hilo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…