Liverpool inabebwa, goli la Salah offside waziwazi

Nimeamini Liver inabebwa goli la Salah dakika ya majeruhi offside ya wazi kabisa.

Ngusero
Basi tunafuta hilo goli tunampa Martial na assist ya Alisson Becker tunampa Jesse Lingard.
Na Man of the match (MOT) tunampa (mwamuzi wa pembeni + VAR) kwa kukataa goal la Firmino sababu Degea kamfuata VvD kwa nyuma kamgusa makusudi.
 
Scenario nyingine ambayo mchezaji anaweza kuwa ahead ya last-but one defender na isiwe offside ni kama pass imetokana na mpira wa kurusha(throw in) au pigo la kona (corner kick)

Sent using Jamii Forums mobile app
Throw-in haina offside. Corner kick phase one haina offside kwasababu mpigaji anakuwa kwenye mstari ila ikiokolewa ikarudi offside rule ina apply kama kawaida.
 
Sasa kumbe ushajijibu mwenyewe.

Kama De Gea alikua nje ya 18, anahesabika kama Last Defender, angalia na Mo Salah alikuwa wapi!!

Halafu bado unakataa kipa kuwa nje ya 18 sio sababu ya OFFSIDE.

Kwa kifupi majibu A na B ni sahihi.
 
Malcom hayupo sahihi mzee hakuna sheria ya hivyo,
Ngoja nikuongezee maarifa mjomba.

Kipa anapokuwa nje ya 18 yake anaruhusiwa kudaka?

Jibu ni kwamba hawezi. Sababu ni kuwa kipa anamiliki sifa ya ukipa anapokuwa ndani ya 18. Anapotoka nje ya 18 tu, hahesabiki kama golikipa. Hapo anakuwa sawa na beki (Last Man).

Kwahiyo ukishakubali kuwa kipindi Allison anapiga mpira, De Gea alikua nje ya 18, urudi sasa kwenye maelezo ya hapo juu.

Ukikaza kichwa hutoweza kuelewa hata kidogo.
 
Mzee weka sheria ya offside hapa tuisome
 
Wewe mwenyewe hujui Sheria za mpira. Offside applies on opposition half. Salah alikuwa kwenye half yao wakati mpira umerushwa/umepigwa.
Sahihi sana nilitaka nisikoment kitu baada ya huyo mtu kudanganya hapo. Ukweli ni huu ulosema
 
Mzee weka sheria ya offside hapa tuisome


Keywords: last but one defender is usually but not necessarily a goalkeeper. Kipa ni mchezaji kama mchezaji mwingine when it comes to offside.

Sasa hawa wenzetu hii habari ya kipa akiwa nje ya 18yard box blah blah wameitoa wapi? Hii niliowafata ni ya Fifa
 
Chukulia mfano foul imetokea pembeni mwa uwanja na linesman/refa wameamua iwe foul na mpira umetoka yaani kama isingekuwa foul ulitakiwa uwe wa kurusha, je mchezaji anaweza kurusha haraka haraka ikichukuliwa kama ADVANTAGE?
Kitendo cha mpira kutoka nje mazingira ya advantage yanakuwa hayapo tena elewa hilo
 
Sasa kumbe ushajijibu mwenyewe.

Kama De Gea alikua nje ya 18, anahesabika kama Last Defender, angalia na Mo Salah alikuwa wapi!!

Halafu bado unakataa kipa kuwa nje ya 18 sio sababu ya OFFSIDE.

Kwa kifupi majibu A na B ni sahihi.

Bro nakushauri nyamaza unatutia aibu hata sisi.

ELEWA HAYA:

- Goalkeeper: Ni mchezaji kama wachezaji wengine, linapokuja suala la offside sharia haitambui kitu kinachoitwa Goalkeeper bali inamtambua kuwa ni mchezaji kama wachezaji wengine.


VIPI MCHEZAJI ANAHESABIWA KUWA OFFSIDE?

- Ni pale awapo katika Half ya Pitch ya Wapinzani iwapo:-
1) Amebakisha mchezaji mmoja tu wa upinzani mbele yake! Si lazima mchezaji huyo awe Goalkeeper, hata kama Goalkeeper ametoka golini na akabakia Beki au Kiungo au Mshambuliaji pekee.

2) Mbele yake hakuna mchezaji hata mmoja wa upinzani, Mfano Timu nzima akiwemo na Goalkeeper wameenda kushambulia kwa kupigwa Corner then Mshambuliaji akawa ameshavuuka Half pitch ya Upinzani na ukapigwa mpira mrefu ukamfika akiwa peke yake mbele hakuna mchezaji wa upinzani yeyote.

VIPI MCHEZAJI ANAKUWA SI OFFSIDE?

√ Iwapo yupo Half Pitch ya Opponents wake lakini mbele yake kuna wachezaji kuanzia Wawili (au zaidi).

Hao Wachezaji Wawili wanaweza kuwa BEKI na KIPA.
Si lazima Kipa awepo, inawezekana Mabeki Wawili pale iwapo Kipa ametoka kwenda kujaza Kona.

NOTE:
Ni kosa kuamini kuwa Offside inahesabika kufa kwa kuwepo Beki mmoja! Pale hapahesabiki Beki, Bali panahesabika kuwa kuna wachezaji Wawili (Beki na Kipa).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…