Live Updates Ndondo Cupu; Kauzu FC VS Kibada

Na Zainab Nyamka, Dar

Timu ya Kauzu Fc imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali michuano ya Ndondo Cup, baada ya kuifunga Kibada Fc bao 1-0 katika mchezo wa robo Fainali iliopigwa jana jioni kwenye Uwanja wa Bandari, jijini Dar es Salaam.

Bao hilo pekee lilifungwa na Rashidi Roshwa, katika dakika za lala salama.



Akizungumza na mtandao huu baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Kocha wa
Kauzu Fc Mashaka Said, alisema kuwa wamefurahia matokeo hayo na kutinga
Nusu fainali mwaka huu ba kusema kuwa wanajipanga na maandalizi ya
kutosha ili waweze kuchukua hasa baada ya mwaka jana kufungwa na
waliokuwa mabingwa Faru Jeuri.
 
UKIFIKA TANDIKA AIDHA MWEMBE YANGA AMA KITUO
Game inapigwa uwanja upi Mkuu?
CHA BANDARI NYOMI SANA KIINGILIO 2000 NA UNAOATA GAZETI LA MWANASPOTI LENYE MATUKIO YA NDONDO TU
 
Kwa hatua hiyo Kauzu wanaungana na timu za Temeke Market, Makumba Fc
pamoja na Misosi katika hatua ya nusu fainali inayotarajia kuwa
mwishoni.mwa wiki ijayo huku Kauzu wakitarajiwa kuvaana na Misosi kwenye
hatua hiyo.





Katika michuano hiyo ya Ndondo Cup kumekuwa na matukio mengi na ya kila
aina huku pia ikisheheni wachezaji wengi wa Ligi Kuu wanaozichezea timu
zao za mitaani, ambapo katika mchezo wa leo uliokuwa mkali na kusisimua
uliweza kuwavutia mashabiki wengi wa soka waliopata burudani murua
kutoka kwa baadhi ya wachezaji wa Ligi kuu.
 
UKIFIKA TANDIKA AIDHA MWEMBE YANGA AMA KITUO

CHA BANDARI NYOMI SANA KIINGILIO 2000 NA UNAOATA GAZETI LA MWANASPOTI LENYE MATUKIO YA NDONDO TU
Mmmh, Mkuu ni Mwanaspot wenyewe au ni la wajanja tu ili wapige pesa.
 
Mmmh, Mkuu ni Mwanaspot wenyewe au ni la wajanja tu ili wapige pesa.
MWANASPOTI NI SEHEMU YA WADHAMINI WAKITOA 300000 KWA MSHINDI NA 200000 KWA MSHINDWA NA 50000 KWA MAN OF THE MATCH
 
MICHEZO INAYOKUJA
2016-07-23
16:00 MAKUMBA Vs Temeke Market

2016-07-24
16:00 MISOSI FC Vs KAUZU FC
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…